Arusha: Watoto watatu waliwa na Simba

Arusha: Watoto watatu waliwa na Simba

Jembe Jembe

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2016
Posts
757
Reaction score
1,822
Watoto watatu kati ya wanne ambao ni wanafunzi wa shule ya Msingi Ngoile na wakazi wa kijijj Cha Ngoile wilayani Ngorongoro Mkoani hapa wameuawa kwa kuliwa na Simba huku mmoja akijeruhiwa wakati wakitoka shuleni.

Akiongea ofisini Kwa kamanda wa polisi Mkoa wa Arusha Justine Masejo aliwataja wanafunzi hao kuwa ni Olobiko Metui(10),Ndaskoi Sangau(9) na Sanka Saning'o (10) ambao wote ni wanafunzi wa darasa la tatu .

Aidha kamanda amedai kuwa kati ya watoto hao ,mtoto mmoja,Kiambwa Lektonyi(11) alinusurika kifo baada ya kujeruhiwa vibaya na Simba na anapatiwa matibabu katika hospitali ya wilaya hiyo.

Masejo alifafanua kuwa tukio hilo limetokea juzi agosti 3 mwaka huu majira ya saa nne asubuhi katika Kijiji hicho wakati wanafunzi hao wakijerea nyumbani kutoka shuleni .

Ends.....
 
"...majira ya saa nne asubuhi katika Kijiji hicho wakati wanafunzi hao wakijerea nyumbani kutoka shuleni ..."

hiyo shule wanafunzi wanaenda shule mdaga gani na wanatoka muda gani? ama walikuwa wameelekezwa warejee nyumbani na walimu?
 
"...majira ya saa nne asubuhi katika Kijiji hicho wakati wanafunzi hao wakijerea nyumbani kutoka shuleni ..."

hiyo shule wanafunzi wanaenda shule mdaga gani na wanatoka muda gani? ama walikuwa wameelekezwa warejee nyumbani na walimu?
Hii shule ,afisa Elimu mkoa wa Arusha hajawahi kufika hapo tangu ianzishwe
 
Back
Top Bottom