KWANINI ARTETA AMECHELEWA KUMTUMIA BEN WHITE KAMA INVERTED FB?
Mikel atakuwa anajuta Siku zote alikuwa wapi kumtumia Ben white kama Inverted FB upande wakulia,amemtumia hivo Zinny ,akamtumia Tierny akashindwa ,akamtumia Kiwior akashindwa
Lakin swali kwanini alikuwa hajafikiria kumtumia Ben white ambaye alikuwa Kiungo chini ya Biesla ?
Atakuwa anajuta kwanini alichelewa,kuna muda alimtumia Hadi Partey....
Uwezo wa Ben White kufanya kazi kama beki wa kulia anayeingia ndani kama Kiungo unampa Arteta chaguo zaidi kwenda mbele, huku pia ni kivutio kwa siku zijazo.
Mchezaji aliyesajiliwa majira ya kiangazi Jurrien Timber, ambaye amekuwa nje tangu Agosti kutokana na jeraha la goti, aliletwa kwa sababu anaweza kucheza kama beki wa pembeni. Lengo kuu ni kuifanya Arsenal isitabirike zaidi,maana timu nyingi zinajua Arsenal anamtumia Zincheko ku invert to midfield,hivo inakuwa rahis ku target huo upande ,mfano vs Liverpool walipomtumia Salah , lakini kitendo Cha kuwa na Ben white anayeweza ku invert kama Kiungo akitokea kulia , pia na Timber amayeweza kufanya hivo akitokea kulia na kushoto ,pia na Zincheko ambaye anafanya hiyo kazi akitokea kushoto ,kuna mpa Mikel Sasa machaguo mengi kutokana mpinzani amekujaje.
n timu zitashindwa kujua kama zitajenga mashambulizi kutoka kushoto au kulia.
Kumtumia White kwa namna hiyo dhidi ya West Ham pia kulimsaidia Kiwior. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Poland ni beki wa kati kwa asili na amekuwa na wakati mgumu alipoombwa acheze kama beki wa pembeni anayeingia kama Kiungo ,lakini uwepo wa Ben white ku invert to midfield,kunamfanya Kiwior abaki nyuma na amekuwa na kiwango kizuri .