Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Tuna changamoto ya kwamba Trossard anakua kama Emile, akianza hakupi kitu kikubwa kuliko akitokea benchi.

Sijui kama mmeona hii ishu au ni mimi peke yangu
Ni kweli ni kama anachoka mapema. Aendelee kuingia sub wapinzani wakiwa washaanza kuchoka.

Ila Martinell wamkalishe wamweleze aachana na kuremba remba mpira.
 
Ni kweli ni kama anachoka mapema. Aendelee kuingia sub wapinzani wakiwa washaanza kuchoka.

Ila Martinell wamkalishe wamweleze aachana na kuremba remba mpira.
Kale katoto jana kameniudhi sana...huwa hakampigii simu hata Vinicious Jr akaelekeze kidogo namna ya kuchachafya mabeki...Kila siku mambo ni yaleyale tu....Martinelli akiwa very direct na asipokuwa anaupaka mafuta sana mpira basi atakuwa hatari sana ila akiendelea hivi...hakyanani atapewa thank you msimu ujao na Arteta na hatoamini...tunahitaji kuwadunda watu makofi ya macho chapchap kumaliza mechi mapema kenyewe kanaleta ubishoo...gemu ijayo ale mkeka kwanza Ili ajifunze
 
Bado gari halijawaka mkuu, after game Kama 4 hivi na Merino akishazoeana na wenzake utakuja kurekebisha
Kuanzia game na Spurs tutakuwa tumeanza kupata rhythm...sasahivi nachofurahi tunacheza kikubwa sana...hata tusipocheza vzuri bdo tutafanya Kila namna kupata matokeo na hcho ndo baba ubaya kipara ten hag anachokosea pale matofali ya kuchoma
 
Kuanzia game na Spurs tutakuwa tumeanza kupata rhythm...sasahivi nachofurahi tunacheza kikubwa sana...hata tusipocheza vzuri bdo tutafanya Kila namna kupata matokeo na hcho ndo baba ubaya kipara ten hag anachokosea pale matofali ya kuchoma
Baba ubaya anachokifanya ndio sisi tunapenda, so far ndio manager wangu Bora wa wiki hii

Bruno false 9

De light ndio sub ya magwaya. inachekesha Sana

Rashford anaanza starting 11 ganarcho yupo bench

Mount eti ni mchezaji wa man u, tena kapendekzwa na huyo huyo baba ubaya

Maino Ni mchezaji tegemezi wa man u. It's disgrace


Baba ubaya piga kazi, washabiki wa arsenal tupo nyuma yako
 
Namkumbuka sana masingeli aisee....alilisema wazi tangu siku ya kwanza baba ubaya sio kocha na anaomba Dua Kila siku apewe mkataba wa maisha Ili tuwe na furaha wapinzani...kwakwli nayaona haya kabisa....masingeli mtu wa maana kabisa🤠🤠
 
Flano
Siku ukimuona hamis77 humu jf, ujue jukwaa la nyumbu linakua mali yake
Hakuna nyumbu anaweza kwenda toe to toe na masingeli
 
Next game ni dhidi ya Brighton.

Wakati yupo De Zerbi timu yao ilikua constant threat ila ni vile walikuta tayari tuna rhythm nzuri ila safari hii wanatukuta bado tunajitafuta.

Binafsi nachukulia Arsenal tuna defense nzuri kwa msimu wa nne mfululizo, so hii ndiyo kete yetu ya kwanza kwa Brighton. Bado hatuna long shot merchant pia forwards zetu hazionyeshi kama zinawazia kaunta.

Kwangu naona dhidi ya Brighton ni sahihi ukiwa unaweza kutumia hivi viwili kama Plan A itafeli.
 
Mimi ninachojua Brighton atapigwa Kama alivyopigwa villa.
Tutamkamatia kwenye high pressing

Brighton wazuri Sana kwenye buildup na transactional football
Kama haupo vizuri kwenye pressing kwa Brighton Bora upaki bus kitu ambacho nyumbu walitakiwa kukifanya Jana
 
| HATUTAKI MAZOEA NA WATOTO. TUNALIPA ZILE MBILI KWANZA.

Arsenal wameibuka na ushindi wa mabao mawili kwa bila dhidi ya Aston Villa wakiwa ugenini dimba la Villa park. Trosaard na Thomas Partey wakipeleka ushindi Gunners huku Raya akiendeleza uhodari wake eneo la goal keeping.

FT | Aston Villa 0-2 Arsenal ( Trossard x Partey ).

Katika mechi ambayo Arteta ametumia hesabu kali sana kimbinu ni hii huku Unai Emery timu yake ikionekana kukosa baadhi ya vitu viwili ( Utimamu baadhi ya wachezaji na Subs za lazima).

1. Arteta anajua ubora wa Aston Villa bila mpira ni Kukabia eneo la katikati hadi chini sana wakiwa na uhodari mkubwa wa kufanya linkup bora sana wanapotapa mpira kwakuwa wana wachezaji wenye kasi.

2. LEON BAILEY, MORGAN ROGERS na WATKINS. Ili kuwatengenezea Big spaces kwenye flanks kuwapata Arsenal kwenye 1v1 baada ya kupata mpira unaadhibu ile rest defence ya Arsenal. Lakini leo Arteta alimgundua Unai how?

3. Usiwe na haraka ya kuwafanyia pressing wakati mashambulizi yanaanzia nyuma ( ili kusiwe na nafasi kubwa kati ya msitari wa ulinzi na ushambuliaji).

4. Thomas Partey kama atasogea. Rice atakuwa karibu na Saliba/Big Gabi. Ikitokea Turnsover tupo karibu na opponts kufanya Covering. Hapa walifanikiwa. Lakini how tunakuwa bora kwenye OFFENSIVE?

NOTE.

1. Nadhani Trossard amekuja kutoa somo la namna ya kufanya MAAMUZI SAHIHI UKIWA ENEO LA HATARI. Shida kubwa ya Arsenal ilikuwa kufanya decision wakifika final third.

2. Martin Odegaard, Kai Havertz na Martinelli walikuwa wanachelewa kufanya maamuzi pale opponents anapo-break defence.

3. Trossard mjanja mjanja sana akiwa eneo la hatari

4. DAVID RAYA ni really GOALKEEPING. Chagua wewe unapenda footworking yake au saves zake? Bila yeye mechi ingekua ngumu sana. Kashatoa SAVES YA MSIMU


5. Bukayo Saka anaibeba sana hii Gunners, Halafu mguu wa ZINCHENKO unahitajika sana kwenye Creativity in LCM? Kuna muda Martinelli anakosa chakufanya akikutana na msitu.

6. WATKINS kakosaje lile goli?


7. Mechi ya pili, Clean Sheet ya pili? Kuna kipa mwingine?

NB. Unai kapata dawa


Zingo

 
Nyie viazi wolvs mlishinda vigoli viwili kwa tabu, sisi wanaume wenu tumewasokomeza sita
 
Flano
Siku ukimuona hamis77 humu jf, ujue jukwaa la nyumbu linakua mali yake
Hakuna nyumbu anaweza kwenda toe to toe na masingeli
Mwamba afanye arudi tu kwa kweli, kama anaona noma kuja na ile Id yake ya Masingeli tuliyoizoea basi arudi hata na ile Id ya Aaron Arsenal
Jamaa linajua sana kuchangamsha jukwaa, likianza kutusimanga unaweza kuhisi ni mtoto wa Hadija kopa kakake Zuchu.
Tokea amepotea jukwaa la Arsenyau limekosa kabisa mvuto, mwamba alikua analifanya jukwaa la Arsenyo linakimbiza kuliko majukwaa yote ya sport hapa Jf.
 
mechi yenu dhidi ya Villa nilikua najiuliza kwa nini Jesus hayupo kabisa kwenye lines-Up, haonekani kwenye 11st wala Sub, kumbe hili tukio lilimsababishia michubuko na maumivu makali sana.
Wahuni sio watu, Get well soon Gabriel Fernando Jesus.
 
Nyie viazi wolvs mlishinda vigoli viwili kwa tabu, sisi wanaume wenu tumewasokomeza sita
Zoeaneni mapema kabla hatujakutana....habari za kuja kusema Fulani hakuwepo ndo maana tumewafunga hatutaki kuzisikia majirani🤠🤠🤠....jikazeni tukikutana mpunguze idadi ya magoli maana safari hii hata draw hampati
 
Japo dirisha la usajili halijaisha (
5 days remains),lakini binafsi ninasikitishwa sana na mwenendo wa usajili wa timu yetu.Katika dirisha ambalo nilijua tutamalizana na usajili mapema sana ni dirisha hili.

Na miongoni mwa nafasi ambazo mtu/watu walikuwa wawe washaletwa mapema ni winger na/au striker wa kuamua matokeo muda wowote ule.

Nico Williams na Osimnhem/Gyokeres muda huu walitakiwa wawe tayari ndani ya uzi mwekundu.

Kama alivyosema mdau mmoja juu huko, timu tunayo, ila na wengine timu wanazo pia. Je tupo kamili ku compete nao?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…