AU's dilemna and the Libyan crisis

Anyaway hata mimi siafiki nguvu za kijeshi kutumika kwa sababu
1. Maisha na mali vinateketea na mbaya zaidi...
2. Wanaowekwa baada ya hao madiktekta kutolewa hawana tofauti na madikteta walioondolewa, na hivyo...
3. Nchi inarudi back to square one....
Sasa kama wale wapya hawataki kubadilika.... kila mara tutumie nguvu za kijeshi kuwaondoa? Na na
 
AU haina maana yoyote, nini wameweza kufanya, Madagascar kimya, Ivory coast wanasuasua tu, Congo wanawake wanabakwa kila kukicha kimya, Kenya mpaka ICC wameitwa wao kimya, kwa Mugabe hamna kitu sasa hii AU kazi yake ni kula tu sioni kingine.
 
Ghadafi kaita raia wake mwenyewe mende na lazima waangamizwe sasa mnamteteaje huyu? Lazima watu watakufa tu kwa njia yoyote ila bora iwe ni katika kuwatetea wapate haki. Rwanda iliachwa wakachinjana leo wanalaumiwa UN hawakuchukua hatua.
 

Mkuu, kwa hali ya kawaida huwezi kufurahia wala kushabikia kinachofanywa na 'big fish', lkn mi natamani waipige libya zaidi ya iraq-kwani huo ndo ukombozi waliokuwa wanautaka walibya,walipewa vya bure wakala wakavimbiwa wakajifanya wanataka ukombozi! Sh...zi wakubwa!
 
Mkuu kwani unafikiria hata hao waliojipa 'uongozi wa kamati ya kuikomboa Libya ' wana tofauti na huyo Ghadafi? Tena wanaweza kuwa wabaya zaidi....
 
Pinga mwenyewe. Waafrika waliokuwa kwenye baraza la umoja wa mataifa walilidhia. Baki peke yako ukipinga kama ghadafi mwenywe.
Mbona ulishindwa kupinga kitendo cha kuwapiga raia wake kwa ndege za kijeshi?
 
Wamefurukuta asubuhi, ikabainika kuwa kumbe wanakula pesa ndefu kweli toka kwa Gaddafi!!!! wote kimya!!! wameaibika!!! wamemshindwa GABGO ndio watawaweza
 

Hivi issue ni miaka mingapi au deliverable? Kama Gaddafi amechokwa kwa miaka 42 ya usimamiaji mzuri wa resource za walibya, nna wac iko siku watu mfano wako wewe mtaandamana kudai M/Mungu asiwepo kwa kuwa yu-alwayz with forever! Teh teh!
 

Kama unakubaliana na Gaddafi kuua raia sasa unataka itumike njia gani ili akomeshe vitendo hivyo? au sisi waafrika tumelogwa? wakati Gaddafi anashambulia na kuua raia AU ilikuwa kimya, wakati UN inapitisha azimio la kulinda raia wa Libya, AU kimya, Wakati Gaddafi anashambulia mji wa Benghazi hapo jana bado ilikuwa kimya.

Lakini baada ya mashambulizi dhidi ya majeshi ya Gaddafi, ndani ya masaa 6 tu AU inasema mashambulizi yasitishwe! Shame on you AU.....!

Hakuna anayependa kuona maisha ya raia yanapotea, lakini tutakuwa wanafiki kama tutaruhusu viongozi wetu kuua raia na tukasema wakiamrishwa kukomesha vitendo vya mauaji ya raia huo ni ukoloni!




 
Mkuu kwani unafikiria hata hao waliojipa 'uongozi wa kamati ya kuikomboa Libya ' wana tofauti na huyo Ghadafi? Tena wanaweza kuwa wabaya zaidi....

Sio wanaweza kuwa wabaya, ni wabaya bcz Libya haikuhitaji upuuzi ule uliofanywa na wanaojiita 'wakombozi' so wacha waadhibiwe kwa usanii wao, si kwamba naunga mkono waasi au wavamizi.
 
Hao rais ambao unaosema wewe sio waasi, walipata wapi silaha?

Kumbuka unaowaita waasi walikuwa wanajeshi wa Gaddafi ambao waligoma kutii amri ya kuua raia na kuamua kujiunga na waandamanaji hivyo vikosi vyote vilivyojiunga na waasi vilienda na silaha zake!

Hizo ndizo silaha walizonazo.



 
Africa Union... hivi mpaka leo imefanya nini cha maana?
 
Kumbuka unaowaita waasi walikuwa wanajeshi wa Gaddafi ambao waligoma kutii amri ya kuua raia na kuamua kujiunga na waandamanaji hivyo vikosi vyote vilivyojiunga na waasi vilienda na silaha zake!

Hizo ndizo silaha walizonazo.




Na zile "special force" alizotangaza muwakilishi wa Urusi NATO zilizoingia Libya kabla ya maandamano zilikuwa za nani na kwanini ziliingia Libya?
 
..dhambi ya kuwafadhili waasi wa Liberia na Sierra Leone inamuandama Gadhafi.
 


Mimi nilishafika Libya kwa week moja; ila ndugu ukisema maisha ni zaidi ya wana Ulaya-ni uongo wa kupindukia. Libya bado ni maskini saaaaaaana kwa vile uchumi wao wa mafuta unamilikia na Ghadafi's family na marafiki zake tu. Bali idadi ya watu ni ndogo sana, na kwamba kama uchumi ungekuwa unamilikiwa na umma, nakubali hali ya maisha ya wenzetu ingebadilika-lakini sivyo!!
 
Hata nikisema maneno hayatasaidi i have always love the americans and the british but on this they made me mad and crazy if i have power i would erase them in this planet.....honesty lets kill all the americans and british.....french are just arrogant.
 
AU mlikuwa wapi siku zote hizi leo ndio mnakuja na utumbo wenu. Gaddaffi deserve this.Yeye anauwa watu wake anategemea nini? wacha wampige tu kichaa huyu.

Kwenye vita ya ukombozi wanaoathirika ni wengi. Wanachokifanya western countries sawa sawa kabisa viongozi wa Afrika ndicho wanachotaka kuachia madaraka kwa aibu. Wacha wapige tu mwendawazimu mkubwa huyu. Alikuwa anataka Afrika yote iwe chini yake ndoto zake za mchana. Amewanunua viongozi wengi wa Afrika.

Piga mpaka aachie ngazi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…