Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Hajatuacha mbali. Kesho tu hapa tunampita. Chelsea, Liverpool na Manchester City nao tutawakuta ndani ya miaka michache tu. Safari yetu inaelekea kileleni mwa hii orodha, na tutafika tu.
 
Hawa viazi mbatata ni kuendelea kuwakula tuuu
 
Phase 4 mkuu. Phase la makombe hilo. Tena kwa hasira, ili ipendeze, Phase 4 tunabeba makombe manne.
Timueni kwanza Tetea Kiwigi ndio muanze kufikiria habari za makombe.
Hauwezi kua na mid table coach halafu utegemee kubeba makombe makubwa, labda kama wenyewe mmeridhika na makombe ya Emirates na community shield.
Wenzenu Spurs washamtimua Ange Postecoglou, nyie endeleeni kufuga huyo Tetea huenda mmeridhika kuokota mayai.
 
Flano ifanyie lamination huu utopolo
Hao tayari wameshajikatia tamaa na hiyo Project uchwara ya Tetea Kiwigi, Mashabiki wa Arsenyau sasa hivi wamekua kama mbuni, wanaficha kichwa kwenye mchanga na kujidanganya kua adui hatawaona.
Kila msimu unaofata kwao ni phase 4 wakati Tetea Kiwigi tokea akabidhiwe timu ni mwaka wa 6 huu unaenda wa 7.
Tetea Kiwigi ni hana tofauti na yai viza, hata ulisifie vipi likipasuka lazima utaziba pua.
Tetea Kiwigi kila mwanzo wa msimu anasifiwa na kupewa majina yote mazuri, utawasikia wanamuita Masterclass, Tactician, Magician ila ligi ikikaribia kuisha utawaona wanaanza kuziba pua kutokana na harufu kali ya yai viza.
Walikuwepo kina Masingeli humu, yaani ulikua huwaambii kitu kuhusu Tetea Kiwigi, ila ilifikia wakati wenyewe wakanyanyua mikono juu na kulikimbia hili jukwaa, nasikia Masingeli huko alikokimbilia sasa hivi X (Twitter) ameanzisha Hashtag ya "Arteta Out"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…