Atheism: Imani nusu na robo

Atheism: Imani nusu na robo

Mimi ni mmojawapo wa wale tusioamini uwepo wa Mungu' ila nilikulia kwenye imani ya kikristo tena wale walokole wa kunena kwa lugha... baada ya kufika umri wa kujitambua,nikajikuta napenda tuu kuchunguza kila kitu kinachohusu dini... hiyo ikanifanya niufuatilie kwa karibu sana uislamu. Kiukweli kabisa ukisoma kwa umakini biblia na quran utagundua kwamba hakunaga MUNGU kabisa yaniii... Na hivi karibuni nikaifuatilia imani ya BUDDHA na hapo ndo nikagundua kwamba mabuddha ni watu wanaojitambua hapa duniani.
Siwezi kuthibitisha ila inaonekana atheists wengi ni kama wametokea kwenye imani ya kikristo sijajua ni kwanini.

Mkuu ni kipi hasa kilichokufanya hadi ukaanza kupenda kuchunguza,na ni kipi hasa ambacho ulikuwa ukikichunguza?
 
Siwezi kuthibitisha ila inaonekana atheists wengi ni kama wametokea kwenye imani ya kikristo sijajua ni kwanini.

Mkuu ni kipi hasa kilichokufanya hadi ukaanza kupenda kuchunguza,na ni kipi hasa ambacho ulikuwa ukikichunguza?
Iko hivyo na ndio maana reference yao kubwa ni Mungu na Biblia, hata mjadala huu umejikita hapo..ni vigumu sana kukuta atheist anaponda satanism budhism kshna Hindu Taoism nk
 
Mkuu dini inafunga akili za watu na kuwatisha ili wasiwe wadadisi...hivyo kuwa chini ya kitu kisichokuwepo na kuwa watumwa kabisa....Ni vigumu sana kwa mtu mwenye uelewa mzuri na mdadisi akaendelea kuamini dini...Huyo Mungu ni wa namna gani mbona hajidhihirishi kwa watu wake na kumaliza malumbano?
Hilo ndiyo tatizo lenu la kupinga mungu kwa kumueleza mtakavyo nyie,sasa kusema mungu ajidhihirishe kwa watu wake ndiyo kunaleta maana gani? ni sawa na mtu ukuulize kuwa umemtafuta mungu sehemu zote na kumkosa hadi useme hayupo?
 
Iko hivyo na ndio maana reference yao kubwa ni Mungu na Biblia, hata mjadala huu umejikita hapo..ni vigumu sana kukuta atheist anaponda satanism budhism kshna Hindu Taoism nk
Mkuu mie nimefuatilia sana unachokisema ni kweli,sijajua ni kwanini ipo hivi?
 
Hilo ndiyo tatizo lenu la kupinga mungu kwa kumueleza mtakavyo nyie,sasa kusema mungu ajidhihirishe kwa watu wake ndiyo kunaleta maana gani? ni sawa na mtu ukuulize kuwa umemtafuta mungu sehemu zote na kumkosa hadi useme hayupo?
Wewe umewahi kumwona huyo Mungu?
 
Hilo pia tatizo lenu lengine,kuniuliza kama nimewahi kumuona mungu inakuwa kama hujui sifa za hicho unachosema hakipo.
Narudia tena, je umewahi kumwona Mungu? jibu NDIYO au HAPANA!
 
Kila kitu ni Imani so hiyo ni atheism nayo ni imani. Imani yao ni kuwa hawaamini eitha juu ya Mungu au shetani.
 
Wewe umewahi kumwona huyo Mungu?

Narudia tena, je umewahi kumwona Mungu? jibu NDIYO au HAPANA!

Sasa kama hujawahi kumwona Mungu wala kumsikia akiongea, ulizijuwaje sifa zake?
CHARMILTON hapa ndio penye kiini cha tatizo kudhani kwamba Mungu ni solid object amekaa mahali fulani na kufanya chochote kinachosemwa kuhusu yeye...! Lakini iko hivi kwenye Biblia kitabu cha mwanzo kinaanza kwa kusema
.....hapo mwanzo alikuwepo neno(conscious energy), naye neno alikuwepo kwa Mungu (conscious mind),naye neno alikuwa Mungu conscious energy + conscious mind= conscious soul)
Kwahiyo chochote kinachotokea duniani kiko wenye muktadha huo na Mungu sio kama yake masanamu ya wahindi au mabudha
 
Siwezi kuthibitisha ila inaonekana atheists wengi ni kama wametokea kwenye imani ya kikristo sijajua ni kwanini.

Mkuu ni kipi hasa kilichokufanya hadi ukaanza kupenda kuchunguza,na ni kipi hasa ambacho ulikuwa ukikichunguza?
ALBADIR ndiyo ilinifanya nianze kuchunguza mambo ya dini, maana ilikua inanipa ukakasi kidogo... iweje MUNGU huyu huyu mwenye upendo kwa watu wake,aweze kuwadhuru vibaya waliokuwemo na mpaka wasiokuwepo kwasababu tuu kuna mtu aliibiwa mbuzi zake huku wengine walikula nyama yake kwenye sherehe bila kutambua?

Basi nilifuatilia mpaka mwisho wake na kupata jibu lililonyooka!
 
CHARMILTON hapa ndio penye kiini cha tatizo kudhani kwamba Mungu ni solid object amekaa mahali fulani na kufanya chochote kinachosemwa kuhusu yeye...! Lakini iko hivi kwenye Biblia kitabu cha mwanzo kinaanza kwa kusema
.....hapo mwanzo alikuwepo neno(conscious energy), naye neno alikuwepo kwa Mungu (conscious mind),naye neno alikuwa Mungu conscious energy + conscious mind= conscious soul)
Kwahiyo chochote kinachotokea duniani kiko wenye muktadha huo na Mungu sio kama yake masanamu ya wahindi au mabudha
Kama Mungu siyo solid object, ilikuwaje akamtokea Musa katika umbo la moto? Je moto siyo solid object inayoonekana na kuhisika?
 
Kama Mungu siyo solid object, ilikuwaje akamtokea Musa katika umbo la moto? Je moto siyo solid object inayoonekana na kuhisika?
Kitu kinapokuwa kwenye form ya kiroho huweza kuvaa umbo lolote
 
Kama Mungu ni roho isiyoweza kuvaa umbo lolote, je Musa alidanganya aliposema Mungu alimtokea katika umbo la moto?
Sijasema hivyo tafadhali hebu rudia kusoma nilichoandika
 
View attachment 395344

kwenye ulimwengu wa vipimo kuna ujazo mbalimbali kama robo nusu na kitu kamili nk.. nusu mbili hutengeneza kitu kamili robo mbili hutengeneza nusu.

Kuna kamchezo ukimtuma mtu asiye mwaminifu akuletee kitu kinachohusika na vipimo kupiga bao! Ukimtuma kilo moja yeye ataleta nusu na robo.

Duniani tuna imani mbalimbali kuanzia zinazoabudu Mungu mmoja,miungu vitu vinavyoonekana hata masanamu kwenye hizi imani kuna mitifuano na mikanganyiko mingi tuu..lakini kiboko ya imani zote ni hii isiyomwamini Mungu mmoja

Jaribu kumuuliza atheist yeyote kwanini huamini katika Mungu atakwambia kwakuwa hajawahi kumuona! Ila muulize kama alishawahi kuiona akili yake au roho yake...hatakupa jibu moja na la moja kwa moja

Hii ni imani isiyotimia isiyojua dhima yake mwanzo wake wala muktadha wa nini inasimamia

Ni imani chongo yenye kengeza barobaro...ikiamini isichokiamini..ikifuata isichokijua

Je atheism ni;
Kuabudu miungu?
Kuabudu shetani?
Kuabudu masanamu?
Kuabudu vitu ?
Ama kutoabudu chochote?

Kila imani ina maelezo fulani kwenye chochote na kila swali lina jibu lake tusiiweke sayansi kwenye kundi la imani..hili ni Somo kama masomo mengine

Kutoamini chochote ni mkanganyiko tu wa akili kwakuwa mwisho wa siku utajikuta unaangukia kwenye imani yoyote japo kwa kificho na imani ya kutoamini chochote ni imani isiyotimia
Una hakika atheists wote hawaamini Mungu kwa sababu hawajamuona?

Au kufikiri hivyo ni matokeo ya kukosa elimu kwako tu?
 
Sijasema hivyo tafadhali hebu rudia kusoma nilichoandika
Je Mungu ni roho ama siyo Roho?

Roho inaweza kuvaa umbo la kitu chochote?

Je Mungu amewahi kumtokea Musa akiwa katika umbo la moto?

Mshana tafadhali jibu hayo maswali matatu precisely!
 
Una hakika atheists wote hawaamini Mungu kwa sababu hawajamuona?

Au kufikiri hivyo ni matokeo ya kukosa elimu kwako tu?
Twende kwa mjadala tuache ubabe wa kukosoa as if unanifahamu....
 
Back
Top Bottom