Flano
JF-Expert Member
- Aug 7, 2019
- 5,844
- 16,298
Unaachaje wali nazi wa maharage nazi matata na kikombe cha chai tangawizi pembeni kisa umetafuna jiwe moja kwa bahati mbaya?
Usiache kuenjoy kina Gyokeres na Saka watakvyokuwa wanamimina magoli malangoni mwa akina nyumbu na kenge kisa Noni. Tena huyo Noni huenda atafanya vizuri kuliko Sterling. Ukiachana na Arsenal, hutaki kuwacheki kina Vini, Yamal, Bruno na Salah kisa Noni?
Naomba urudishe moyo nyuma na uzingatie upya uamuzi wako. Naona kile unachojimyima hakiendani na sababu ya kujinyima hicho kitu.
Muacheni Castr apumzike kwanza, mtu mpaka akifikia hatua ya kuomba watu wasimquote ujue ameshavulia sana mpaka uvumilivu umefikia mwisho, ni hatari sana kwa afya ya mwili na akili kuendelea kumng'ang'aniza mtu kwa jambo linalomnyima furaha.
Walikuwepo kina Labyrinth 84 wakahama timu kwa maumivu makali, walikuwepo kina Masingeli wakiwaongopea watu humu kwa false hope kama wewe halafu mwisho wa siku wamelikimbia jukwaa kwa uchungu mkubwa.