Asante Mungu leo nimewahama Rasmi NBC

Asante Mungu leo nimewahama Rasmi NBC

Si uongo NBC Kimeo, naanza mkakati..... new bank account, nahamisha mshahara, nitawabwaga bwaaaaaaaaaaaaaa
 
Ila umatumbini kwetu nuksi sana mkuu...

By then wakati ndio ATM zinaanza kuwa installed, na watu kuanza kuzitumia basi kulizuka ujambazi wa kubomoa vibanda vya ATM....imebidi ziwe zinalindwa sasa.

Halafu pia nashangaa Bongo nzima sijawahi kuona Deposit Friendly ATM's, sijui kama kuna benki ina hii kitu aisee...

Jana waliniambia wanaleta hzo machine mdau njoo huku hakuna shida
 
Nbc ndo baba lao benki zote ni watoto we mshamba umechemka sana kuihama benki kubwa kuliko zote na wote mnaohama mabenki ni washamba
 
Alafu ukitaka kufanya T/T za nje rate zao balaaa kudadadeki, mwezi uliopita niliagiza gari kupitia huko walicharge 1 usd kwa 1800 nikagoma na ugomvi juu wakanipa 1720 na ukienda kuchange nje hawataki kutuma mpaka uwe na acc hapo yan hii bank haifai bora iwe saccos tu tena ya wapaa samaki pale feri manina zao
 
Hii sio ndio benki aliyouza Che Nkapa kwa bei ya kutupa? Laana za Nyerere zitaimaliza. Ndio maana hata Che Nkapa mwenyewe akachanganyikiwa akapotea hata njia ya kwenda kwao baada ya kustafu badala ya kwenda Ntwara kijijini kwake kama alivyokafanya nzee Nyerere yeye akaelekea Ushoto. Na bado! Si ajabu tukasikia kahamia Somalia. Chezea nzee Nyerere wewe! Nzee kahangaika kajenga viwanda na mashirika mengi ya umma kama hiyo benki lakini Che Nkapa alipoingia kapiga minada vyote hata visivyostahili. Walipoona haitoshi wakachukua hata hata Ngodi wetu wa Kiwira nanyumba za serikali alizokajenga nzee. Hizo hata kuishi hawana amani nazo. Tamaa mbaya!
 
Baada ya kuwavumilia kwa takriban miaka minane na manyanyaso, Huduma mbovu ndani ya benk kadhalika na Atm machine zao, LEO nimeamua kuachana kabisa na benki hii kwa kufanya mambo yafuatayo
1; nimehamisha salio langu lote
2; nimevunja kadi zao zote kuanzia utambulisho mpaka atm kadi zao
3;nimehamisha mshahara kupitia kwao kudadadeki zao
4;nimezinguana na costomer service manager wao
wa tawi moja hapa town
5;nimekuja kuwapa taarifa humu wana jf wenzangu wanaofikiria kujiunga na benk hii wasithubutu itakula kwao.
Benk hawataki kubadirika, kazi kuajiri midioker tu na watu wasiojiweza, mtu dirishani kwa teller anatumia zaidi ya nusu saa bila sababu ya msingi, na siyo dar tu nimeenda matawi yao kibao kama Tabora, morogoro, dar ndo balaa, mtwARA ndo shida kabisa kudadadeki zao, nimejiendea CRDB yan burudani kumbe nilikuwa nachelewa tu siku zote hz, hongereni CRDB hasa holland branch kwa kazi nzuri.
Wewe utakuwa Marketing Manager wa CRDB, lakini unajaribu kujificha kwenye koti la aliyekuwa mteja wa benki ya NBC!
 
Nilikuwa mteja wa nbc tangu 2008,hivi majuzi mwaka huu mwezi wa tisa nikawaomba kamkopo kadogo tuuu.wakanizungusha weeeeeh na vigezo vyao kibao.nikaona heee kumbe hii ni benki ya ccm.....kwa hasira nikatoa pesa zangu zote!!!!!eti ikabaki 4600 ikagoma kutoka kwenye ATM.....nikatumia sim banking nikaweka vocha yoooooooote.ile kadi yao nakampa jamaa mmoja gerage awe anapakia puti.
Sasa niko ACB nafurahia huduma bora za kibenki.NBC tupa kuleeeeeee
 
Wewe utakuwa Marketing Manager wa CRDB, lakini unajaribu kujificha kwenye koti la aliyekuwa mteja wa benki ya NBC!

Hapana mdau mi ni mwathirika tu wa bank hyo yan ndi ilikuwa benk yangu namba 1 kwa miaka minane lakin hizi siku za hv karibuni wamekwamisha mambo yangu mengi kwa huduma za mbovu, nimewavumilia sana kudadadeki zao acha tu.
 
Nadiliki kusema NBC tawi la KAHAMA ndilo tawi linaloongoza kuwanyanyapaa wateja wake kuliko matawi yote
mimi nilipoteza kadi yangu ya NBC nikiwa huku kahama,nikafata taratibu zote za kuripoti polisi na kila kitu kinachotakiwa kufanywa,cha ajabu nilipotaka huduma ya kutoa pesa kupitia kwa teller eti wwakanambia haiwezekani mpaka nirudi tawi husika nililiofungua account..ilibidi niwafundishe kazi kwamba wanaweza wakawasiliana na tawi lao la UDSM ili wanipe 'go ahead' jibu walilonipa ndilo lililonifanya niwahame, eti tuko bize kwasasa na pia mtandao unasumbua?! sitamsahau kale kadada kallichonijbu hivyo maana nilikuwa na shida ya muhimu sana na pesa kwa wakati ule na hajui tu ni nini alinisababishia kukikosa kutokana na kiburi chake.
NBC tawi la KAHAMA wana ubaguzi wa wateja..Kuna wateja wakiingia ndani wanahudumiwa kama wafalme na huwa hata foleni hawapangi,wamekaa kujuana juana sana achilia mbali wasukuma wenye mihela yao wakija ndani,yaani wengine wote mtatolewa nje kama wezi mpaka mijamaa imalize shida yao ndo mnaambiwa muingie ndani..bora wangesema tu NBC tawi la kahama ni kwa ajili ya wanyantunzu na wasukuma matajiri tujue moja kuliko kutunyanyapaa wateja wengine.
 
Crdb wenyewe wanajisahau sana, foleni za kijinga. Wananichosha sana. Wateja wanakuwa kwa kasi ila hawatanui matawi yao hasa zile sehemu zenye mizunguko mikubwa kama dar. Ukienda mcity kama mtu usiependa foleni utaishia kukasirika tu


Kuna siku nilienda hapo nikiwa na haraka nikatamani kupasuka kwa hasira

Akaribie ila uvumilivu muhimu
 
Mimi nilihamisha salio langu loooteee mwaka jana mwshonibaccount ikabaki empty...last week nikatumiwa text eti account yangu imeblokiwa so niende nikahakiki na kuupdate taarifa zangu wkt nilishafanya hivyo....mafala sana
 
Mkuu hapo kwenye west ulitaka maanisha nini? Au ulitaka sema waste??
Just ignore, (he is wasting time with NBC). Tunahangaika na dhana kubwa haya mambo ya spelling ni madogo na wanaofikiri kidogo ndio they mind.
 
Sijui kwa siku za karibuni lakini hao CRDB zamani walikuwa wananikera sana na kile kipengele chao cha kuwa na mdhamini ambaye ni mteja wa CRDB pindi unapotaka kufungua akaunti CRDB.

Pia kwenye matawi yao hususani hapo Dar es Salaam, huwa yanajaza sana wateja kiasi kwamba inakubidi usubiri sana kupata huduma. Kuna matawi sugu kwa kuwa na watu wengi haswa yale ya mjini kati kama Holland, Azikiwe na pia pale PPF Tower...Mlimani City ndio usikaribie kabisa maana hadi kwa ATM mshine kuna msururu utadhani enzi za kununua Yanga yanga....

Hata hivyo kwa sasa mji kama wa Dar es Salaam una mabenki mengi tu yenye huduma zisizo na usumbufu zenye kujali muda pia. Pengine alternative hiyo ya CRDB ni muafaka kwa wale watumiaji wa huduma za mabenki walio nje ya Dar...

watu8

Masuala ya kuwa na wadhamini watatu wenye account hapo CRDB yamebaki kule NBC tu. CRDB ni kitambulisho chako kinachotambuliwa na serikali na kama huna basi barua ya mwenyekiti wa serikali za kitongoji unachoishi mambo yatakuwa poa.

Msongamano CRDB si mkubwa kama NBC. Jengo la pale PPF mkabala na Posta mpya pamoja na kuwa na wateja wengi kuna matawi mawili ili kupunguza msongamano yameuatana hapo hapo na ATM nyingi.

Kwa vile mteja ni kama mfalme wameweka viti wakati unasubiria kwenda counter unakaa kwenye viti na kusogea mbele kutoka kiti kimoja hadi kingine hadi unafika kwa counter unatokea kwenye seat. Mambo hayo NBC huwezi kupata kamwe.

Mlimani city kuna wateja wengi yes, mimi huwa napendelea pale mjini wana matawi mengi na hakuna usumbufu kabisa kama ni kusubiri basi ni dakika chache.

Barabara ya Nyerere (Pugu road) toka mjini kabla ya Tazara kuna matawi mawili pale Shope and Relax, wanakasi sana katika huduma zao.

Hii ni bank inawafaa na kuwajali sana wafanyakazi, wafanya biashara na wasomi wanaojali muda na uwazi, na ndio maana wanazidi kutanua matawi nchini.

Morogoro kuna matawi mawili, moja kubwa sana pale karibu na kituo cha mabasi cha daladala Masika kabla hujafika kituo kikuu cha daladala mjini. na pale kona ya kwenda uwanja wa mpira au polisi kuna tawi lao pia. Hawa jamaa wanazidi kukata mbuga kiulaini.

:msela:KILA MWEZI WATAKUTUMIA BANK STATEMENT KWENYE EMAIL YAKO:msela:​
 
Halafu huwezi kutoa zaidi ya Tshs. 200,000/- kwenye ATM zao kwa mkupuo. Imagine unataka kutoa 1M!

Maximum amount ni 400,000 kwa mkupuo mmoja. Ukitaka millioni moja itabidi utoe mara 3
 
Back
Top Bottom