Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

game ya arsenal na bayern munich nasubiri kuona bookies odds zitavokuwa japo naona ni kama vile hakuna favourite kumzidi mwenzie hapo.
1000011238.jpg
 
Tunashukuru kwa taarifa mkuu...umeshashiba tambi unakuja kutufanyia Fujo sasa
[emoji23][emoji23][emoji23] Mkuu ni tambi na maharage mixer lile kombe kubwa la uji.
Ila kuweni makini ndugu zangu huyu Bayern akikufunga ni kama vile anakuachia na laana kabisa ya haya mashindano, ingawa kweli tembo yuko mtini ila hatutaki tuwakose kwenye hii michuano kwa miaka 8 tena mingine ijayo.
tapatalk_-1956244963_488x640.jpg
 
Tunatakiwa kulipa kisasi dhidi ya Barcelona siku ya fainali.

Naombea tukutane na Barcelona.

Uhuni walioufanya 2006, hatujausahau. Barcelona timu ya majizi sana.

Japo ili kufika hapo tutahitaji kupanda milima mirefu kwelikweli. Uzuri Arsenal hii inaweza kupambana na timu yoyote na ikapata matokeo.
 
[emoji23][emoji23][emoji23] Mkuu ni tambi na maharage mixer lile kombe kubwa la uji.
Ila kuweni makini ndugu zangu huyu Bayern akikufunga ni kama vile anakuachia na laana kabisa ya haya mashindano, ingawa kweli tembo yuko mtini ila hatutaki tuwakose kwenye hii michuano kwa miaka 8 tena mingine ijayo. View attachment 2935704
Sisi hatuna msalie mtume safari hii...tutawadunda kama Ngoma wale watu
 
Kati ya Madrid na City ya sasa ni nafuu kukutana na Madrid.

Bayern ina beki Eric Dier. Ina kocha Tuchel.

Timu nyingine ambayo ilikua inatutishia historia ilikua Porto. Ni miongoni mwa timu ambazo zimemaster kufanya mid na low block.

Kitakwimu ni rahisi kupata goli ukicheza na Madrid/ Bayern kuliko Porto. Walipotupiga 1 wote tukaona historia iko upande wetu.

Ikawa upande wetu ila kwa dakika 30 zaidi na Raya kuhusika kutuokoa.

Arsenal ni underdog kwa yeyote atakayekutana naye CL na siyo kwa ajili ya quality ya wachezaji ila ni kwaajili ya uzoefu wa kua humo CL.

Arteta aliwazia mwaka wa kwanza wa CL uwe ni kutembea kisha unaofuata kuchukua. Kutokana na jinsi muda ulivyoenda mashabiki tunaona tunastahili kombe, mwaka ujao be damned.
 
Njia imekaa vzr ,tukifika fainal inakuwa rahisi ,

Bayern anakuja Emirates,amefungiwa kuja na mashabiki,kwahiyo Emirates itajazwa na mashabiki 60,000 wote wa Arsenal


Bayern ana ego ya kupishana ,

Tukifika Fainal itakuwa kazi ngumu tumeifanya nusu ,
 
Tuchel: "We now face one of the best teams in Europe."

Neuer: "They're a very strong team with a very good spirit"

Müller: "Arsenal are a team who'll give us two thrilling games"

Eric Dier: "Arsenal have a young team who are performing very well."
20240316_065317.jpg
 
Punguzeni midomo tusijikute kwamba aya mashindano tume dominate wakati tumekaa nje ya game muda mrefu, Tumueshimu aliye tutangulia.
Mnaboa
Kwhyo Hawa wanaokuja hmu ndani kutupiga spana na kutuletea stats mara historia za Bayern tukicheza nao nao wapige kimya au...wacha watu waongee...wanaokandia wape nafasi...wanaopiga midomo kwmba tunapita nao waongee...ndo maana ya jukwaa huru...bila ya kukandiana ama kutamba hakutakuwa na maana ya haya majukwaa tena
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom