Askofu Bagonza: Kuna kitu hakiko sawa

Askofu Bagonza: Kuna kitu hakiko sawa

Askofu Amani awataka mapadri, watawa kuchukua tahadhari ya corona​

THURSDAY JANUARY 21 2021​


Summary

  • Askofu wa Jimbo Kuu Katoliki la Arusha, Isaac Amani ametoa waraka akiwataka waumini kuendelea kuchukua tahadhari ya ugonjwa wa Covid-19 ikiwa ni pamoja na kunawa mikono kwa maelezo kuwa ugonjwa huo bado upo na unayasumbua mataifa mbalimbali duniani.
By Mwandishi Wetu
More by this Author

Arusha. Askofu wa Jimbo Kuu Katoliki la Arusha, Isaac Amani ametoa waraka akiwataka waumini kuendelea kuchukua tahadhari ya ugonjwa wa Covid-19 ikiwa ni pamoja na kunawa mikono kwa maelezo kuwa ugonjwa huo bado upo na unayasumbua mataifa mbalimbali duniani.

Katika waraka huo kwenda kwa mapadri, watawa na walei wa jimbo hilo aliouita ‘kutembea pekupeku juu ya mbigili’, amesema baada ya kutangazwa kuwa ugonjwa huo haupo nchini, watu wameacha kuchukua tahadhari.

"Maji ya kunawa mikono yameondolewa kanisani na mahala pengine yapo, lakini watu hawanawi tena kwa imani kwamba hakuna corona, ile tahadhali ya kujikinga wameiacha na bado wanashikana mikono,” amesema huku akigusia utaratibu wa utoaji sadaka na kukomunika.

Amesema mapadri na watawa walihimizwa kuwa waangalifu zaidi ili wasisababishe maambukizi miongoni mwao na wanaowahudumia, “ilihimizwa pia kuvaa barakoa kwenye vyombo vya usafiri wa watu wengi, sokoni, kwenye ibada na hospitali.”

"Kutokana na hali halisi inapaswa kujenga utamaduni na tabia mpya za kujinusuru kwa vingine kwa hakika tunatembea sasa pekupeku juu ya mbigiri, tutafakari hali halisi kwani mwenye macho haambiwi tazama,” amesisitiza.

Amebainisha kuwa lengo la waraka wake ni kumwalika kila mtu ajisimamie kwa usalama wake binafsi na kujali usalama wa wengine kwani Corona inatikisa ulimwengu, “na sisi tusijidanganye kiasi cha kutochukua tahadhari.”

"Tusimjaribu Mungu kwakufanya uzembe na afya zetu, Turejee tahadhari za kuzuia maambukizi bila kuwa na hofu, hakuna haja ya kufungiwa, tuendelee kusali na kuchukua tahadhali. Ukiona unawashwa kwenye koo, kukauka koo kikohozi kikavu, joto kubwa na kupumua kwa taabu haraka mwone daktari ili usaidiwe." alisema
 
Usikute kayaongea haya kwenye ibada ya watu zaidi ya 200 na wote hawajavaa mask na bado wamesongamana kwenye kutoa sadaka alaf bado anashindwa kumtukuza Munga kwa hilo yeye analeta janja janja za siasa.
Umetumia akili au matope kuandika maneno haya?
 

UK bans flights from Tanzania and the Democratic Republic of Congo in latest bid to stop South African 'more vaccine resistant' Covid strain spreading here​

By James Robinson for MailOnline22:33 21 Jan 2021, updated 23:15 21 Jan 2021

wire-38329146-1611268440-18_1908x1146.jpg

  • The UK will introduce a ban on arrivals from the two African nations from Friday
  • The rule will not apply to returning UK nationals, and those with residency rights
  • It comes amid growing concern over the South African mutant Covid variant
  • Scientists are concerned the new strain may make current jabs less effective
The UK has banned arrivals from Tanzania and the Democratic Republic of Congo in the latest bid to stop the 'more vaccine resistant' South African Covid strain taking hold in Britain.
Transport Secretary Grant Shapps tonight announced the ban on arrivals entering the country from the two African nations.

wire-38329148-1611268444-392_634x421.jpg
More countries have been added to the arrival ban list in a bid to prevent the South African Covid-19 variant from taking hold in the UK. Pictured: The arrivals area of Heathrow Airport
The decision comes after UK's chief scientific adviser Sir Patrick Vallance warned this week that coronavirus variants were a 'real issue of concern'.
Scientists believe the vaccines currently being rolled out may be less effective against the South African variant, known as 501Y.V2.
Mr Shapps tweeted: 'To help to stop the spread of the Covid-19 variant identified in South Africa, we are banning all arrivals from Tanzania and Democratic Republic of Congo from 4am tomorrow.
 
Corona ipo ila tumshukuru Mungu wengi tumeweza kuishi nayo kwa miili kujenga kinga. Baadhi wanasayansi wanapendekeza kutovaa musk ili kubadilishana virus na bacteria kujenga kinga imara zaidi.
Mhuuu hil
Tatizo anaongeaga sana..ilikua ni sentensi mbili tu..corona ipoa tanzania,tuchukue tahadhari...basi...kanajifanya kana hekima kumbe kawaida tu.....et Mungu anaweza kuwepo kwwnye corona...hiv anajua mungu ni nan.
Jadili hoja sio mashambulio
 
CORONA BADO IPO DUNIANI

Kufuatia taharuki inayotokana na vifo kadhaa mwishoni na mwanzoni mwa mwaka hapa Karagwe, watu wengi wamekuwa wanapiga simu kwangu na kwa uongozi wa hospitali teule ya Nyakahanga kuulizia kulikoni? Jibu hili litoshe kusaidia kujibu maswali hayo:

1. Corona BADO iko duniani. Tanzania ni sehemu ya dunia. Malizia sehemu inayobaki. Maswali yaliyobaki waulizeni wenye dhamana na masuala ya Afya ngazi ya Mkoa na Wilaya.

2. Tanzania si makao makuu ya Mungu. Yeye ni wa wakati wote na wa mahali pote. Mahali alipo, Corona yaweza kuwapo pia. Wenye dhambi na watakatifu wote wanaugua na kufa. Makutano yetu ni ufufuko.

3. Uhai tulio nao si mali ya serikali wala ya dini yoyote. Tuna wajibu wa kuulinda. Tuchukue tahadhari zote bila kusubiri maagizo ya serikali au ya dini. Nawa mikono, tumia barakoa, jiepushe na mikusanyiko, nyungu haizuiwi na tiba mbadala nyingine hazizuiwi. Ramli ni marufuku hospitalini.

4. Kama si lazima usiende hospitalini kutembea. Kama si lazima tibiwa nyumbani kwako. Kama si lazima usizushe kuwa una ugonjwa ambao haujathibitishwa kwa vipimo.

5. Tunapakana na nchi zilizojitangaza kuwa zina maambukizi makubwa ya Corona. Majirani wema huzaa watoto wanaofanana kwa sababu ya kuhusiana vizuri. Hii ni vita, ujirani uchukue viwango vipya.

6. Idadi ya wagonjwa wenye matatizo ya kupumua imeongezeka ndani ya muda mfupi. Yawezekana ni uchovu wa mwisho wa mwaka! Idadi ya mitungi ya Oksijeni tuliyo nayo ni ndogo. Wasamaria wema wanakaribishwa kusaidia mitungi zaidi. Siasa safi ni kujitolea mitungi zaidi ili wenye shida ya kupumua wasaidiwe. Karibuni.

Kwa nia njema na kwa mapenzi makubwa kwa watu nilioagizwa kuwachunga na kuwalisha.
Chato ni chaka la kuepuka maambukizi ... Kabisa ilikua hivyo hapo mwanzo inaonekana hivyo hata sasa ... na itakua hivyo hapo baadae

Amakweli watanzania wasasa sio wajinga tena ... kama na dhambi nizipate ila nafsi yangu inaomba waanze kupukutika huko juu ...

Watakapoanza kuputika wao ndio watachukua hatua zitakazo pelekea na sisi wachini tunusurike otherwise wataendelea kutuhadaa kwa faida zao za kisiasa haliyakua sisi wachini ndio tunaumia na familia zetu

Haya twendeni tuombe kwa pamoja ...

... Ewe Mungu Baba tunakuomba uanze kuwapukutisha mmoja baada ya mwingine kuanzia barazani chamwino mpaka pale sebuleni mjengoni ili hatua za makusudi zichukuliwe na sisi wachini tunusurike AMEN!!!
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Baba ktk ubora wake
CORONA BADO IPO DUNIANI

Kufuatia taharuki inayotokana na vifo kadhaa mwishoni na mwanzoni mwa mwaka hapa Karagwe, watu wengi wamekuwa wanapiga simu kwangu na kwa uongozi wa hospitali teule ya Nyakahanga kuulizia kulikoni? Jibu hili litoshe kusaidia kujibu maswali hayo:

1. Corona BADO iko duniani. Tanzania ni sehemu ya dunia. Malizia sehemu inayobaki. Maswali yaliyobaki waulizeni wenye dhamana na masuala ya Afya ngazi ya Mkoa na Wilaya.

2. Tanzania si makao makuu ya Mungu. Yeye ni wa wakati wote na wa mahali pote. Mahali alipo, Corona yaweza kuwapo pia. Wenye dhambi na watakatifu wote wanaugua na kufa. Makutano yetu ni ufufuko.

3. Uhai tulio nao si mali ya serikali wala ya dini yoyote. Tuna wajibu wa kuulinda. Tuchukue tahadhari zote bila kusubiri maagizo ya serikali au ya dini. Nawa mikono, tumia barakoa, jiepushe na mikusanyiko, nyungu haizuiwi na tiba mbadala nyingine hazizuiwi. Ramli ni marufuku hospitalini.

4. Kama si lazima usiende hospitalini kutembea. Kama si lazima tibiwa nyumbani kwako. Kama si lazima usizushe kuwa una ugonjwa ambao haujathibitishwa kwa vipimo.

5. Tunapakana na nchi zilizojitangaza kuwa zina maambukizi makubwa ya Corona. Majirani wema huzaa watoto wanaofanana kwa sababu ya kuhusiana vizuri. Hii ni vita, ujirani uchukue viwango vipya.

6. Idadi ya wagonjwa wenye matatizo ya kupumua imeongezeka ndani ya muda mfupi. Yawezekana ni uchovu wa mwisho wa mwaka! Idadi ya mitungi ya Oksijeni tuliyo nayo ni ndogo. Wasamaria wema wanakaribishwa kusaidia mitungi zaidi. Siasa safi ni kujitolea mitungi zaidi ili wenye shida ya kupumua wasaidiwe. Karibuni.

Kwa nia njema na kwa mapenzi makubwa kwa watu nilioagizwa kuwachunga na kuwalisha.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Kazi aliyofanya Mungu Tanzania kwenye issue ya Corona ni kubwa Mno na haitakiwi kkudhihakiwa atakiona cha mtena joho lake pete na kofia na fimbo yake ya kiaskofu ni takataka tu Mbele za Mungu aliyemdhihaki baada ya kufanya kazi kubwa ya kupigania Tanzania dhidi ya Corona
Acha ujinga wako! Ujinga siyo mali. Jifunze kila siku!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom