Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Wafuatano inabidi watupishe
1. Nketia
2. Cedric
3. Elneny
4. Nelson
5. Lokonga
6. Nuno tavares
7. Joginho au Partey


Wafuatao ukija pesa nzuri, watupishe
1. Tomiyasu
2. Jesus

Wafuatao wapewe final chance (6 months)
1. Rowe
2. Fabio Vieira

Usajiri
Tunahitajia namba: 9 na 6 machine za maana
White na Saka waletewe watu
Central defender mmoja




.
.

KILLING STARTING 11


.....Martinel. ..................9..........................Saka.......

.
.. ..............Rice. .............6 ..................Odegard
.
.
.........Timber.........Gabriel........Saliba............White
.
.
. .. ........... ..................Raya. ................... ...............

Sub;
Kai
Trossad
Zichenko
Rowe
Vieira
Tomiyasu
Jesus
 
Jumamosi ya bahati kwenu si mbali. Hebu tuone kama mtaingia ulaya.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] Guardiola hawezi kuridhika na kombe moja tu kwa msimu mzima, hio jumamosi tunaenda kuchezea kipigo cha mbwa koko, Arsenyau ombeni sana tufungwe ili tufunge midomo, ila tukibahatisha kumfunga City na kubeba kombe mtapata shida sana humu[emoji16][emoji16][emoji16]
 
Shida kwetu si midomo yenu. Sisi tunajitambua. Tumewazidi kila idara so midomo yenu kwetu ni kama kelele za mbu aliye nje ya chandarua. Atatukosesha usingizi kwa dakika chache ila usingizi ukikolea, hata afanyeje tunalala usingizi na damu hanyonyi.

Kumbahatisha Kipara ina maana kwenu kuliko sisi. Nyie ndio mnaohitahi kuingia Ulaya. Cha zaidi labda ushindi wenu utavyotusaidia sisi ni kumfanya Kipara apunguze confidence. Ajiulize 'mbona nimetoka kubeba treble jana halafu leo napata ligi tu tena kwa kupambana sana?' Na hiyo itatusaidia wengine kuongeza ari ya ushindi dhidi yake, kuzidi kumpandisha presha na hatimae tutamshinda au kumfukuza akimbie ligi kama mwenzake Klopp.

Ila kamwe usijidanganye eti nyie kubahatisha na kuwa na maneno mengi itatusumbua sisi hata kidogo. Kumbukeni sisi hatuna shida na nyie. Nyie ndiyo mnashida na sisi. Sisi tumeshawaona nyie siyo level zetu na hatuwezi kujihangaisha na nyie.
 
False hoper
 
Kuna watu ambao timu isipochukua ubingwa hawaoni kitu kingine cha maana tulichokifanya.

Wanashindwa kuangalia tulipotoka ni wapi ukilinganisha na hapa tulipo hivi sasa... mbaya zaidi hata mashabiki hata mashabiki wa Arsenal baadhi wako na hizi fikra kwamba baada ya kuukosa ubingwa basi hakuna kingine cha kujivunia.

Binafsi naona kama kusingekuwa na improvement yoyote kulinganisha na msimu uliopita basi tusingestahili hata kupigiwa makofi.

-Ukiangalia msimu huu points tulizokusanya(89) ni nyingi kulinganisha na tulizokusanya msimu uliopita(84).

-Mechi tulizoshinda(28) ni nyingi kulinganisha na tulizoshinda msimu uliopita(24)

-Magoli tuliofunga msimu huu(91) ni mengi kulinganisha na tuliofunga msimu uliopita(88), japo msimu jana tulikuwa na wafungaji wengi(19) kulinganisha na msimu huu(16).

-Magoli tulioruhusu msimu huu(29) ni machache sana kulinganisha na tulioruhusu msimu uliopita(43).... bila kusahau kwa mara ya kwanza tumemaliza msimu tukiwa na cleansheets 16, hii inaonesha ni jinsi gani defense yetu ilivyoimarika mara dufu.

-tukiacha na hizo records hapo juu, pia tukumbuke tumeshaondoa ule unyonge kwa wakubwa wenzetu, tumeshinda big matches zote hapo mwishoni..... sikumbuki mara ya mwisho ni lini tuliweza kushinda dhidi ya Chelsea, Tottenham, Manchester United na tena wakiwa wamefuatana fuatana ndani ya mwezi mmoja tena tukielekea kumaliza msimu kwenye nyakati ambazo ni za pressure.

-Vile vile pia tusisahau sisi ndio timu pekee tuliokuwa kiboko ya kipara msimu huu, kwenye mechi mbili zote ameambulia point moja tu something we had never done before, na pia sisi hawa hawa ndio tulimzuia Kipara asi achieve sextuple kwa pale uingereza baada ya kumtandika kwenye ngao ya jamii..... na iko wazi kuwa sasa hivi sisi ndio tunaomnyima usingizi kipara.

Kiukweli kuna massive improvements ambazo tumezifanya na zinatuweka mahala pazuri sana za kuchukua ubingwa msimu ujao... sasa kama kuna shabiki wa Arsenal ambaye anaona licha ya timu yetu kufanya hayo yote lakini bado ana nung'unika badala ya angalau ya kijivunia hapa tulipofika, basi nashauri mtu huyo atafute timu nyingine ya kushabikia ambayo anaamini itamuhakikishia mataji kila msimu.

We true gooners are so much proud of these little achievements we have made this seaso so far.
 
Hebu andika tena, unaonekana una machungu hata huelewi unataka kusema nini.
 
Ukawa umeenda jangwani kufunga na kusali Arsenal isichukue kombe.

Tofauti yetu na time zote za EPL, siyo Burnley pekee, ni hii hapa.

Hili ni kombe la nne kwa City mfululizo lakini hakuna anayezungumzia hicho kitu kama mafanikio makubwa badala yake timu inayoongelewa ni Arsenal.

Timu yako haiendi michuano yoyote ya Ulaya, hakuna anayeshangaa. Nyumbu atacheza FA na 115 fc lakini kila mmoja anajua nani atashinda hilo kombe.

Hiyo ndiyo tofauti
 
Mkuu ivi yule beki wetu wakushoto alie injury anarudi lini maana nasemaga angekuwepo na yeye basi arsenal ingekua ingekua bora mara 12

Ni beki flani tulimchukulia ajax
 
Trophies won from 2022-24

Man United: 1
Arsenal: 0

Cup finals reached from 2022-24

Man United: 3*
Arsenal: 0

😁
 
Mpira unatiwa siasa


The UK government has admitted that its embassy in Abu Dhabi have discussed the 115 charges levelled at Man City by the Premier League, but are refusing to disclose the correspondence because it could risk the UK's relationship with UAE.

(Source:
@PJBuckingham
)
 
Tunajua wana hatia.
Tunajua pia kuwa hawataadhibiwa.
Kilichobaki ni tutakaza na kuwapiga hivyo hivyo na ufisadi wao.
 
Hebu andika tena, unaonekana una machungu hata huelewi unataka kusema nini.
Soma ukiwa huna konyagi wala K-vant kichwani mwako utanielewa nimeandika nini...

Hao akina Nketiah wameiwezesha Arsenal kushika nafasi ya pili na wamekuwa title contender kwa mechi 38 zote, yaani mpaka mechi ya mwisho kimahesabu walikuwa bado wana nafasi ya kuchukua ubingwa.....haya sasa wewe wachezaji wa timu unayoishabikia wamewafikisheni wapi? Kama mmemaliza ligi Arsenal akiwa juu yenu, basi hiyo yako wachezaji wake ni viazi mbatata kama ulivyo wewe unatakiwa uwape heshima hao akina Nketiah
 
Manchester City sio Everton au Nottingham Forest, unapo deal na City hapo jua una deal na Falme nzima ya kiarabu na hicho sio kitu rahiso hata kidogo.... kila mtu anajua City wana hatia, lakini watafanywaje??? Na nani wa kuwachukulia hatua?

Sana sana hapo hili sakata litakopoishia ni City kufungiwa usajiri tu angalau kwa misimu miwili basi.... kuhusu kushushwa daraja au kunyang'anywa mataji hilo tusahau.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…