Bado tupo sana humu, ni fedheha kujisifu kuifunga Chelsea hii ya Cappuccino, hawa jamaa ni wa kuruhumiwa tu kwa kweli.
Ndio maana binafsi hua namkubali sana 7 Hag, yule kocha ana utu na ubinaadamu mkubwa sana ndani mwake, baada ya kuona Cappuccino amekalia kuti kavu aliwaambia vijana wake mnusuruni huyu kocha wa Kihindi, sisi tusiwe sababu ya familia yake kufa njaa baada ya kibarua chake kuota nyasi, halafu siku ya kiama sisi ndio tukahukumia na kuonekana wadhambi mno kwa kushindwa kumsaidia walau kwa points 3 tu ili kuinusuru familia yake ipate kwenda chooni.