Arsenal (The Gunners) | Special Thread

We Mpira hujui bora ukafatilie mieleka. Nyie mna mchezaji wa kumweka nje Skelly? Hembu kuweni serious
 
Mashabiki wa Arsenal mna zero knowledge of football kwenu kila mchezaji ni Bora kama tu anacheza kwenu
Nimekuelewa mkuu maana kuna wachezaji wanabebwa na mfumo na wengine hata peak ya timu inamfanya aonekane mzuri. Kimsingi sisi mashabiki wengi tunaangalia mpira wa matokeo ila sio process ya kupata matokeo.

Ndio maana sijawahi kumkubali mchezaji anaitwa Rashford hata kama anafunga goli kibao
 
Umeongea short and Clear ndio maana Barca wakamuacha Rashford ni kweli mchezaji wa kawaida. Mfano mzuri Gabriel na Saliba wanasifika kuwa ni best defenders kwenye ligi lakini ukiangalia mpira vizuri wanabebwa na system ya uchezaji wa Arteta, Arsenal wanakaba as team work wanaacha space ndogo baina ya mstari mmoja kwenda mwingine ndio maana inakuwa ngumu sana kufikika mara kwa mara golini kwao na ukitaka kuliona Hilo umemuona vizuri Gabriel kule World cup na Brazil yake alivyokuwa anapinduliwa pinduliwa ovyo ovyo ile ndio level halisi ya mchezaji mwenyewe. Wachezaji ambao unaweza kusema wapo level ya juu wanajiweza wao Wenyewe ni wawili tu pale Arsenal ni Declain Rice na Kipa wao Raya. Leo hii Bruno Fernandes anachukuliwa kawaida pale Man u ni kwasababu ya performance ya Team yake lakini yeye kama yeye ni mchezaji wa daraja la juu. Hakuna team yoyote atakayoenda alafu akaa benchi hivi vitu mashabiki wa Arsenal hawawezi kuona ni kwamba hawana uelewa ila wachezaji wengi wa Arsenal ni wa kawaida wanabebwa na performance ya team nzima mpaka wale wa kawaida wanaonekana wanajua.
999 chatta
Castr
mkorea
Henry 14
 
Mimi Yamal, asee yule mtoto sijawahigi kumuelewa hata kidogo, anatembea na nyota ya barca na spain
 
Upo sahihi kabisa Mkuu. EPL hua haina mwenyewe, usajili pekee hautoshi. Majeruhi, bahati , fomu ya wachezaji nk nk.
Niwatakie Kila la kheri kutetea ubingwa msimu ujao.

YNWA
 
Updates: Usajili- Arsenal wafanya mazungumzo na Aston Villa kumsajili beki wa kati Ezri Konsa.


Ezri Konsa, beki wa kati wa Aston Villa na timu ya taifa ya Uingereza.

Kwa mujibu wa jarida la The Athletic, mazungumzo kati ya klabu hizo mbili yamefanywakatika "level" ya wamiliki ambapo wamiliki wa timu hizo mbili ambao ni wamarekani wamefikia makubaliano kwamba ada ya usajili ipunguzwe.

Aston Villa walikuwa wameweka dau la pauni milioni 60 ambazo Arsenal hawakuwa tiyari kukubali na sasa baada ya mazungumzo katika ngazi za huko juu, dau hilo laweza kushuka hadi pauni milioni 35 au 40.

Wakati huo huo mshambuliaji Gabriel Jesus nae yumo katika mchakato wa kwenda Napoli endapo ada ya uhamishowake itakubaliwa kati ya klabu hizo mbili.

Tuendelee kusikilizia yanojiri katika dirisha hili la usajili ambalo sasa limeshika kasi kabla ya ligi kuanza, inagwa dirisha hilo litafungwa tarehe 31 mwezi huu wa August.
 
Usajili Updates: Arsenal wakubaliana na Aston Villa kumsajili beki wa kati Ezri Konsa kwa pauni milioni 51.

Arsenal imekubali kulipa dau la pauni milioni 51 kwa Aston Villa kumsajili beki wa kati Ezri Konsa.

Konsa ambae pia ni beki wa kati wa timu ya taifa ya Uingereza ataelekea London jioni hii kwa ajili ya kufanyiwa vipimo vya afya yake.

Konsa ambae amekuwa target ya muda mrefu ya Arsenal hucheza nafasi ya beki wa kati na hata upande wa kulia na meneja Arteta amekuwa akilenga kuimarisha safu ya ulinzi ya mabingwa hao wa ligi kuu ya Uingereza.

Konsa atakuwa mchezaji wa nne kusajiliwa na Arsenal baada ya Bruno, Guimaraes, Christos Tzolis, Illan Meslier ambae ni kipa kutoka Leed United,

Ikiwa masuala yote yatakamilika by Ijumaa, basi Konsa atacheza mechi ya kwanza ya msimu wa ligi kati ya Arsenal na Coventry City ijumaa jioni.
 
Ni jambo zuri hili kwetu, ukizingatia ana miaka 28? Naona kama si jambo baya maana Timber, Saliba, White bado wana shida za fitness. Haswa Saliba, ambaye Konsa ameletwa makusudi kuziba pengo lake ili tusimtegemee Mosquera pekee yake kuziba nafasi ya RCB na RB.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…