mkorea
JF-Expert Member
- Aug 16, 2016
- 8,599
- 19,241
Daaah unanikumbusha mbali sanaVipaji vingi vinapotea mtaani, kwetu shule ndio ilikuwa kipaumbele, ila ningeweka umakini kwenye game huenda mingekuwa mbali sana.
Kuna kipindi nilikuwa sina mazoezi, shule yetubhaikuwa na mambo ya michezo, ilivyotokea yale mashindano ya shule za sekondari tukapangwa, mwalimj wetu alikuwa ni mkenya anaioenda saana arsenal, mara kibao kanifumania nimetoroka shule niko mtaani nacheki game, siku ya kwanza kunifuma ilikuwa msala lakini kwa kuwa mshabiki wa arsenal na class nilikuwa fresh haikuwa kesi kubwa sana.
Sasa yule ticha alitupambania kwa mkuu wa shule tukacheze ile game, aana wale masister(wahindi) walikuwa wameshatia ngumu, kweli tukapiga mazoezi siku 3, siku ya 4 game..
Mie nilichelewa kufika, nikakuta game ishaanza, nikaingia kipindi cha pili.
Aisee nilicheza kama namba 10, timu ilikuwa imekufa pale, aisee nilichowafanya ile timu pinzani kwa dk 15, 20 hivi kabla pumzi kisoda hazijakata ni balaa uwanja ulikuwa kila nikipatabmpira unatapika, uwanja ulikuwa wa wapinzani wetu lakini nilioata mashabiki kinooma, game inaisha watu wananisherehekea japo tulipigwa 4-2, mademu, washikaji wa shule ile wanakuja kunipa pongezi.
Kauli moja naikumbuka vizuri saan, alikuja beki wao, ambae si chini ya mara 3 nilimlambisha mchanga akaniambia "mwanangu we ni fundi saana, inaonekana huna mazoezi ila unaujua saana mpira, ungezaliwa ulaya ungecheza timu kubwa bila shaka"
Nikaondoka nimepata hela za wanakijiji.
Aisee hili tukio sintosahau, ika ndio hivyo tena, sasa hivi miguu yetu tunagombania daladala za mbagala.
Naandika, nafuta. Naandika tena nafuta. Nina vingi Sana vya kuelezea kuhusu mpira
Tukio langu ambalo sitalisahau. Ilikua tanga muheza nilienda likizo kwa bro kipindi hiko nipo form six
Sasa mtaani pale kulikua na timu alafu kulikua na mashindano ya kombe limedhaminiwa na mbunge
Nikawa kwenye mazoezi naenda kupiga nao tiz, siku kwenye mechi naenda na mm kuangalia (pale pale muheza Mjini) uwanja upo karibu na hospital
Siku ambayo chama langu lipo uwanjani, Kama kawaida tukawasili uwanjani (hapo Mimi Kama mbeba maji ya wachezaji)
Mpira ulikua mkali Sana siku ile(tanga Wana vipaji Sana
Dakika ya 70 wachezaji wetu wawil waliumia namba nane na winger, sub moja ya winger ikapatikana
Ila huyu kiungo wachezaji walikua hawaiwez ile namba sijui ata sielewi
Mara kocha akaniita oya MKOREA vaa jezi kwasababu hauna tiz, kacheze namba 10. Namba kumi aje nane
chamsingi saidi kukaba tu.
Kumbuka Hadi hapo timu tulikua tunacheza nao ya kutokea amani/amana tupo moja moja
Nikaingia, kabumbu likaanza. kupiga One two one two Sana tu
Sasa damu ikachemka nasambaza upendo tu, zikitokea faulo au Kona huwa nakaa area ambazo mpira uki-bounce zile dead balls zinanikuta
Sasa Kuna Kona ilikua tunapiga dakika za lala salama, Mimi nikaka nje ya box. Ule mpira kipa aliutema huku yeye mwenyewe akaangua ukanikuta nipo on move
Ilisikika sauti moja tu 'misssssss' nilikandamiza shuti kimoja Cha mbuzi na kipa alikua ameanguka ule mpira ulipita kama upepo
Ubao unasoma 2-1
Mpira umeisha kocha ananiuliza ndio wewe au? Mbona haukusema mkorea
.
.
Kwenye mpira huwa nacheza namba nane, nikipatiwa namba sita mzuri kwenye kukaba na winger zinazotembea unaweza ukasema pirlo ana mdogo wake huku bongo
Pia napenda Sana kupiga, zile za Steve Gerald
Sehemu kubwa ya mpira nimecheza kishule shule zaidi, hizi zamchangani sijui ndondo nilikua zisikubali kabisa
Na ata nilivyokua mdogo, nyumbani wakisikia nimecheza mpira tena maeneo ya mbali ni msala, Yani nilizaliwa ili nisome kwaio nachangiwa na watu wawili mke na mume wake kwenye kupigwa
Kuna siku nilishuhudia pale kajiungeni Kama unaenda chanika mtu anavunjika mguu Kama kuni hivi kwa rafu ya makusudi kabisa. I was so sad, kama nimefanya Mimi hivi
Umiseta nilifika Hadi kibaha. Ila Bongo nyoso sana wazee kmmk. Tulioandikwa majina Tukaambiwa tutaitwa/kupigiwa simu. Hadi Sasa nasubilia huko kuitwa