Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Kweli jamaa ni mbaguzi sana,Parteyaliondoka bure,kwenye game mbili za mwisho tumepoteza point tano
 
Shambolic defending,

3 on target, zote goli.
Arsenal kwenye kulinda ni mbovu. Anaokolewa sana na kushambulia ila ukiwatia presha huwa wanafungwa sana tu.
Na timu hizi zinazocheza low block na kubana nafasi zote ujue kazi kuwafunga ndo tukaja na mbinu ya kona ila Arteta aache kukalili ndo maana huwa timu zinatushangaza kama hivi ila ndo mbinu za mwalimu kuzidiwa.
Timu letu pia linawavivu kibao ni kama kukaba wameachiwa mabeki peke yao.
 
Nasema hv, wageni wote wameshinda, Kama hutaki kufa 😂
 
Wewe hii false hopes mbona ya mbaliii hivi ubaguzi wa africa unaingiaje kwenye kipigo cha leo , tafuta false hopes nyingine hii nimeikataa
 
Arsenal inawachezaji nyoronyoro ndo maana timu ikitupa game tough hatutoboi zaidi ya sare au kufungwa.Angaliaga game za Astonvilla au Newcastle, Arseanal anapata sana shida sababu jamaa huwa hawanaga abiria uwanjani na hawakabi kwa macho. Arsenal tutazionea timu nyoronyoro kama sisi. Sasa Rice ndo akabe na kushambulia peke yake uwanje mzima.
 
Kabisa, eneo lile unaachaje cunha ana drible hadi anapiga. Hakunantracking wala quick blocking
 
Mbadilike kenge nyie team inategemea set piece na kuwazuia makipa kwenye kona
Timu hata kasi haina sababu wengi kung'ang'ania mpira. Yaan mpaka anaachia pasi basi timu pinzani imeshaweka shape yake yakujilinda. Unakuta wanaanza kupiga back passes ambazo haina maana zaidi yakuchoma tu. Na wakiona timu haitoki mpaka mabeki wanaenda kuongeza idadi kushambulia hapa ndo inapokujaga hatari Arsenal akipoteza mpira kwenye eneo la mpinzani..Anakuwa wazi tu nyuma na watu wanakimbia kwenye space kuwashambulia.Arteta ajaribu kuja na mbinu timu icheze style tofautitofauti na atafute wachezaji tough siyo wote waaina moja shida lazima iwepo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…