Awamu ya Zanzibar kutuletea mgombea urais

Awamu ya Zanzibar kutuletea mgombea urais

Wazanzibar sasa ni wakati wenu kututolea mtu wa kuendesha hili lori TANZANIA maana kila kukicha ni bara tuuu ina maana wazanzibar nyie hamna uwezo wa kutoa mtu wa kusimama kidete?

Kwa kuwasaidia tu anzeni kumuandaa mtoto wa mzee Mwinyi aje kupeperusha kwa niaba ya wazenji.

Miaka hii mitatu inatosha kujiandaa.
Hilo lingewezekana endapo na zanzibar ingekuwa
tayari kupata rais kutoka bara awe rais wa zanzibar,kama hili haliwezekani
basi tutabaki kuwaenzi wazee wetu Nyerere na Karume
mengine tuyaweke kapuni kama azimio la arusha,kila mtu aendeshe kwake
maana kila mtu ana bendera,jeshi,wimbo wa taifa na bunge.
 
Lini na sisi tutawapelekea mgombea kule kwao? Ujinga huu hata Nyerere hakuukubali na ndio maana haujaandikwa sehemu yoyote. Haikuwa bahati mbaya.
 
Wazanzibar sasa ni wakati wenu kututolea mtu wa kuendesha hili lori TANZANIA maana kila kukicha ni bara tuuu ina maana wazanzibar nyie hamna uwezo wa kutoa mtu wa kusimama kidete?

Kwa kuwasaidia tu anzeni kumuandaa mtoto wa mzee Mwinyi aje kupeperusha kwa niaba ya wazenji.

Miaka hii mitatu inatosha kujiandaa.
Hata akitoka Zenji bado atakuwa ni sisiemu, chadema bado sana!
 
Sifikirii kama Zanzibar ina shauku la kutaka kutoa raisi wa Tanzania,Zanzibar kuna vuguvugu kubwa la kutaka mamlaka kamili...
 
Wazanzibar sasa ni wakati wenu kututolea mtu wa kuendesha hili lori TANZANIA maana kila kukicha ni bara tuuu ina maana wazanzibar nyie hamna uwezo wa kutoa mtu wa kusimama kidete?

Kwa kuwasaidia tu anzeni kumuandaa mtoto wa mzee Mwinyi aje kupeperusha kwa niaba ya wazenji.

Miaka hii mitatu inatosha kujiandaa.
miaka 3 tu umechoka aha ama kweli
 
Wazanzibar sasa ni wakati wenu kututolea mtu wa kuendesha hili lori TANZANIA maana kila kukicha ni bara tuuu ina maana wazanzibar nyie hamna uwezo wa kutoa mtu wa kusimama kidete?

Kwa kuwasaidia tu anzeni kumuandaa mtoto wa mzee Mwinyi aje kupeperusha kwa niaba ya wazenji.

Miaka hii mitatu inatosha kujiandaa.
Mwalla,
Hii fikra ya Zanzibar kutoa rais mbona hujaiweka vyema?
Umetanguliza gari mbele na punda nyuma.

Itakuwa tabu kuvuta mzigo.

Vipi CCM Zanzibar wafikirie kutoa rais wa Jamhuri ya Muungano ilihali wana tatizo
kubwa la kushinda urais Zanzibar toka uchaguzi wa vyama vingi uanze mwka 1995?

Swali lako labda lingekuwa hivi - ''Zanzibar ifanye juhudi ya kuondoa tatizo la uchaguzi
wa rais ili waweze kutoka mgombea urais wa Jamhuri ya Tanzania,'' au mfano wa hivi.

Vinginevyo utakuwa muhali mkubwa kwa Zanzibar kutoa mgombea urais ambae hawezi
kushinda kwao.

Lakini juu haya yote umeleta jamvini mada nzuri sana ya kufikirisha.
Nasema ya kufikirisha kwani ikiwa hii fikra ipo Zanzibar haiwezi ikawa chanzo ni CUF.

Fikra kama hii itakuwa CCM Zanzibar na wao ili kufikia hatua hii watahitaji kupata kiongozi
kwanza ambae ataweza kuleta umoja wa Wazanzibari wote.

Kwa hali ya Zanzibar ilivyo kwa hivi sasa hii si kazi ndogo.
 
Wazanzibar sasa ni wakati wenu kututolea mtu wa kuendesha hili lori TANZANIA maana kila kukicha ni bara tuuu ina maana wazanzibar nyie hamna uwezo wa kutoa mtu wa kusimama kidete?

Kwa kuwasaidia tu anzeni kumuandaa mtoto wa mzee Mwinyi aje kupeperusha kwa niaba ya wazenji.

Miaka hii mitatu inatosha kujiandaa.
Mtanzania yeyote mwenye sifa ana haki ya kuwa Rais wa nchi hii. Siyo lazima atoke zanzibar maana na Zanzibar ni sehemu ya Tanzania kama ilivyo CHATO, Mtwara, Nkasi n.k
 
Mtanzania yeyote mwenye sifa ana haki ya kuwa Rais wa nchi hii. Siyo lazima atoke zanzibar maana na Zanzibar ni sehemu ya Tanzania kama ilivyo CHATO, Mtwara, Nkasi n.k
Ungekuwa unajua maana ya muungano usingeleta upuuzi wako huu
 
Wazanzibar sasa ni wakati wenu kututolea mtu wa kuendesha hili lori TANZANIA maana kila kukicha ni bara tuuu ina maana wazanzibar nyie hamna uwezo wa kutoa mtu wa kusimama kidete?

Kwa kuwasaidia tu anzeni kumuandaa mtoto wa mzee Mwinyi aje kupeperusha kwa niaba ya wazenji.

Miaka hii mitatu inatosha kujiandaa.


Kama ni Hussein Mwinyi hata mimi nakuunga mkono. Mimi simfahamu binafsi lakini nina rafiki yangu wa karibu ambaye anamfahamu huyo bwana vizuri sana, alikuwa anaongelea mambo mazuri sana kuhusu yeye. Nakumbuka hayo maongezi yalikuwa takribani miaka miwili iliyopita na mimi bila kusita nikamwambia rafiki yangu huyu anaweza akawa rais sikumoja. Rafiki yangu anasema Dk. Mwinyi alikuja hapa Uingereza kusomea shahada ya udakitari lakini kwasababu masomo yake ya awali aliyafanyia Uturuki Waingereza wakawa na shaka na kiwango chake cha elimu wakamwambia arudie level ileile ambayo alikwisha isoma Uturuki kwa kiwango cha hapa Uingereza lakini baadae wakamwacha aendelee na level ya juu kwasababu kila kitu kilikuwa rahisi kwake. Lakini si elimu tu, pia nasikia ni mtu wa busara. Halafu nilivyokuja likizo Tanzania mwaka 2015 nilikuwa naongea na mdogo wangu mambo ya siasa ikaja tena habari ya Dk. Mwinyi. Mdogo wangu akaniambia pale Muhimbili alikuwa ni mchapakazi kweli mpaka baadhi ya madaktari wenzake walikuwa wanamchukia, baadhi yao walikuwa ni wavivu (kama tulivyo Watanzania!). Sasa wakimuona anafanya kazi sana wanasema eti anajifanya anajua. Nasikia alikuwa akimaliza kazi pale Muhimbili haondoki mpaka afanye 'handover' kwa daktari anayefuata wakati daktari mwingine angeondoka na kuacha wagonjwa akawahi kukata kiu kwenye baa.
 
Back
Top Bottom