Baada ya kaburi la kiyeuyeu kuhamishwa...

Wewe Lokissa, ni mbumbumbu wa maandiko, na wala humjui Yesu! Unajua miujiza aliyoifanya Eliya wakati alipokuwa anapambana na Wafalme? Hujui! Ngoja nikupe darasa! Soma katika Biblia, miujiza ya Eliya, alipokuwa akipambana na Mfalme Ahabu (1WAFALME 17:1; YAKOBO 5:17-18), na pia alipokuwa anapambana na Mfalme Ahazia (2WAFALME 1:1-18).

Unasema eti Kakobe aheshimu mamlaka "halali"! Mamlaka "halali", inayopingana na Mungu? Unajua kwamba, Yesu huyo, (unayefikiri unamjua) alimwita Mfalme Herode, "MBWEHA"? Hujui! Soma LUKA 13: 31-32, utaona! Unajua kwamba Meshaki, Shadraka na Abednego; walipingana na mamlaka ya Mfalme Nebukadreza, unayoiita wewe "halali"? Walipotupwa kwenye moto, unajua kwamba, "mtu wa nne", alikuja kuwatetea? Huyo, hakuwa "mwana wa miungu", bali Mwana wa Mungu, Yesu Kristo (DANIELI 3:1-30). Ilikuwaje basi Yesu, kuwatetea watu ambao "hawakuheshimu mamlaka halali", kama unavyodai? Kwenye maandiko, wewe bado ni chekechea! Kaa chini, ujifunze! Hujui neno lolote bado! (1WAKORINTHO 8:2).

Eti Kakobe asubiri kuaibika! Lini tena? Pole, bado unasubiri wa kuaibika, hadi sasa? Baada ya MIAKA MIWILI, wa kuaibika, amekwisha kuaibika tayari! Ni yupi? NI SERIKALI! Serikali iliyotumia bunduki, kung'oa mabango, kwa mbwembwe nyingi, ili kupitisha HARAKA, umeme wa 132 KV kwa ubabe, imeshindwa kuupitisha hadi leo, MIAKA MIWILI SASA! Hata kama leo Serikali ingefanikiwa kuupitisha umeme huo, IT IS TOO LATE! Bado tutawauliza, kwa nini imechukua MIAKA MIWILI? Kushindana na Mungu, na Watumishi wake, HAKULIPI! Serikali ijifunze kumuheshimu Mungu, na kuwaheshimu Watumishi wa Mungu!


Big Up gumegume, kwa kumkomesha Lokissa, na blabla zake za "kuheshimu mamlaka halali". Mamlaka "halali", inayoiba kura, ili kuendelea kuwepo madarakani? Serikali ya namna hii, ina uhalali upi? Shame upon you, MAGAMBA!
 
Hakuna lolote lile,nguvu za uchawi zimezidiana tu,wa-JAPAN wachawi lakini kakobe ni kubwa lao. Utasema nini kuhusu reli zilizogoma kupita mbuga ya Tsavo kenya?Mara ngapi wakandarasi wanang'oa miti mikubwa ya matambiko au kubomoa nyumba fulani then kesho yake asubuhi wanaukuta ule mti umeshamiri pale pale au nyumba imesimama imara pale pale na bibi mwenye nyumba yuko nje anasaga ugoro bila wasi wasi?.


Jaguar, umekiri kwamba Kakobe ni kubwa lao! Safi sana, hata kama unatumia lugha ya ovyoovyo! Wajapan wamesalimu amri, siyo! Wamekutana na "Baba wa Sayansi", kama anavyosema Kakobe!

Baada ya Farao na wachawi wake, kushindwa kupambana na Musa, aliomba Musa amwombee baraka. Vivyo hivyo, baada ya Simoni mchawi, kushindwa kupambana na Filipo, na Mitume; aliomba Mitume wamwombee. Acheni kupambana na Mtumishi wa Mungu! Hakuna faida yoyote! Kama Farao, mwombeni Kakobe, awaombee baraka!
 
Serikali ingefanya kulitunza hilo kaburi ingekuwa moja ya kivutio ambacho kingetuletea fedha za kigeni ila kutokana na wamelala kila kitu kinaendelea kulala hivyo hivyo
Ni vigumu kutunza maajabu ya Shetani.Unakumbuka Tiba ya maajabu Babu Loliondo?Serikali ilishindwa kumuhamishia Arusha mjini ilikuepusha vifo lakini mizimu yake ikamushauli aende kwenye maeneo wanapozikwa Wafu.Wataalamu wa Dawa duniani walianza utafiti ili kuanda dawa hiyo ktk vidonge mizimu ya Babu ikakataa.
 
Big Up gumegume, kwa kumkomesha Lokissa, na blabla zake za "kuheshimu mamlaka halali". Mamlaka "halali", inayoiba kura, ili kuendelea kuwepo madarakani? Serikali ya namna hii, ina uhalali upi? Shame upon you, MAGAMBA!
Umemuona Kikwete kwenye gzt mwananch leo? Amevaa gamba yupo Uswisi,ila Gamba la Prof Magembe limenitisha kidogo!
 
Mkuu umekuwa na wazo zuri sana ambalo serikali yetu haijawahi kulifikiria ambapo hapo pangetupatia pesa za kigeni nyingi na kilichotakiwa kukifanya pale ni kulitangaza tu neema ingetujia

Mbona pointi zako za kitoto sana??kidato cha pili wewe..??
 
Wangekuwa wazungu mngesema miujiza..! Kwa kuwa imetokea Afrika basi ni nguvu za giza..Tubadilike,tuheshimu tamaduni zetu.
 
Jamani kuna jamaa wa iringa ninafanya naye kaz,ni mjukuu wq kiyeyeu anasema waliohusika kuhamisha kaburi la kiyeyeu wote wamekufa mmoja baada ya mwingine,kuanzia aliyechimba kaburi,mpaka aliyekaa kikao na kukubaliana kuondoa makaburi
 
Wakati ujenzi wa barabara kipande cha Iringa-Mafinga ukiendelea,Tanesco nao wamekuwa na zoezi la kurekebisha mpangilio wa nguzo zao.Kwa wanaokumbuka pale mahali palipokuwa na kaburi la kiyeuyeu ambapo nguzo na nyaya za tanesco zilikwepeshwa,hivi sasa Tanesco wameunga umeme straight kupita juu ya lile eneo lilipokuwepo kaburi la Kiyeuyeu.Ninachojiuliza;Ina maana ni kweli Tanesco hapo mwanzo walilikwepa lile eneo kwa kuamini nguvu za giza?,Kama si kweli,je ni kwanini baada ya makaburi kuhamishwa na wao ndo wameamua kupitisha nyaya zao umeme pale mahali?
Nitoe masahihisho ni Kiyeyeu. Hakuna ukweli wo wote kuhusu nguvu za giza kuzuia umeme. Natokea hizo sehemu, kilichotokea ni kwamba wakati ilipogundulika kuwa nyaya inabidi zipite juu ya makaburi hayo lilizuka suala la fidia kwa ndugu wa marehemu hao ili makaburi yahamishwe. kwa kuwa nguzo zilikuwa tayari zimefika hapo, kilichoamuliwa ni kuikwepa sehemu hiyo. Walitafuta the cheapest solution to what was an impediment to the project. Mambo ya nguvu za giza ni porojo tu zisizo na mashiko yo yote.
 
Jamani kuna jamaa wa iringa ninafanya naye kaz,ni mjukuu wq kiyeyeu anasema waliohusika kuhamisha kaburi la kiyeyeu wote wamekufa mmoja baada ya mwingine,kuanzia aliyechimba kaburi,mpaka aliyekaa kikao na kukubaliana kuondoa makaburi


Mh jaman ya kweli haya?

Maana habar yenyewe ya huyu kiyeuyeu tangu january 2012

So mpaka leo nov 2013 ni kiyeuyeu tu?
Hehehe........
 
Acheni uzushi bana

Hakuna kiyeuyeu wala kiyuiyui

Habari za mwaka 2012 january ndio mnatuletea leo!!

Mmekosa cha kujadili ama !!
 
Na huenda watasema gharama halisi ya kulihamisha kaburi hilo yakiwemo maisha ya waliyoshiriki kulihamisha!!

Na hii ndio habari niliyosimuliwa Iringa. Wanasema Tanesco wali propose fidia ndogo sana kwa makaburi yote matatu ya akina Kiyeyeu, hivyo wenye ukoo wakagoma kupokea hiyo fidia kwa sababu ilikuwa haitoshi kwenda kununua plot maeneo mengine na kuhamisha masalia ya miili ya wapendwa wao. Kwa kuwa Tanesco walikuwa na haraka na mradi, option ikawa ni kukwepesha nguzo ili zisipite juu ya makaburi. Ukitaka kuamini hilo, Tanroads waliwalipa fidia hao akina Kiyeyeu na makaburi yakahamishwa tar 30.12.2010 na mpaka leo kila kitu kipo OK kabisa.
 
haha Tanzania bana..huku Simiyu kuna uchawi balaa..waalimu wanataka kuhama kufundisha shule fulani maana wamebandika maharage jikoni akienda kufunua kuongeza maji anakuta nyama ....anakula ugali na mchicha asubui anakuta kuna mifupa ya kuku mezani...kudadadeki
 
Back
Top Bottom