Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Kuambiwa £60 million plus litakuwa jambo la kawaida...watu watachukulia kesi ya Caicedo....Chelkenge wameweka mfano mbaya sana pale England
 
Tuchel on Havertz:

"Dennis Bergkamp, Robin Van Persie, Barbetov kind of player. He can play in the half position because he makes good runs, feels free from the 9 and creates overloads to one side and he arrives in the centre."
Kai anajipata mdogo mdogo ila ni tusi kubwa kumuweka na Dennis berkgamp.

Tuchel afungiwe kufundisha soka maisha yake yooote.
 
Huyu jamaa siyo wa kumchukulia kiwepesi
 
Kai anajipata mdogo mdogo ila ni tusi kubwa kumuweka na Dennis berkgamp.

Tuchel afungiwe kufundisha soka maisha yake yooote.
😆😆😆 tumemsoma jamaa huku tunamcheka kwa dharau kichini chini. Yaani Denis "the iceman" bergkamp anatajwa sentensi moja na Kai "shot off-target" Havertz?
 
😆😆😆 tumemsoma jamaa huku tunamcheka kwa dharau kichini chini. Yaani Denis "the iceman" bergkamp anatajwa sentensi moja na Kai "shot off-target" Havertz?
Tuchel apigwe ban ya maisha asijihusishe na BOLI akawe mwalimubwa rede huko.
 
Tugeeni chance tushee CV.

Haya maisha yanachapa bakora nyingi sana
 
Onana

D Luiz

Palinha

Hizi taarifa inamaana kuna anaitajika mmja au kuna maingizo mawili January mmja na Summer kuna kiungo mwingine pia maana kila siku taarifa mpya Jana onana leo zimeibuka za D Luiz
 
Nadhan kazungumzia profile
Hakupaswa kumzungumzia na kumuweka daraja na berkgamp kwa namna yoyote.

Labda tu kwakuwa wote wamevaa jezi za arsenal. 🤣
Ni kweli kai kaanza kujipata ila huko kwa kina van persie ni utovu wa nidhamu
 
Onana

D Luiz

Palinha

Hizi taarifa inamaana kuna anaitajika mmja au kuna maingizo mawili January mmja na Summer kuna kiungo mwingine pia maana kila siku taarifa mpya Jana onana leo zimeibuka za D Luiz
Hapo tunataka tumuingize mkenge kubwa jinga moja, hasa Chelsea.

Walivyosikia tunamtaka Palhinha nao wamemueka kwenye list.. So far, priority ya Arsenal kwenye mid kwa january bado haijajulikana, lengo ni kuwapiga chenga copycats kama Chelsea.

Hizo habari zote za kina Douglas Luiz, Palhinha na Onana tunazohusishwa nazo usikute ni decoy akaja kuchukuliwa Yossouf Fofana au Cheikh Doucoure.

Unpredictability, remember?
 
Sema watu mna chuki sana na Kai .. halafu hazina Sababu
Kai achukiwe kwa kipi.. Humu sidhani kama tunaweza leta chuki binafsi kwa mtu ambae hatuna muingiliano na wengine hata huku mitaani kuishi kwa chuki hatuwezi.
Tunapoongea humu ni burudani tu kuchambua mpira, kuelezea kile unachokiona na kukijua kwenye ball.
Si lazima mfanane mawazo, ndio maana mwalimu huyu anaweza mtumia chama, yule akamkataa, huyu akamuona ode hafai, kisha huyu akamuona ode anamfaa. Soka liko hivyo.
Kila mtu ana kitu kimpendezacho kwa mchezaji.
 
Msimseme sana King Kai n Ozil mpya hapa arsenal
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…