Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Unajua wabongo wengi hatujui mpira, nilimsikia mchambuzi wa clouds fm anasema anashangaa Arsenal kuhusishwa na usajili wa Zubimendi sababu tayari eneo la kiungo mkabaji ,DM, kwamba Arsenal ina wachezaji wengi kama Partey, Jorginho na Declan Rice, kwa hiyo haoni umuhimu wa Zubimendi to Arsenal, alichoshindwa kuelewa ni kwamba

kwanza, Partey & Jorginho wapo kwenye kipindi cha mwisho wa mikataba yao

pili, Zubimendi is the latest and better version of Jorginho

Tatu, profiles za Zubimendi + Rice zinacompliment kutumika kwenye double pivot kitu ambacho kinachange the team's dynamics, the most creative player ambaye ni Saka anaweza kuingia interior na kutumika km no.10 na kutatua tatizo kubwa tulilonalo la creativity, yaani timu inakuwa haina tena RCM role bali RCM inakuwa converted to no.10 ambaye mostly anakuwa kwenye Zone 14 na system inachange from 433 to 4231.
 
Kwetu wabongo beki ni beki na striker ni striker, yaani beki azuie, striker afunge, mpira tunauona hivyo, lakini kumbe unaweza kusajili beki na akatatua matatizo ya attack, mfano, usajili wa calafiori lengo lilikuwa, ok, ku stabilize defense lkn kubwa zaidi ni kuaffect our attacking dynamics, ndiyo maana Mikel arteta anasema after Timber's ACL injury last season kulizuia plan yake ya kuifanya Arsenal kuwa unpredictable force, leo ukimtoa Skelly lewis na kumtumia Kieran Tierney usitegemee kuwa na similar dynamics, mfano mzuri ni namna tulivyokuwa wazuri na fluid going forward baada ya usajili wa zinchenko, leo tupo sawasawa kwenye kutengeneza nafasi lkn tupo hovyo kwenye finishing, naamini tunahitaji usajili wa striker sababu ya finishing, na ieleweke kwamba finishing ni suala la mtu binafsi sio jambo la system
 
Kuna shabiki wa Chelsea aliwahi kunambia kwamba Arsenal tuna a lots of system plyers, leo naamini, baada ya hili tatizo la finishing, sio kai havertz tu, ila a lots of our players wana Miss hizo big chances, Rice, Merino, odegard, havertz etc hii ni kukosa individual brilliance level ya Mo Salah, tukumbuke plan A ilikuwa ni Dusan Vlahovic, Mykhalo Mudryk
 
Nyie KENGE, kuna mchezaji wenu ana hatrick?
 

Attachments

  • Screenshot_20250117_005745_FotMob.jpg
    Screenshot_20250117_005745_FotMob.jpg
    99.3 KB · Views: 8
Kama umewahi kumuangalia Busquet na ukasema ni mid mzuri hakuna namna Partey utamuona hovyo.

Same profile. Muachia namba 6 anakuchezeshea timu vizuri tu.

Sasa huyo Zubimendi ni Busquet mwingine, so siyo mbaya kama tutampata akiwa kwenye prime.

Ila sisi hatutengenezi chances? Shida ni chances au shida ni kuscore? So who do we really need?
Yaani nyie ni vigeu geu, mkisikia mchezaji mnamtaka huwa mnampamba akiwakataa mnaanza kumponda na kumuwekea vinyongo.

Nakumbuka huyo huyo Zubambendi mlishampamba kipindi kile mnamtaka sijui ikawaje,cjui aliwakataa? aisee mlimponda balaa. Sahivi mmeanza tena kumpamba, nyie mashabiki wa Arsenal kuna sehemu nyaya zimechunika.
 
Nimejichanganya. Nilikuwa namfikiria Gyokeres na kuwa atataka kumfuata Amorim.

Sesko atatufaa? Angalau siyo Kai 😄😄
Huyu Sesko kwangu namchukulia kama Gabriel Jesus. Reliant wa skills na tech kuliko mwili na nguvu, so hatokua goal machine ambayo mashabiki tunatamani awe kwa kumuangalia Gyokeres ila atakua anascore na wakati mwingine kushiriki kuzipita defense
 
Yaani nyie ni vigeu geu, mkisikia mchezaji mnamtaka huwa mnampamba akiwakataa mnaanza kumponda na kumuwekea vinyongo.

Nakumbuka huyo huyo Zubambendi mlishampamba kipindi kile mnamtaka sijui ikawaje,cjui aliwakataa? aisee mlimponda balaa. Sahivi mmeanza tena kumpamba, nyie mashabiki wa Arsenal kuna sehemu nyaya zimechunika.
Usiwe unajumuisha.

Sema fulani ni kigeugeu. Mashabiki wa Arsenal hatujuani kila mtu ana tabia zake binafsi, kama umemuona kigeugeu, mpole, mwizi, mwema ni tabia ya huyo uliyemuona siyo ya Arsenal wote.

So, mtaje hapa ambaye aliwahi kumsifia Zubimendi halafu alivyoona amegoma kuja akaanza kusema vingine.
 
Ila nahisi uongo. Sesko akija atakua hachezi CL sasa wa nini?
Mkuu, nadhani hii mara ya tatu naona ukiandika kuhusiana na mchezaji kutoweza cheza timu mbili tofauti ndani ya msimu mmoja UCL.

Hili lilifanyiwa marekebisho 2019 kama sijasahau. So Sesko akitua now (which is very unlikely kwa Arsenal yetu) anakipiga freshi tuuu

Case study, Diaz Porto to Liverpool, Haaland Salzburg to Dortmund.
 
Mkuu, nadhani hii mara ya tatu naona ukiandika kuhusiana na mchezaji kutoweza cheza timu mbili tofauti ndani ya msimu mmoja UCL.

Hili lilifanyiwa marekebisho 2019 kama sijasahau. So Sesko akitua now (which is very unlikely kwa Arsenal yetu) anakipiga freshi tuuu

Case study, Diaz Porto to Liverpool, Haaland Salzburg to Dortmund.
Anhaa sikua aware na hii ishu ya marekebisho.

Kama hizi ripoti zikiwa confirmed na ni za ukweli tutakua tumepiga hatua kwenye kurekebisha swala la finishing
 
Huyu Sesko kwangu namchukulia kama Gabriel Jesus. Reliant wa skills na tech kuliko mwili na nguvu, so hatokua goal machine ambayo mashabiki tunatamani awe kwa kumuangalia Gyokeres ila atakua anascore na wakati mwingine kushiriki kuzipita defense
Ni mchapa kazi? Ukiwa kocha wewe itampanga mbele ya Jesus au mbele ya Kai?
 
Usiwe unajumuisha.

Sema fulani ni kigeugeu. Mashabiki wa Arsenal hatujuani kila mtu ana tabia zake binafsi, kama umemuona kigeugeu, mpole, mwizi, mwema ni tabia ya huyo uliyemuona siyo ya Arsenal wote.

So, mtaje hapa ambaye aliwahi kumsifia Zubimendi halafu alivyoona amegoma kuja akaanza kusema vingine.
Ni vile sio mtaalamu wa kuzitafuta old comments, hata huyo Gyokeres alishapondwa sana hapa nahis pia baada ya kukataa kuhama.
 
Back
Top Bottom