Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Dunia inaenda Kasi sana.
Kaumia Kai yupo victor
Kaumia odegadinho yupo nanweri
Kaumia Saka yupo madueke
Nje una trossard,merino na eze eberech.

Unalitazama bench unamuona kiwior,white,mosquera,Lewis kipa level za kepa Yuko nje.

Halafu una kiwembe kama Downman kinasubiri dakika chache tu kilete matatizo makubwa.on paper tuna a good squad ila maisha yanahitaji sana "BAHATI" bahati ikiwa upande wetu labda tunaweza pata kitu msimu huu
 
Bahati kama ya first match, una shambuliwa ila still una pata point 3.
 
Kuna rhythm tumeipoteza, japo game ya kwanza na man u tulikuwa hovyo zaidi, hii kipindi cha kwanza tukawa hovyo cha pili kwa mbaali tuwa arsenal, lakini chama hili bado..
Huyu ZUBIMENDI atulize akili, hajakaa sawa.
Odegaard ni kiazi, anaforce sana kukaa na mali, kibaya zaidi yule mtoto nwanweri nae anaiga ujinga ule ule..
Kuna sehemu kadhaa gyokeres alikuwa anatengeneza mikimbio na wao hawapasii wanaung'ang'ania mpira bila sababu za msingi..
Tumjaribu na eze tuone ataongeza nini, ila bado hatujawa vizuri.
 
Mdogo mdogo gari lita changanya to
 
naona mwenyewe umejiachiiiia kwenye keyboard unatype tu. Tuombe uhai hiyo next week
 
Ule upuuzi anaofanya Odegaard na Nwaneri utasababisha tusiuone ubora wa Bouncer lenu Gyokeres, yaani mtu anajijua kabisa yeye sio Messi halafu analazimisha kukaa na mali mguuni muda ambao Gyokeres tayari ashajipatia position muruwa kabisa, matokeo yake kujigongagonga kama Budo Mutale possession lost no chance created. Mlikuwa sahihi kukomalia deal la Eze coz inaeleweka Mateta ameenjoy sana pass zake.
 
Huenda Eze akamuweka Ode bench na Gyökeres, Madueke na akina Martinelli na Trossard wote wakafaidi sana na uwepo wake.
 
Misimu kadhaa tumekuwa tukianza kasi sana halafu baadae tunakata moto.

Kuanza kwa gia hii naona iko poa muhimu tubebe 3points na magoli ya maana.

Ukiangalia mara nyingi mabingwa wa Epl huwa wanaanza na gia ndogo wanaenda huku wanaongeza kasi hii husaidia hata players kusave energy.

Hawa kina Saka na Ode ni heri waumie mapema ili wawe fit nyakat muhimu tutakazowahitaji.

Arteta akikosa Epl au Uefa basi wamuwambe makofi na afukuzwe sa 7 mchana.
 
Wanaona wanamtania kumuita Jokeres kumbe wanamsifia
Baada ya Saka kuumia nasikia Tetea Kiwigi anaenda ku-hijack dili la Isak ili jumapili awepo dhidi ya Liverpool pale kwenye dimba la Kuku choma (Anfield)
Tokea jana usiku Isak kafanya mgomo wa kula na kupumua akishinikiza Newcastle wafanye haraka kukamilisha hili dili ili jumatatu atue Arsenyo.
Isak haitaki timu yoyote anaitaka Arsenyo.
Here we go soon.
 
Mashabiki wa mid table team mna tabu saba.
 
Eze amesikia kilio chenu ndugu zangu....yule Odegaard akae nje kidogo...Captain unakuwa bishoo sana kama nn sijui.....
Msichokijua huyo Mmasai wenu Eberechi Kili Paul Eze ni black version ya Jack Grealish.
Jipeni false hope za kutosha lakini baadae hatutaki kuwasikia mnamtukana huyo muimba kuchikuchi wenu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…