Awamu ya tano ndio imeleta chuki na kuvunja Umoja wa Kitaifa kwa Watanzania

KISHADA

JF-Expert Member
Oct 18, 2012
2,224
3,290
Huo ndio ukweli. Kuna watu wanazunguka sana kutafuta mchawi wa kinachoendelea hapa Tanzania. Kwa sasa kuna chuki za kisiasa na uhasama uliopitiliza na kuhatarisha umoja wa Kitaifa.

Awamu ya Tano haiwezi kuepuka lawama hizo kwa hoja mbalimbali.
Tukumbuke tu kwamba kwa kiasi hiki cha miaka kama 25 baada ya kuja vyama vingi Tanzania, Utamaduni wetu uliathiriwa kwa kiasi fulani na ushabiki wa kivyama na kutengeneza ushindani wa sera na kufanya chaguzi kupata viongozi mbadala. Hapa paliongezeka kionjo kwenye utamaduni wa Watanzania na kuongeza siasa za kuvumiliana kama sehemu yautamaduni wetu.

Siasa ni sehemu ya Utamaduni wa watanzania lakini ikiendeshwa kwa kufuatwa kanuni zake japo watawala waliopita nao walikuwa na madhaifu yao. Madhaifu hayo yalikuwa ni kama mchezo wa kisiasa na kamwe haikufika mahali kukajengeka chuki kiasi hiki.

Awamu ya tano imevunja utamaduni wa kisiasa uliojengwa wa kuvumiliana na kushindana kwa hoja leo tunaona siasa ya Dola dhidi ya vyama vya siasa.

Vyama vya siasa vimeporwa uhuru wa kufanya siasa za kishindani kwa kuzuiwa kufanya mikutano na maandamano.

Viongozi wa upinzani wananyanyasika kupata haki zao za kisiasa kutoka vyombo vya dola kama Polisi na kuingiliwa shughuli zao kinyume na taratibu na utamaduni wa kisiasa.

Chama tawala kinanufaika na Udola kwa viongozi wake kutumia mwavuli wa Kiserikali kujiimarisha huku wakiacha dhambi hiyo ikiitafuna Taifa.

Huwezi kuamini kwamba Rais na Mwenyekiti wa CCM anafanya kampeni kweupe kabla ya muda kufika kwenye mikutano yake tena na kupigiwa kampeni na wakina Harmonize si msajili wa vyama vya siasa wala Mutungi anayejali. Katika hali hiyo lazima chuki ijengeke.


ATHARI
Wanasiasa wa upinzani, wanahabari, wanaharakati na taasisi za kiraia wote ni wanajamii na wana wafuasi wao, kinachowapata makundi hayo kinaipata jamii vile vile.

Huu mgawanyiko uliopo na kuombeana mabaya NI ZAO LA CHUKI HIYO. Na awamu hii ya tano inahusika.

Makundi mbali mbali yameshaeleza hatari iliyopo na kubezwa na hakuna hatua zinazochukuliwa hadi sasa si viongozi wa serikali si msajili wala viongozi wa dini.

Jamii inazidi kugawanyika, kuombeana mabaya na kuongezeka visasi baina ya watanzania.

NINI KIFANYIKE?

Tunarudia tena kufanywe mjadala wa Kitaifa na kuwakutanisha wanasiasa wote kwa Maslahi ya Tanzania. Tuanzie hapo.

Katiba mpya ipewe kipaumbele ili kutenganisha siasa na Udola, na kuweka taratibu zetu vizuri ili kuendana na mahitaji ya vyama vingi, uchumi wetu, maadili na haki.


Kwenye hili la chuki na kupotea umoja wa kitaifa awamu ya tano haiwezi kukwepa lawama na ndio ina wajibu wa kuurejesha.


Kwa hisani ya mtu wa Tanzania.

Kishada.
 
Huo ndio ukweli. Kuna watu wanazunguka sana kutafuta mchawi wa kinachoendelea hapa Tanzania.
Tanzania kwa sasa kuna chuki za kisiasa na uhasama uliopitiliza na kuhatarisha umoja wa Kitaifa.

Awamu ya Tano haiwezi kuepuka lawama hizo kwa hoja mbali mbali.
Tukumbuke tu kwamba kwa kiasi hiki cha miaka kama 25 baada ya kuja vyama vingi Tanzania, Utamaduni wetu uliathiriwa kwa kiasi fulani na ushabiki wa kivyama na kutengeneza ushindani wa sera na kufanya chaguzi kupata viongozi mbadala.

Siasa ni sehemu ya Utamaduni wa watanzania lakini ikliendeshwa kwa kufuatwa kanuni zake japo watawala walioipita nao walikuwa na madhaifu yao. Madhaifu hayo ilikuwa ni kama mchezo wa kisiasa na kamwe haikufika mahali kukajengeka chuki kiasi hiki.

Awamu ya tano imevunja utamaduni wa kisiasa uliojengwa wa kuvumiliana na kushindana kwa hoja leo tunaona siasa ya Dola dhidi ya vyama vya siasa.

Vyama vya siasa vimeporwa uhuru wa kufanya siasa za kishindani kwa kuzuiwa kufanya mikutano na maandamano.

Viongozi wa upinzani wananyanyasika kupata haki zao za kisiasa kutoka vyombo vya dola kama Polisi na kuingiliwa shughuli zao kinyume na taratibu na utamaduni wa kisiasa.

Chama tawala kinanufaika na Udola kwa viongozi wake kutumia mwavuli wa Kiserikali kujiimarisha huku wakiacha dhambi hiyo ikiitafuna Taifa.
Huwezi kuamini kwamba Rais na Mwenyekiti wa CCM anafanya kampeni kweupe kabla ya muda kufika kwenye mikutano yake tena na kupigiwa kampeni na ajkina HARMONIZE si msajili wa vyama vya siasa wala Mutungi anayejali. Katika hali hiyo lazima chuki ijengeke.


ATHARI
Wanasiasa wa upinzani, wanahabari, wanaharakati na taasisi za kiraia wote ni wanajamii na wana wafuasi wao, kinachowapata makundi hayo kinaipata jamii vile vile.

Huu mgawanyiko uliopo na kuombeana mabaya NI ZAO LA CHUKI HIYO. Na awamu hii ya tano inahusika.

Makundi mbali mbali yameshaeleza hatari iliyopo na kubezwa na hakuna hatua zinazochukuliwa hadi sasa si viongozi wa serikali si msajili wala viongozi wa dini.

Jamii inazidi kugawanyika, kuombeana mabaya na kuongezeka visasi baina ya watanzania.

NINI KIFANYIKE?

Tunarudia tena kufanywe mjadala wa Kitaifa na kuwakutanisha wanasiasa wote kwa Maslahi ya Tanzania. Tuanzie hapo.

Katiba mpya ipewe kipaumbele ili kutenganisha siasa na Udola, na kuweka taratibu zetu vizuri ili kuendana na mahitaji ya vyama vingi, uchumi wetu, maadili na haki.


Kwenye hili la chuki na kupotea umoja wa kitaifa awamu ya tano haiwezi kukwepa lawama na ndio ina wajibu wa kuurejesha.


Kwa hisani ya mtu wa Tanzania.

Kishada.
Uko sahihi kwa asimia zote. Tujisahihishe.
 
Well said Kishada ila sikubaliani na hiyo sehemu ya mwisho, 'nini kifanyike'. Mimi nashauri wananchi waendelee kudunduliza hela, zikipatikana za kutosha wanunue high powered rifles, halafu wanione niwashauri.
 
Kwahiyo viongozi wa CHADEMA walituzuia kuto kumuombea dua Lissu ili nafsi zao ziridhike?
Dua mnaweza fanya hata chumbani mwenu au hata hapo ulipo unaweza mfanyia dua yeyote yule

kama ni nyumba ya ibada hamna aliewanyima wala hatatokea mtu awanyime kwenda mkajumuike kufanya dua

Lissu ndio pekee wakuleta mshikamano na umoja hii nchi kumbe? sikua najua
 
Umeandika, ''Tanzania kwa sasa kuna chuki za kisiasa na uhasama uliopitiliza na kuhatarisha umoja wa Kitaifa''.

Hizo chuki unazodai ziko wapi wakati kila siku tunasikia wanachama wa chama tawala (CCM) wanahamia kwenye vyama vya upinzani au wanachama wa vyama vya upinzani wanahamia chama tawala.

Kama kuna chuki huwezi hata kusikia hawa wanachama wakiongea na kukubaliana kuhamia vyama vingine!

Mfano, kama una chuki na mtu fulani, utaweza vipi hata kuanza kutongozana na kukubaliana kuishi pamoja?

Tuache kupiga kelele kwa suala ambao halipo bali maneno matupu ya wanasiasa.
 
Well said Kishada ila sikubaliani na hiyo sehemu mwisho, 'nini kifanyike'. Mimi nashauri wananchi waendelee kudunduliza hela, zikipatikana za kutosha wanunue high powered rifles, halafu wanione niwashauri.
Hatari Mkuu. Hatujafika huko.
 
Kila zama na kitabu chake. Neno mjadala wa kitaifa unalitumia vibaya.
Kipindi cha mijadala kiliisha awamu ya nne,sasa nk kazikazi.


#PUMBAVU,LOFA.
 
Umeandika, ''Tanzania kwa sasa kuna chuki za kisiasa na uhasama uliopitiliza na kuhatarisha umoja wa Kitaifa''.

Hizo chuki unazodai ziko wapi wakati kila siku tunasikia wanachama wa chama tawala (CCM) wanahamia kwenye vyama vya upinzani au wanachama wa vyama vya upinzani wanahamia chama tawala.

Kama kuna chuki huwezi hata kusikia hawa wananchama wakiongea na kukubaliana kuhamia vyama vingine!

Tuache kupiga kelele kwa suala ambao halipo bali maneno matupu ya wanasiasa.
Unataka dalili gani ndio uamini ? Unasubiri ifike siku watu wasusiane kama kule Zanzibar ndio uamini kama kuna chuki?

Washauri watu wetu wa usalama waangalie ango zote kama tuko sawa. Jamii imetetereka.
 
Unataka dalili gani ndio uamini ? Unasubiri ifike siku watu wasusiane kama kule Zanzibar ndio uamini kama kuna chuki?

Washauri watu wetu wa usalama waangalie ango zote kama tuko sawa. Jamii imetetereka.
Mkuu;
Wewe umeona dalili gani ambayo ni mpya nchini?
 
Mkuu;
Wewe umeona dalili gani ambayo ni mpya nchini?
Dalili mpya? Huoni Ilivyokamatwa Bombadier na reaction ya upande wa Pili, Huoni Kilichompata Lissu na reaction ya Upande mwengine?

Huoni humo mitandandaoni chuki ilivyo?

Huoni mikesi ya wapinzani na wanavyosumbuka bila sababu hizo zote ni chuki au unatakla watu wakatane mapanga ndio uamini?
 
Dua mnaweza fanya hata chumbani mwenu au hata hapo ulipo unaweza mfanyia dua yeyote yule

kama ni nyumba ya ibada hamna aliewanyima wala hatatokea mtu awanyime kwenda mkajumuike kufanya dua

Lissu ndio pekee wakuleta mshikamano na umoja hii nchi kumbe? sikua najua
 
Back
Top Bottom