Inside10
JF-Expert Member
- May 20, 2011
- 33,614
- 40,161
Mwanaume mmoja anayefahamika kwa jina la Baraka Melami (40) mkazi wa kitongoji cha juhudi kijiji cha Olevolosi kata kimnyaki wilayani Arumeru Mkoani Arusha amekatwa uume wake na mkewe anayejulikana kwa jina la Anna Melami miaka (30) usiku wa kuamkia tar 19 saa saba usiku.
Akisimulia kisa hicho Baraka amesema kuwa jana usiku mkewe alimsogelea kitandani akijua anataka kufanya tendo la ndoa lakini baada ya baraka kupata hisia mkewe alishika kisu na kukata sehemu hiyo ya siri na kuiondoa kabisa kisha kuitupia chini ya uvungu wa kitanda.
Amesema kuwa kwa kuwa alijua mkewe nia yake ni njema pia alifungulia radio sauti ya juu na hata Baraka alipokuwa anapiga kelele kuomba msaada hakuna mtu alimsikia mpaka alipotoka nje na kupiga kelele na watu kumsaidia kumkimbiza hospitali.
Hata hivyo Baraka ameomba watanzania wenye nia njema wamsaidie matibabu ambapo kwasasa amelazwa katika hospitali ya Selian ya Ngaramtoni Arusha.
Mwenyekiti wa Kitongoji hicho cha Juhudi bwana Jonas Kisite amethibitisha kutokea kwa tukio hilo baada ya kupigiwa simu majira ya usiku na majirani wa Baraka.
Akisimulia kisa hicho Baraka amesema kuwa jana usiku mkewe alimsogelea kitandani akijua anataka kufanya tendo la ndoa lakini baada ya baraka kupata hisia mkewe alishika kisu na kukata sehemu hiyo ya siri na kuiondoa kabisa kisha kuitupia chini ya uvungu wa kitanda.
Amesema kuwa kwa kuwa alijua mkewe nia yake ni njema pia alifungulia radio sauti ya juu na hata Baraka alipokuwa anapiga kelele kuomba msaada hakuna mtu alimsikia mpaka alipotoka nje na kupiga kelele na watu kumsaidia kumkimbiza hospitali.
Hata hivyo Baraka ameomba watanzania wenye nia njema wamsaidie matibabu ambapo kwasasa amelazwa katika hospitali ya Selian ya Ngaramtoni Arusha.
Mwenyekiti wa Kitongoji hicho cha Juhudi bwana Jonas Kisite amethibitisha kutokea kwa tukio hilo baada ya kupigiwa simu majira ya usiku na majirani wa Baraka.