Hili laweza kuwa somo zuri na fundisho tosha kwa wale wanaopenda mno kuongea na kufunguka kuhusu mambo yao binafdi
Mazungumzo yote aliyorekodi Gwajima ya mchumba wa Dr Slaa na wengine pia yametufundisha mengi
1: kwamba Dr Slaa pamoja na uwezo wake wote wa kujieleza na kusimamia mambo kwa ufanisi, elimu yake ya theologia na daraja lake LA upadri hakuwa anajiamini na alikuwa dhaifu mno kwenye mahusiano mpaka kutafuta msaada wa Gwajima
2:Zile enzi za usipige picha hapa zimepitwa na wakati kutokana na technolojia kukua
3:gwajima ni mjanja mtoto wa mjini mhuni anayejiamini asiyeogopa chochote aliyeaminika mno na wale waliomwamini na hivyo kumpa nafasi kubwa ya kumwamini na kumwambia yao ya ndani bila kujua kuwa jamaa alikuwa anaweka kumbukumbu kwa matumizi ya baadae, wengi sasa matumbo joto Wakiwa hawana uhakika kama nao walirekodiwa au la
4: Serikali imeshikwa pabaya na kupitia Gwajima mambo mengi yaliyo nyuma ya pazia bila kujifahamu wamempa loophole kubwa sana ya kuyafahamu kwahiyo kuanzia sasa inabidi waende naye kwa tahadhari kubwa la sivyo atazidi kuharibu