At your own risk

At your own risk

Wengine ni baba tu mwanzo mwisho.

Sijawahi kuona mtu kama baba yangu. Najaribu kuvaa viatu vyake kwa mabinti zangu lakini naona havinienei.

Kila mtu anasema hakuna kama mama lakini hakika ni kweli kabisa kwangu kuwa hapajapata tokea mtu kama baba.
 
Mkuu nimeguswa haswa na uzi wako, mama yangu alifariki nikiwa shule ya msingi miaka 17 iliyopita. Haijawahi kupita siku sijammis. Graduations, harusi, kupata watoto, nikiwa kwenye misukosuko, neema,vipindi vyote hivyo nilitamani awepo tufurahi wote, anifariji, aone wajukuu. Nimeishi zaidi ya nusu ya umri wangu wa sasa bila yeye, upendo wangu kwake haujawahi kupungua na nahisi kumhitaji kila siku ila ndio hivyo alipangalo mola. Pumzika kwa amani mama,Amein!
 
I love my dad! The best dad ever (until you ask my daughter then she'll tell you that I'm the best dad in the whole wide world)

Nami pia nampenda sana baba, he has always been there to support me. Ila pengo la mzazi yeyote kwangu halizibiki.
 
sipati connection ya ulichoandika na title..

Maana yake ni kuwa baada ya kusoma unaweza kumbuka na ukahuzunika au kukusababushia maumivu fulani. So soma hii post at ur own risk, umeelewa sasa?
 
Si kweli! Kumkumbuka mtu aliyekutoka kwa uchungu inategemea na jinsi alivyokuwa anakujali.
 
Hapa duniani hakuna mtu anayeishi maisha magumu kama yule aliyefiwa na mama yake mzazi.

Ni bora ya mtu asiye na pesa, atahangaika atatafuta na ipo siku atazipata hata kama ni uzeeni atapata tu lakini ukimpoteza mama ndio imetoka hiyo. Mama hautaweza kumtafuta, mama hana mbadala, mama ni mmoja tu, ukimkosa huyo uliyenae hujikumpata mama mwingine.

Mtu asiye na mama anakuwa kwenye wakati mgumu sana hasa nyakati za:
1. GRADUATION 2. HARUSI 3. ANAPOPATA MAFANIKIO

Katika hayo matukio ndio ambapo kila mtu anakumbuka sana mama yake, utakapokuwa kwenye harusi unawish mama yako angekuwepo, utakapokuwa kwenye graduation unawish mama yako angekuona unapomaliza chuo.

Mtu anapomzungumzia mama yake basi nawewe unawish mama yako angekuwepo, mtu akipigiwa simu na mama yake unatamani mama yako angekuwepo labda angekupigia simu.

Mtu asiye na mama kila akikumbuka mama yake alipokuwa akimuita, akimfulia nguo, akimnyoshea nguo, akimuwekea chakula na kumfundisha mambo mengi ya kimaisha ataishia kulia tu.

Uchungu wa kumkosa mama hauna kifani wanajamiiforums, ukimkosa mama unaweza ukajiuliza unaishi ili iweje sasa?

POLENI WOTE MLIOFIWA NA MAMA ZENU PIA NISAMEHENI KWA KUWAKUMBUSHA MACHUNGU NA KUWATOA MACHOZI.

Dr. MCHUNGUZI HURU (PhD)

At least leo uchunguzi wako uko sahihi
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli kabisa,ni uchungu usio na kifani. Mama yangu ni mwaka mmoja na miezi kadhaa ulipotuacha kwa ghafla uchungu ninaousikia hauna maelezo yoyote! Mpaka leo kuna vitu huwa nawaza nitamwambia mama yangu ndio atakaenielewa , baadae nakumbuka kuwa hatunae tena,ila kwa uhakika kiroho bado niko nae!

pole kwa hilo ndg yangu kumbuka karudi kwenye makao ya milele kwa mapenzi ya mungu alitupa kwa muda ili tumtumie sasa kamrudisha kwake
 
Poleni sana nyote mliondokewa na wazazi wenu hususan mama.... Kazi ya Mola haina makosa.
 
aiseeeee kwa hili nasoma michango ya watu tu
 
Ni kweli kabisa,ni uchungu usio na kifani. Mama yangu ni mwaka mmoja na miezi kadhaa ulipotuacha kwa ghafla uchungu ninaousikia hauna maelezo yoyote! Mpaka leo kuna vitu huwa nawaza nitamwambia mama yangu ndio atakaenielewa , baadae nakumbuka kuwa hatunae tena,ila kwa uhakika kiroho bado niko nae!
Pole sana
 
Mie mama yangu ana miaka karibu 17 tangu afariki na baba amefikisha 18 pia. Kusema kweli sikuwa rafiki sana na baba. Na bahati nzuri nina watoto lakini baba yao ana tabia kama za babangu hivyo siwezi hisi upendo wake. RIP my Dad & Mom.
 
Nilimshuhudia bibi harus mmoja wakat wa zawad kwa wazazi wake alienda baba ake tu. Mama ake alifark na hvyo akamchukua mama wa mume wake akamtunza zawad nyng sana lakini alilia sanaaa
 
Ukweli usiopingika 100% true love you my mum nakuombea maisha marefu nakupenda mamaangu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom