Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Unawatazama strikers walioko sokoni,
Unajiuliza sababu kuu ya sisi kukosa kombe lolote la maana msimu huu jibu linakuja kwa haraka majeruhi,ila baada ya muda unasikia sauti ya utulivu kabisa ndani yako ikikwambia "mshambuliaji"

Kwanza unaleta ubishi kwa kuangalia namna tulivyoathiriwa na majeruhi ya defenders,strikers tulionao,wings na hata viungo na jinsi walivyotuathiri kwa kukaa nje muda mrefu na unahitimisha kwa kusema " majeruhi" ni chanzo.

Kisha ghafla katika kufikiri unakumbuka Bayern kachukua ubingwa ana harry cane,
Inter wako final UEFA na lautaro
Barcelona Wana kombe na lewandowsk.
Liverpool Wana Salah japo sio natural striker.unafikiri na unajiuliza mwenyewe hivi kweli tatizo ni majeruhi tu au ubutu wa safu ya ushambuliaji.

Unawazaaaa ila unaamua kupotezea kwa kusubiri mechi ya fainali ya UEFA.Next season is loading

Same owner
Same players
Same coach
Same stadium
Same fans
Same attitude
Same love for our team.

Anything will change? Muda utaongea
 
Hivi nyie jamaa mmeona nini kwa huyo sesko mpaka kufikia kumfungia macho dogo gykoers dah mngejua huyo ndio missing piece yenu mko kama walevi na management yenu haipo serious utaskia wanafukuzia, tena another midfielder dah
Hawa viazi hawajawahigi kuwa serious, huyo Sesko kazidiwa magoli na Lacazette, sa si bora wangebakigi tu na Lacazette.
Ushangae walimfukuza Emiry wakamchukua Kiwigi! Wakati Emiry ana IQ kubwa sana kumzidi huyo kiwigi.
 
Fact, lakini kwa muonekano wa kawaida ni mchezaji anayependwa na mashabiki ila kiuhalisia haipi timu balance ya ushambuliaji, sidhani kama Arsenal wanaweza kusajili mtu kwenye eneo hili sababu kuna ujio wa vijana wa Academy Nwaneri na Max dowman
 
Suala la majeruhi nadhani sio peke yenu mliathirika, tafuteni sababu nyingine ya kumtetea Arteta wenu.
Shukuruni kwa hat trick ya runner up, inatosha.
Suala la kumkosa Jesus na havertz kwa wakati mmoja unadhani ni jambo dogo? hapo sijazungumzia wachezaji wengine, timu kama Spurs walipata majeruhi ila wamemaliza nafasi ya ngapi, vipi kuhusu Man City na Man united? Isiwe kila wakati mnatanguliza mahaba ya ushabiki, kuna wakati unaipa akili nafasi ifanye kazi hata kidogo.
 
Mnahamisha magoli kila uchwao!
Wakati mnazidiwa pointi chache sana na city na sasa liverpool utetezi wenu ulikuwa maamuzi ya marefarii ndio imekuwa sababu. Leo hii baada ya kupigwa gap kubwa la pointi mmehamia kwenye suala la majeruhi.

Man utd iko kwenye declining mode huwezi kuilinganisha na Arsenal iliyokuwa na consistency ya karibu misimu 3 nyuma plus majeruhi ya key players, City ana kikosi kimechoka kiumri plus majeruhi ya key players lakini bado mmemzidi point 3!

Hoja ya singi inabaki kuwa hamkuwa wala hamko karibu kuchukua ubingwa wa EPL angalau ungesemea UCL ambayo mmefurukuta kufikia nusu fainali.
 
Kwa sasa hakuna kocha bora duniani kumzidi Tetea Kiwigi, ukibisha huna akili.
Tetea Kiwigi kavunja rekodi ya kua binaadamu pekee aliebeba community shields nyingi kuliko mtu yoyote kwenye historia ya soka hapa Ulimwenguni.
 
Kwa hiyo point yako ni ipi sasa? mimi nimekubali majeruhi sio tatizo
 
Uzuri hali halisi ya timu yako unaijua. Endelea kujipa furaha hapa kwetu
Najua unapitia kipindi gani ndugu yangu
 
Suala la majeruhi nadhani sio peke yenu mliathirika, tafuteni sababu nyingine ya kumtetea Arteta wenu.
Shukuruni kwa hat trick ya runner up, inatosha.
Kuna suala la dhulma za waamuzi pia. Points 12 tumepoteza kwa dhulma sa marefa wenye njama dhidi yetu msimu huu. Tunaweza kudai kuwa tungezipata hizi points 12 .... huenda tungekuwa mabingwa....😀
 
Brother mimi hili nililiona toka bado anaimbwa sana na watu wengi,kwenye level tuliyofika yeye anatukaba kwenye maeneo mengi sana,yeye anasababisha tunakuwa predictable sana huyu arteta akicheza anaweza akasababisha tusifike malengo yetu,anajuhudi sana lakin kwenye creativity,tight space kwenye mechi kubwa naona bado sana
 
lakin kingine pia hata martineli sio first eleven tena,brother sio finisher kabisaa
 
Wakipaki basi/low block wanasema ni haram football na wanajisifia ila timu nyingine wanaita underdogs.
Hili jukwaa ni sehemu sahihi kabisa ya kupunguzia stress sioni haja ya kwenda baa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…