Asante Mungu leo nimewahama Rasmi NBC

Asante Mungu leo nimewahama Rasmi NBC

Mkuu we NBC isikie hivyo hivyo. Nina kademu kangu ni staff wa NBC hapa Moro kila siku anafanya application kwenye benki zingine. Anasema staff wamekuwa demoralized totaly. Makampuni makubwa wameanza kujiondoa NBC. Mimi ninafahamu mazungumzo ya vikao vya juu vya TTCL kutaka kufunga expenditure and collection account all together kwa sababu ya ujinga wao NBC

Sasa mnatutisha bana!

Manake nikifikiria hela niliyonayo huko nakosa raha kabisa.
 
Crdb walikuwa na hiyo deposit kwenye atm nadhani holland branch? Hebu waulizie

CRDB walikuwa nayo wakasitisha kwakuwa bandwith waliyokuwa nayo isingeweza ku accomodate wateja wengi na waliiacha pale Azikiwe kama Pilot badae wakasitisha.

Oooh...kumbe kitu kama hicho kimeshawahi kuwepo, ni vyema wakarudisha hii kitu aisee maana naona wameng'ang'ania sana kwenye e-banking wakishirikiana na makampuni ya simu (sijui kwa kuwa wanjaua huko kunalipa kiaina)...
 
Baba, na huu unyang'anyi wa siku hizi bora ukapange foleni. Hawakawii kudhani una vibunda vingi vya hela wakikuona hapo then waishie kufly na kibanda na kichwa chako.

Ni rahisi unatoa tu hela from mpesa unaingiza bank. Then unatoa bank na kurudisha kwa simu. You dont need to que
Oooh...kumbe kitu kama hicho kimeshawahi kuwepo, ni vyema wakarudisha hii kitu aisee maana naona wameng'ang'ania sana kwenye e-banking wakishirikiana na makampuni ya simu (sijui kwa kuwa wanjaua huko kunalipa kiaina)...
 
Now, two things. Either Paw ananichezea fraud (kwamba card yake haifanyi kazi nje ya nchi ) or it aint a visa card. But i thought nbc hawana visa wala master card kwenye atms zao? But then clicks in my mind, kuepuka long que ya atm ya crdb i mostly use ya nbc ama exim kutoa hela.

I am launching a serious investigation. Asante kwa clue.
Hapana, hapo umekosea kabisa. Na licha ya kwamba siipendi NBC lakini kwenye hilo nitawatetea.

Kadi za NBC hata nje ya nchi zinafanya kazi ili mradi ziwe tu na nembo za Visa/ MasterCard na kama unatoa hela kwenye ATM basi nayo iwe na nembo za hayo makampuni mawili na utaweza kutumia kadi yako bila adha yoyote ile.

Hata kwenye gas stations, kwenye gas pump zinafanya kazi kama kawaida.

Na hilo nalijua kwa uhakika kabisa kwa sababu mimi ni mteja wa NBC na mara kwa mara huwa naitumia kadi yao (well, kabla hawajaifungia akaunti yangu wakinidai niende kuhakiki taarifa zangu).

Najua wengi hatuipendi hiyo benki lakini si mbaya kiviiiiile kiasi hata cha kadi zao zisiweze kutumika nje ya nchi.

Watendee haki bana aaah!
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: Paw
niliachana nao mwaka 2000 wkt nasoma marekan wakanikata hela nilivunja kadi nikaweka mlangoni
 
Now, two things. Either Paw ananichezea fraud (kwamba card yake haifanyi kazi nje ya nchi ) or it aint a visa card. But i thought nbc hawana visa wala master card kwenye atms zao?

Sina hakika sana kuhusu Visa lakini MasterCard wanazo na ninayo yangu hapa naitazama sasa hivi. Na inafanya kazi ndani na nje ya nchi. Nishawahi kuitumia Doha, London, na kwingineko.
 
me nina miezi7 sasa toka nikimbie benki teller wote wazee shinyanga town
 
Wame zuia kadi yangu pamoja na huduma ya mobile money siku ya sita leo eti wana boresha taarifa zangu.Nili wapelekea form,picha,barua ya mtendaji toka lhamisi iliyopita lakini kimya mpaka leo.Nime kua loyal customer toka 2011 ila kwa hili jambo naona maji yame zidi unga.Naenda kuhamishia pesa zangu zote kwenye account ya crdb sitaki huu ushenzi kabisa na account naisusa.Haiwezekani wao wana behave kama ndo bank pekee Tanzania kwa kua na huduma mbovu kiasi hiki.Kwa heri nbc nilikupenda sana lakini ume nikwaza kupita kiasi.
 
Nilishawatupia kapuni miaka miwili iliyopita, Nilikaa nje muda zaidi ya miezi sita hivyo account yangu haikuwa active, nikaambiwa nianze process zote kuanza utambulisho wa makazi kwa mwenyekiti wa serikali ya kijiji, mahakama nk kana kwamba ndo nafungua upya account. Process zilinichukua zaidi ya siku nne bila kuona kinachoendelea, basi rafiki yangu pale kaniambia nenda CRDB uone mambo. Kwa vile nilikwa NBC pale tawi la Twiga makao makuu mkabala na bandari karibu na St Joseph Cathedral, nikachanganya miguu hadi jengo la William Mkapa mkabala na posta mpya, nikapokelewa kama mfalme na kukabidhiwa form ya kufungua account na kwamba taratibu za kufungua account ni kitambulisho tu kilicho halali kiserikali.

Nikageuza na kwenda NBC kuchukula pesa zangu zote bila kuacha salio na kwenda kuzitumbukiza zote CRDB. Hawa wako wazuri, na huduma zao kama bank za ughaibuni vile. Wanaoendelea NBC nawapa pole. CRDB statement naipata kwa email kila mwezi.
Mimi pia nipo mbioni kuondoka huko kwa sababu waliweka matangazo yao ya mobile banking, nikajaza From na wakaniambia kuwa baada ya siku tatu (3) nitapata sms ikinieleza jinsi ya ku-activate hiyo Mobile Banking. Baada ya wiki mbili sikupata sms yoyote ikabidi niende tena kwenye tawi nililojaza form. Baada ya kuangalia kwenye data zao wakadai kuwa hawazioni wakanishauri nijaze tena na nikafanya hivyo. Wakasema tena nisubiri siku 3 nitapata sms. Ikapita mwezi sikupata sms yoyote, nikaenda tena wakanipa form nyingine tena ambayo ilikuwa na tofauti kidogo na zile 2 za mwanzo wakaniambia nisubiri nitapata sms. Leo hii ninavyoandika hapa nadhani ni miezi 6 kama siyo 8 tangu nijaze form ya mwisho na sijapata sms wala simu wala ujumbe wowote!!!!Wakati CRDB nilijaza form siku 1 na baada ya saa 24 nilipata sms na hadi leo nina-enjoy huduma za Simbanking.
 
Baada ya kuwavumilia kwa takriban miaka minane na manyanyaso, Huduma mbovu ndani ya benk kadhalika na Atm machine zao, LEO nimeamua kuachana kabisa na benki hii kwa kufanya mambo yafuatayo
1; nimehamisha salio langu lote
2; nimevunja kadi zao zote kuanzia utambulisho mpaka atm kadi zao
3;nimehamisha mshahara kupitia kwao kudadadeki zao
4;nimezinguana na costomer service manager wao
wa tawi moja hapa town
5;nimekuja kuwapa taarifa humu wana jf wenzangu wanaofikiria kujiunga na benk hii wasithubutu itakula kwao.
Benk hawataki kubadirika, kazi kuajiri midioker tu na watu wasiojiweza, mtu dirishani kwa teller anatumia zaidi ya nusu saa bila sababu ya msingi, na siyo dar tu nimeenda matawi yao kibao kama Tabora, morogoro, dar ndo balaa, mtwARA ndo shida kabisa kudadadeki zao, nimejiendea CRDB yan burudani kumbe nilikuwa nachelewa tu siku zote hz, hongereni CRDB hasa holland branch kwa kazi nzuri.
Mkuu juzi nilienda ya pale Chuo Mlimani walai kwa saa moja walihudumia watu 3....hiyo bank haifai kabisa
 
Sina hakika sana kuhusu Visa lakini MasterCard wanazo na ninayo yangu hapa naitazama sasa hivi. Na inafanya kazi ndani na nje ya nchi. Nishawahi kuitumia Doha, London, na kwingineko.
Card za Visa wanazo pia ndiyo ninayoitumia mimi
 
ulipotoa pesa zako nbc walikupa hundi ama pesa taslimu?

Na kufungua akaunti hapo crdb ilichukua muda gani?


mimi ilinichukua si zaidi ya lisaa limoja kufungua akaunti pamoja na kupewa visa kadi yangu...
 
Sina hakika sana kuhusu Visa lakini MasterCard wanazo na ninayo yangu hapa naitazama sasa hivi. Na inafanya kazi ndani na nje ya nchi. Nishawahi kuitumia Doha, London, na kwingineko.

Visa na mastercard zipo Kwa wenye card mpya
 
Nilidhani umehamia WB kumbe umehamisha Ac kwenye kabenki kengine katanzania? Subir utawajua tuu hao crdb wako. Siku utakapopata mshahara tarehe 35 ndipo utakapoitamami nmb nao watakugonga makakato ya kijinga utaitamani dcb mwisho wa siku utajikuta upo women bank. Hizo benk za kibongo zote sawa tuu utaishia kuzunguuka tu

Afadhali za Tanzania kuliko hiyo ya Mkapa, Yona na Makaburu toka South Africa.
 
Nilidhani umehamia WB kumbe umehamisha Ac kwenye kabenki kengine katanzania? Subir utawajua tuu hao crdb wako. Siku utakapopata mshahara tarehe 35 ndipo utakapoitamami nmb nao watakugonga makakato ya kijinga utaitamani dcb mwisho wa siku utajikuta upo women bank. Hizo benk za kibongo zote sawa tuu utaishia kuzunguuka tu

Utajiju na kijiba chako cha roho au na ww mdioker wa nbc nn kudadadeki
 
Huduma zao za kiwango cha kimataifa, wako wazi, hakuna kuzungushana na haraka. Ugunguaji account mpya ni kitambulisho chako kama passport, leseni ya udereva, kitambulisho cha taifa, kama huna basi utatakiwa uwe na barua ya mwenyekiti wa serikali za mitaa. Tofauti huku NBC unahenyeshwa kama si raia na vitambulisho haikubaliki mpaka barua ya mwenyekiti serikali za mitaa na pengine wakudai pia notary mahakamani.

Some time wanahitaji mpaka utambulisho wa wakwe zako sa cjui manake nn kama c matusi yan hawa watu kboko
 
Back
Top Bottom