Arusha: Watoto watatu waliwa na Simba

Arusha: Watoto watatu waliwa na Simba

Simba walikuwa wangapi? Simba mmoja hawezi kula watoto watatu kwa wakati mmoja/Simultaneously.
 
Sijui, ila wenyewe wanajua na watamtafuta, watu wanatafuta hadi mamba aliekula mtu na wanamkamata wanamuua.
... huko chama miaka yote kinapita kwa ushindi wa kimbunga cha ajabu! Hao ndio wapiga kura wetu waaminifu (loyal). Kwani simba wameanza kula watu leo? Hebu mtupishe!
Wamasai huwa hawauliwi na simba kuna dawa hupaka hawa watoto imekuwaje aisee, inasikitisha sana
Wamasai hameni mbugani.
Pole kwa wafiwa.
Ngorongoro ni hifadhi ya taifa ambayo kuna watu wakiwa na mifugo yao wameamua kuishi pamoja na wanyama pori. Ni vema watu na wanyamapori wayazungumze yaishe. Yanazungumzika tu, maana ndio maajabu ya dunia.
 
Kwa majina na eneo itakuwa jamii ya Wamasai ambao wanaishi jirani sana na simba. Hio ni ajali tu, ila huyo simba atatafutwa hadi auawe kwasababu kashaonja nyama ya mtu hataacha.
Kwamba ndio nyama tamu kuliko zote kwa simba au imekaaje hiyo mkuu??
 
... watamjuaje kwamba huyu ndiye aliyewala?
Hatakuwa mbali na eneo hilo. Probably huyo (hao) simba ni mbarara (nomads) ambae anakuwa amefukuzwa kwenye pride so anazurura hovyo hivyo ni rahisi ku identify simba kama huyo.

Lakini kutokana na sheria za maliasili na vile NCAA wanavyotoa elimu kwa wafugaji jinsi ya kuishi humo na wanyama pori sio rahisi kuuwawa huyo simba maana ni ajali tu kama nyingine.
 
"...majira ya saa nne asubuhi katika Kijiji hicho wakati wanafunzi hao wakijerea nyumbani kutoka shuleni ..."

hiyo shule wanafunzi wanaenda shule mdaga gani na wanatoka muda gani? ama walikuwa wameelekezwa warejee nyumbani na walimu?

Nilisoma sehemu kwamba hao watoto walikuwa wanatafuta mifugo(Mbuzi) yao iliyopotea ndio wakavamiwa na kikundi cha simba ,watoto watatu wameuawa ila mmoja amejeruhiwa.
 
Wamasai huwa hawauliwi na simba kuna dawa hupaka hawa watoto imekuwaje aisee, inasikitisha sana

Ile dawa yao ni hatari inanuka balaa ,kuna siku kuna mmasai mwanadada alipanda basi alitokea mvomero akawa anaenda msamvu ,noma abiria ilibidi wamwambie dereva amshushe alikuwa anatema harufu kali ndio wadau wakasema ni dawa yao ili wasivamiwe na wanyama wakali.
 
Ile dawa yao ni hatari inanuka balaa ,kuna siku kuna mmasai mwanadada alipanda basi alitokea mvomero akawa anaenda msamvu ,noma abiria ilibidi wamwambie dereva amshushe alikuwa anatema harufu kali ndio wadau wakasema ni dawa yao ili wasivamiwe na wanyama wakali.
Sio kweli bro King Kong. Watu huwa wanaaminishwa myths tu na wanakubali na kusambaza kama vile ni kweli.

Hizo harufu ni uchafu wake tu kutokana na kutokuoga, kuhudumia ng'ombe (kukamua maziwa), kulala sehemu chafu n.k ndio zinafanya mtu atoe harufu hizo mbaya.
 
Watoto watatu kati ya wanne ambao ni wanafunzi wa shule ya Msingi Ngoile na wakazi wa kijijj Cha Ngoile wilayani Ngorongoro Mkoani hapa wameuawa kwa kuliwa na Simba huku mmoja akijeruhiwa wakati wakitoka shuleni.

Akiongea ofisini Kwa kamanda wa polisi Mkoa wa Arusha Justine Masejo aliwataja wanafunzi hao kuwa ni Olobiko Metui(10),Ndaskoi Sangau(9) na Sanka Saning'o (10) ambao wote ni wanafunzi wa darasa la tatu .

Aidha kamanda amedai kuwa kati ya watoto hao ,mtoto mmoja,Kiambwa Lektonyi(11) alinusurika kifo baada ya kujeruhiwa vibaya na Simba na anapatiwa matibabu katika hospitali ya wilaya hiyo.

Masejo alifafanua kuwa tukio hilo limetokea juzi agosti 3 mwaka huu majira ya saa nne asubuhi katika Kijiji hicho wakati wanafunzi hao wakijerea nyumbani kutoka shuleni .

Ends.....
Ndio akili ya mmasai anathamini mifugo mpka simba kaua familia yake...navyowajua hapo wanahasira n huyo simba sema hawawezi kumsaka
 
Back
Top Bottom