Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Ndio kufeli kwenyewe huko, tusitafute excuse, alifeli.
 
Nilijua tu Maktaba kuu Flano akiiona tu hii post lazima atakuja na maneno mengi.
Nimefurahi sana kumuona mkorea chawa kindakindaki wa Masingeli analia kwa uchungu mkubwa kua Masingile alimuingiza chaka kwa zile analysis zake za pressing & Overloading

Ila Masingeli ni Konyo sana yule mtu kwa ushawishi, yule anaweza kuwaaminisha kua Kai Harvez ni Black baba yake ni Msenegal na kundi la watu humu wakaamini, yaani Masingeli kama sio dalali wa Magomeni basi atakua na undugu na yule msela aliemshawishi mama yetu kula tunda kule bustanini
 
Ndio kufeli kwenyewe huko, tusitafute excuse, alifeli.
Sio kufeli kwani kipindi fabregas yupo Barca akawa hapati namba ya mara kwa mara kwani alikuwa mmbaya au ni kwasababu nafasi alikuwa anacheza ilikuwa ni ngumu kupata namba baada ya kuamia Chelsea akawa top assist. Kukosa namba sehemu Kuna sababu kuu mbili moja ni kusidiwa uwezo, mbili preference ya kocha kulingana na mfumo wake
 
Nacheka sana nyumbu wanavyogombana kisa kutosajili
Ni mwanzo wa July. Siyo muda wa kujistress sana japo timu zinaweza kuonekana kama hazifanyi kitu. Huku kwetu sisi wenyewe tulikuwa tunastress na bado tunastress kuhusu sajili. Hata pale tulipojua tumeshamchukua Zubimendi, watu walipata wasiwasi kuwa Madrid wanaweza kumchukua. Watu walibidi wahakikishiwe kuwa jamaa tumempata May ila hatutamtangaza mpaka July kwa sababu za kifedha ila haikusaidia sana kuwapa amani. Na mpaka sasa bado tunastress maana kama mashabiki tunataka tuwe tumeshamaliza kusajili na kuuza wachezaji ili tuwe tuanawatambia na kuwapiga biti akina Nyumbuz na Chelkenge na kuwaonya wasiingize timu uwanjani ila hatuoni hizo sajili mapema...

Manyumbu watulie tu. Sajili zitakuja tu.

Cha muhimu ni waelewe kuwa sajili zao hazitawasaidia chochote. Bado sisi na timu zingine tutaendelea kujipigia na kuchota points 6 au zaidi kwao kama kawa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…