Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Anaitwa Kai Miguno...Kai michano...Kai miswaga🤠🤠...jana kashangilia kishenzi...Chelsea inaonekana walimtimua kabisa yle jamaa...wakaleta Kai wa kiafrika🤠🤠...mzee wa kubadili blichi kichwani...na wakimshindwa watupe sisi tumtumie yy na mwenzie Mudryk
Mi mwenyewe leo nimemuacha Kai huku mtandaoni ila jana alishanitibua wakati wa game. Alipofunga nilishangaa sana halafu ndiyo nikashangilia
ai
 
Tunapo zungumzia malezi ya pande mbili hua mnahisi kama vile tuna chuki tu binafsi dhidi yenu, ina nakuhakikishia katika majukwaa ya timu zote humu hili jukwaa lenu ndio linaongoza kwa utovu wa nidhamu.
Malezi, Malezi, Malezi, vijana wengi badala ya kulelewa na baba na mama wao wamelelewa na beki 3.
Arsenal hatuna huu uhuni kabisa mkuu, huyu atakuwa ni wenu au livakuku

Amini maneno yangu 😂
 
Mi mwenyewe leo nimemuacha Kai huku mtandaoni ila jana alishanitibua wakati wa game. Alipofunga nilishangaa sana halafu ndiyo nikashangilia
Mie kai alipofunga sikushangilia wala nini, kwanza ile game niliona kabisa wanakufa sikuwa na muamko na goli, pili kai alikuwa kaishanikera mpaka kunikera tena.

Kuna mpumbavu mmoja kai alipofunga akaniambia kaka umemuona kai huyo😂,
Nikamwambia chizi akiokoa mtoto kwenye moto haimaaninshi kapona, anaweza kwenda mbele huko akamdumbukiza kwenye kisima.😂

Kisha nikammaliza kwa kumwambia mtu si mbwa, kama ye ni bora kwa kufunga hizo mbili mbona ben cheupe katupia mbili na tena ni beki😂.

Akakaa kimya. 😂
 
Mie kai alipofunga sikushangilia wala nini, kwanza ile game niliona kabisa wanakufa sikuwa na muamko na goli, pili kai alikuwa kaishanikera mpaka kunikera tena.

Kuna mpumbavu mmoja kai alipofunga akaniambia kaka umemuona kai huyo😂,
Nikamwambia chizi akiokoa mtoto kwenye moto haimaaninshi kapona, anaweza kwenda mbele huko akamdumbukiza kwenye kisima.😂

Kisha nikammaliza kwa kumwambia mtu si mbwa, kama ye ni bora kwa kufunga hizo mbili mbona ben cheupe katupia mbili na tena ni beki😂.

Akakaa kimya. 😂
Kipigo tulichowapa Chelkenge jana kilikuwa ni adhabu ya kutuuzia yule kiazi. Tena tukaamua kumtumia kiazi huyo huyo kuwaadhibu.
 
Kama sio masihara, tungewakafua hata 8 wale kenge.
Dhambi ya kutuuzia kai na kuwatapeli man u kwa mlima mason, itawatafuna mnoo 🤣
Kai alipata chance ya kushoot afunge, eti anajaribu kumpa pasi Rice na kuna beki kati yao. Next move similar situation ila hakuna beki kati yake na Trossard ila kuna beki kati yake na kipa na amepata chance ya kutoa pass, akashoot na kukosa goli.

Mimi namuandama sana jamaa ingawa kuna mazuri pia anafanya. Kama goli la kwanza alihusika kwenye build-up alipopokea mali kwa Saka, akampa mali Partey, Partey kwa Rice na Rice kwa Trossard...
 
Nadhani bado kidooogo. Everton wana mechi 5 bado. He akiruhusu kwenye mechi moja kati ya hizo halafu zingine asiporuhusu na wakaishia wote na 14 clean sheets?
Ndio makombe yenu haya msimu huu

1) Raya cleansheet Cup
2) We defeated Liverpool Cup
3) Odegaard BiG IQ cup
4) We scored Many Goals Cup
Hapo Quadraple tayari.
 
Back
Top Bottom