Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Kiungo na ukuta huko hakuna shida kabisa, tena naona cleansheets zitakua zakutosha
Nyumbu, kenge etc watakula kipigo cha mbwa, points 6 with cleansheets
Kidura kinaendelea, muda wa usajili tambo kibaaaooo, msimu uanze muanze kusifia overload na download, mwisho wa msimu holaaa. Mnarudi tena kwnye usajili tambo kama hizi😂😂😂
 
Kidura kinaendelea, muda wa usajili tambo kibaaaooo, msimu uanze muanze kusifia overload na download, mwisho wa msimu holaaa. Mnarudi tena kwnye usajili tambo kama hizi😂😂😂
Wacha maneno weweeee. Hapo saizi kina Kolpama wanajiuliza watakuwa wanapita wapi. Halafu tunaleta mmoja kati ya Gyokeres au Sesko...au wote tu, kwani shida iko wapi?...huku akina Badiashile nao wanajiuliza hii Arsenali ni nani wa kuizuia..?...
 
Wacha maneno weweeee. Hapo saizi kina Kolpama wanajiuliza watakuwa wanapita wapi. Halafu tunaleta mmoja kati ya Gyokeres au Sesko...au wote tu, kwani shida iko wapi?...huku akina Badiashile nao wanajiuliza hii Arsenali ni nani wa kuizuia..?...
Msisahau kumchukua na Madueke pls. Atawasaidia sana kwenye mbio za big4.
 
Clinical finisher
Rw
Lw

Hapo arteta na beta watulize akili, watuletee watu wa kazi
Nimeangalia YouTube tu ila nafikiri tutafute mabeki wawili - Jorrel Hato wa Ajax na Alexsandro wa Lille. Hato ni mfano wa Timber na Alexsandro ni mfano wa Gabriel na Kiwior na anatumia miguu yote vizuri. Ikiwa tuchukue mmoja tu basi naenda na Alexsandro. Tomiyasu anaumia sana, Tierney ameondoka na Zinchenko huenda akaondoka pia. Hapo tumalizane na upande wa ulinzi.

Mido - Zubi amekuja na Partey akiondoka sifikirii kuleta mtu mwingine katikati japo Jorginho ameondoka pia. Namba 6 Rice na Lewis-Skelly wanaweza kuicheza.

Kule mbele sasa ndipo waje wazee wa kazi, kama ulivyosema. Gyokeres na Sesko wote nawakubali, tuchukue mmoja wapo au wote. Tulete mbadala wa Odegaard pia. Wingers muhimu sana. Upande wa Saka naona tumuendee Kududs. Kushoto sijaona yupi atatufaa zaidi ya Gittens ila huyu naona Chelsea wameshamchukua. Tumehusishwa na Rodrygo ila sidhani kama anataka kuondoka Madrid na bei yake haitakuwa ndogo.
 
View attachment 3377464
Arsenal wake mezani na huyu mwamba, bado tunamuhitaji kwa misimu miwili
Huyu n mtu sana
Nashangaa kwanini hawajamalizana na huyu jamaa ili kuwekeza nguvu kwwnye maeneo ambayo yanaupungufu unaoonekana Wazi wazi ongezeko la zubi ilitakiwa na huyu jamaa abaki alf maeneo ya mbele yaboreshwe zaid ila akiondoka huyu inatakiwa tena kuingia sokon kutafuta kama huyu na hapo bajet inazid kupungua sijui hii timu ina laana.
 
1750585162655.png


OOOOO SANTI CAZOOOORLAAAAA

Jamaa ana miaka 40.

Kila mtu anaijua historia yake na sisi, ila tuangalie jamaa anavyomalizia historia yake kwenye boli la kulipwa.

Aliamua kurudi kwenye timu yake ya utotoni, Oviedo ambayo ina zaidi ya miaka 20 haijakuwepo La Liga na ilinusurika kufilisika kabisa ila kwa miujiza flani.

Jamaa alitaka kucheza bure kabisa na anatoa misaada na pesa zake kuliko anazopokea (kisheria, ilibidi apokee kile kiwango cha chini kabisa kinachoruhusiwa kisheria maana kisheria ni lazima alipwe) na kweli ameipambania sana timu.

Kifupi, jamaa alianzisha bonge la comeback kwenye play-off ya kuingia La Liga na Oviedo wameingia La Liga kwa msimu ujao. Bonge moja la stori kutoka kwa mchezaji niliyemkubali kuliko wote na mpaka sasa hakuna mchezaji ninayeweza kusema nampenda zaidi ya Santi.
 
Partey akiondoka solution ni kutafuta AM. Zubimendi na Rice watacheza Double pivot baadhi ya mechi, AM inabidi awe mzuri kuliko Ø, awe mbunifu na mwenye kupiga mashuti, kwa ufupi awe na uwezo wa kulitafuta goli, viungo tunao wengi wa kuziba nafasi ya Partey muhimu kocha awe tayari ku coach multi systems. Ujio wa Zubimendi unabadilisha majukumu ya Ø, Je ataweza kuibeba Arsenal kwenye sekta ya kutafuta magoli?
 
Tetesi za usajili wa Harrel Hatto nadhani ni kutengeneza mazingira ya kumpata Rodrygo goes ili kubalance team's dynamics, Sababu hakuna 1v1 LW aliyekamilika zaidi ya Nico Williams kwenye soko kwa sasa, ukimpata Rodygo ambaye anacheza inside forward kuna threat unapunguza left wide, Jarrel hatto anaziba hilo pengo lkn pia anaweza kuwa CB cover
 
Ø kinachombeba ni uwepo wa Nwaneri na Max dowman, the kids are talented but not ready, vinginevyo dirisha hili angetafutiwa mbadala
Mawazo ya kuchekesha, kutoka kwa shabiki wa timu ya kuchekesha.

Liverpool wana Rio Ngumoha, 16y lad with same potential kama Max na Nwaneri, lakini hao hapo wamevuta Wirtz.

United wana Chido Obi, wote tunajua few weeks nyuma walijiingiza kwenye dili la Gyokeres

Pia nikumbushe, Charlie Patino yupo wapi now?
 
Partey akiondoka solution ni kutafuta AM. Zubimendi na Rice watacheza Double pivot baadhi ya mechi, AM inabidi awe mzuri kuliko Ø, awe mbunifu na mwenye kupiga mashuti, kwa ufupi awe na uwezo wa kulitafuta goli, viungo tunao wengi wa kuziba nafasi ya Partey muhimu kocha awe tayari ku coach multi systems. Ujio wa Zubimendi unabadilisha majukumu ya Ø, Je ataweza kuibeba Arsenal kwenye sekta ya kutafuta magoli?
Kwenda na Ode as our AM next season, matokeo yake ni kama yale ya kwenda na Martinelli as LW last season.

LW Martinelli as a starter kwa 24/25, then 25/26 tunatafuta winga.

AM Ode as a starter 25/26, then 26/27 (baada ya kuboronga) tunatafuta tena AM

Matatizo ya timu ya mwaka huu, yanatafutiwa ufumbuzi mwakani
 
Nimeangalia YouTube tu ila nafikiri tutafute mabeki wawili - Jorrel Hato wa Ajax na Alexsandro wa Lille. Hato ni mfano wa Timber na Alexsandro ni mfano wa Gabriel na Kiwior na anatumia miguu yote vizuri. Ikiwa tuchukue mmoja tu basi naenda na Alexsandro. Tomiyasu anaumia sana, Tierney ameondoka na Zinchenko huenda akaondoka pia. Hapo tumalizane na upande wa ulinzi.

Mido - Zubi amekuja na Partey akiondoka sifikirii kuleta mtu mwingine katikati japo Jorginho ameondoka pia. Namba 6 Rice na Lewis-Skelly wanaweza kuicheza.

Kule mbele sasa ndipo waje wazee wa kazi, kama ulivyosema. Gyokeres na Sesko wote nawakubali, tuchukue mmoja wapo au wote. Tulete mbadala wa Odegaard pia. Wingers muhimu sana. Upande wa Saka naona tumuendee Kududs. Kushoto sijaona yupi atatufaa zaidi ya Gittens ila huyu naona Chelsea wameshamchukua. Tumehusishwa na Rodrygo ila sidhani kama anataka kuondoka Madrid na bei yake haitakuwa ndogo.
Well said,
Ukimya wa arsenal kwenye huu usajiri unaanza kutia mashaka
 
Well said,
Ukimya wa arsenal kwenye huu usajiri unaanza kutia mashaka
Usione tuko kimya kisa timu zingine zimesajili. Kumbuka tulimchukua Zubimendi kitambo sana pamoja na kuwa huenda hatutamtangaza mpaka July. Sesko tumefukuzia zaidi ya mwaka na sasa hivi dakika za mwishoni yeye na wawakilishi wake wameanza kuleta utoto mwingi.

Gyokeres anatusubiri, huenda tutaamua kuachana na Sesko tumchukue yeye. Changamoto ni umri wake maana tunakuwa na kazi ya kuscout striker mwingine wa kuchukua baada ya miaka kama miwili. Naona hii ndiyo moja ya sababu ya kumtaka Sesko badala ya Gyokeres.

Lengo letu kuu kwenye mido kwa wakati huu ni kumuongezea mkataba Partey ila tunashindwana kwenye malipo na muda wa mkataba.

Ni hisia tu, ila nadhani ndani ya wiki 2-3 utaona mambo mengi kutoka kwa Arsenal.
 
Back
Top Bottom