Gurudumu
JF-Expert Member
- Feb 5, 2008
- 2,349
- 261
Nina miaka mingi tangu nilipokwenda kanisani kusali tofauti na kusindikiza maharusi. Mimi hupinga ulokole kwa sababu ni brainwashing na haina tofauti na uganga wa kienyeji.
Lakini kuna wakati nasikiliza mahubiri ya walokole kwenye tv. Baada ya muda sasa nimegundua yafuatayo;
1. Kuna wahubiri ambao wanaigiza, wanapiga kelele hovyo hovyo
2. Kuna wahubiri wanahubiri chuki dhidi ya wenzao na hawa hawana mantiki
3.kuna wahubiri wanaosoma biblia peke yake, inawezekana hata magazeti hawasomi hivyo wana uchambuzi mwembamba sana kuhusu maisha na utawala wa nchi
4. Kuna kakobe peke yake, anasoma tafiti na nadharia nyingi na anachambua mambo kwa upana sana. Anajua sana kupangilia hoja kimamtiki. Lakini mwisho humalizia na vile vitendo vya uganga wa kienyeji - majini, maradhi, ajira, kutozaa, n.k
tangu wiki mbili zilizopita kakobe amekuwa akitoa elimu pana sana ya uraia kusaidia upigaji kura kwa kuchambua hoja badala ya kushabikia.
Ndiyo maana nasema askofu kakobe Jana Leo na kesho. Naomba aendelee hadi siku ya tarehe 30 October. Anatoa elimu pana yenye mantiki zisizo na ukakasi. Anafanya kazi waliyoshindwa NEC na TAKUKURU. Jana na leo kapiga shule ya rushwa elimu ambayo inatoboa mfupa. Anatumia tv ya channel ten
Asante askofu kakobe, anatoa mchango mkubwa sana kwa gharama kidogo wakati serikali inatumia mabilioni kwa taasisi ya rushwa ili isimamie na kuwalinda wala rushwa.
Siyo kila kifanywacho na viongozi wa dini ni udini
Lakini kuna wakati nasikiliza mahubiri ya walokole kwenye tv. Baada ya muda sasa nimegundua yafuatayo;
1. Kuna wahubiri ambao wanaigiza, wanapiga kelele hovyo hovyo
2. Kuna wahubiri wanahubiri chuki dhidi ya wenzao na hawa hawana mantiki
3.kuna wahubiri wanaosoma biblia peke yake, inawezekana hata magazeti hawasomi hivyo wana uchambuzi mwembamba sana kuhusu maisha na utawala wa nchi
4. Kuna kakobe peke yake, anasoma tafiti na nadharia nyingi na anachambua mambo kwa upana sana. Anajua sana kupangilia hoja kimamtiki. Lakini mwisho humalizia na vile vitendo vya uganga wa kienyeji - majini, maradhi, ajira, kutozaa, n.k
tangu wiki mbili zilizopita kakobe amekuwa akitoa elimu pana sana ya uraia kusaidia upigaji kura kwa kuchambua hoja badala ya kushabikia.
Ndiyo maana nasema askofu kakobe Jana Leo na kesho. Naomba aendelee hadi siku ya tarehe 30 October. Anatoa elimu pana yenye mantiki zisizo na ukakasi. Anafanya kazi waliyoshindwa NEC na TAKUKURU. Jana na leo kapiga shule ya rushwa elimu ambayo inatoboa mfupa. Anatumia tv ya channel ten
Asante askofu kakobe, anatoa mchango mkubwa sana kwa gharama kidogo wakati serikali inatumia mabilioni kwa taasisi ya rushwa ili isimamie na kuwalinda wala rushwa.
Siyo kila kifanywacho na viongozi wa dini ni udini