HENRY14
JF-Expert Member
- May 13, 2021
- 3,643
- 7,073
Partey anlipaswa kukatwa 50k au zaidi kwenye mkataba wake, siyo kuongezewa. Ni mzuri sana ila muda mwingi huwa hayupo uwanjani.Policy yetu ya uhamisho (kuuza na kununua) ni hovyo. Wakati mwingine tunatumia akili ndogo kufanya maamuzi. Hebu niambie:
Partey alikuwa anataka nyongeza ya £50k ili aendelee kubaki, ambapo kwa mwaka angekula £600k zaidi. Lakini kwa akili ndogo za Arteta na Berta wakaaona ni heri kutoa £10m kumnunua Norgaard kuliko kumuongeza Partey 50k.
Ni akili za kijinga sana. Ukiwa na watu wapumbavu kama hawa kwenye kampuni, huwezi kufanikiwa