Azimia kuacha kuangalia video/picha za ngono 2023

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Aug 6, 2020
3,520
6,503
Watu Wana malengo mengi Sana kila mwaka mpya ukianza na mengine ni Makubwa mno hata hayatekelezeki hata katika ndoto kwasababu hakuna ajuaye kesho yake, ingawa hii haitufanyi tusiache kuweka malengo.

Ndugu zangu ili tufanikiwe basi tunahitaji Sana msaada wa Mwenyezi Mungu, kwani si akili zetu pekee au ujanja wetu ambao unatuwezesha kutimiza malengo yetu pasina msaada wake.

Lakini tutakuwaje karibu na Mola wetu wakati kila siku tunaangalia mambo ya haramu?

Na mambo hayo ndio hutuhamasisha zaidi kufanya zinaa, kwasababu porn ina kawaida ya kumfanya mtu apate matamanio ya Hali ya juu na mwisho wake anaishia kuzini.

Porn ndio inayohamasisha watu kufanya mapenzi kinyume na maumbile, watu wengi sana siku hizi kutokana na kuathirika na video za ngono katika mitandao wamejikuta ni wahanga wakubwa wa kutaka kujaribu mambo ambayo huyaona huko katika porn.

Tubadilike ndugu zangu porn zinatuweka mbali na utukufu wa Mola wetu, kuangalia utupu ambao sio WA mume wako au mke wako ni haramu na INA mchukiza Sana muumba wetu.

Lakini hata ukija katika mazingira ya kawaida Tu, porn huwafanya watu kuwa tegemezi kwenye ngono, yaani hata akiwa na mkewe au mumewe ndani basi hawezi sisimka mpaka avute hisia za kwenye porn ndio aweze kupata hamasa na hamu ya Kula tunda na mwenza wake,je huo sio utumwa WA hisia?

Na humpunguzia hamu ya kuwa na mwenza wake pia, just imagine kila siku unaangalia utupu wa wanawake wangapi tena wa Aina mbali mbali, matokeo yake hata mkeo akiwa mtupu faragha na wewe hakuna kipya kwake kwasababu unaangalia za walatino, wabrazil, wachina, wahindi na listi inaendelea.

Vile vile porn iko na uraibu mkubwa Sana, yaani unakuwa Teja kiasi ambacho ukiwa Peke yako unatamani kuangalia huo uchafu, kuna mtu siku moja alionwa anaangalia porn ndani ya daladala, ebu just imagine mpaka unafikia kuangalia hayo madudu katika usafir WA umma ujue wewe tayar ni Teja la 5G.

Nadhani mnakumbuka Kule mjengoni kuna mbunge alionekana katika cctv camera yupo bungeni watu wanachangia mijadala lkn yeye anaangali porn.

Huu uraibu ni mbaya Sana,na ndio huwafanya watu kujichua kufanya masterbation na matokeo yake baada ya Mda mishipa ya uume hulegea na kuwafanya vijana kukosa nguvu za. Kiume.

Kuacha Kuangalia Porn ni Vita kubwa kuliko hata ya mrusi na Ukraine,inahitaji upambane haswa kushinda hizo temptation za kuangalia hayo madudu na hasa kama umekuwa na uraibu mkubwa.

Utaepuka mambo mengi Sana yenye kuzuru nafsi yako na mwili wako kama utafanikiwa kuacha kuangalia porn movies.

Weka Nia thabiti na azimia kwa nafsi yako na moyo wako wote kuwa no mor e porn 2023.

Mungu awabariki Sana.

Nawapenda Sana.

Kutoka kwangu ETUGRUL BEY

Ni hayo Tu!
 
Nashukuru huu uraibu nimeushinda kwa siku hizi na ninaomba nisije kurudi nyuma
Screenshot_20230104-234204.jpg
 
Unaazimia kuacha kuangalia ile unaingia Twitter unakutana na thread za watoto wameshalala, ukienda insta unakuta mademu wanatwerk, ukienda Telegram unakutana na group au channels za pisi kali.

Basi unasema unazima data jirani yako anakutega makusudi tu. Au umelala usiku unasikia chumba cha jirani mwanachuo kaleta demu.

Mradi tu na wewe ufanye dhambi zisizo za lazima
 
Back
Top Bottom