𝐌𝐀𝐑𝐓𝐈𝐍𝐄𝐋𝐋, 𝐀𝐋𝐈𝐕𝐘𝐎𝐊𝐀𝐓𝐀𝐋𝐈𝐖𝐀 𝐎𝐋𝐃 𝐓𝐑𝐀𝐅𝐅𝐎𝐑𝐃 •
Kama walivyo mastaa wengi kutoka Amerika ya kusini ikiwemo, Roberto Firmino, Antony, Gabriel Jesus wanatokea katika familia maskini ambazo hazikuwa na uwezo hata wa kuwapeleka shule.
Haikushangaza upande wa Gabariel Martinell alikuwa miongoni mwao, amezaliwa kijiji cha Guarulhos huko São Paulo ambacho kilikuwa kinasifika kuwa na wakazi wasiojiweza kimaisha, mzee wake Joåo Martinelli aliendelea kupambana ili Gabriel asome akiamini ndiyo sehemu pekee itakayompa maisha na kuiokoa familia yake. Lakini ilikuwa tofauti.
Maisha ya Martinelli yalianzia katika Academy ya Corinthians, lakini yeye alipendelea zaidi kucheza mpira kuliko kusoma, wakati anaendelea na masomo yake, mitaa ya Guarulhos iliitazama miguu ya Martinelli kama kivutio kikubwa kwenye jioni za mpira wakiamini anakipaji kikubwa.
Siku moja kocha wa Timu ya Academy anayosomea alimualika kufanya majaribio kwaajili ya kuona kitu kipaji chake, Martinelli alionyesha kipaji chake kama hatacheza tena na kupewa nafasi kwenye klabu ya Corinthians.
Maisha yake ndani ya Corinthians yalikuwa bora sana baada ya kufunga jumla ya mabao 202, aliweza kuwavutia ITUANO FC ambao walikuwa wakishika nafasi ya nne kwenye Ligi ya Brasil. Kwanini Manchester United?
Baada ya kusainiwa na ITUANO FC (2015) aliendeleza moto wake zaidi ya kuzivutia klabu kubwa kama Fc Barcelona, Real Madrid na Manchester United kumualika kufanya majaribio.
Wakati anafanga majaribio na Man United mara nne katika awamu tofauti akiwa na matumaini ya kusajiliwa, ilikuuwa tofauti baada ya kuambiwa hana nafasi ndani ya Old Traford.
"Kiukweli nilifanya majaribio mara nne Man Utd nikiwa na miaka 13, 14, 15 na 16. Nikiwa kwenye mazoezi ya klabu hiyo nilikutana na wachezaji wa Timu kubwa kama, Zlatan, Paul Pogba, Wayne Rooney na Evra.
Lilikuwa tukio ambalo sikufikiria kama nitakutana nalo kwenye maisha yangu ya soka, niliweza pia kucheza na wachezaji kama Mason Greenwood".
Wakati anaondoka uwanja wa Carington, Martinelli alikutana na PAUL POGBA na kumuuliza, vipi kuhusu majaribio yako na utachezea klabu gani hapo baadae?. Martinelli alimuelezea kwa unyonge kukataliwa kwake ndani ya Man United baadae alimruhusu wapige picha pamoja.
Baadae alitua LA MASIA pale FC Barcelona kwaajili ya mualiko wa majaribio lakini hakufanikiwa baadae alirejea ITUANO huko kwao Brasil. Baadae wakala wake alimuuliza, vipi kuhusu Arsenal?..
Majibu ya Martinelli yalikuwa rahisi sana baada ya kumwambia hakuna jibu lingine ni wakati wa kuelekea London, wakati huo Jopo la mascout wa Arsenal walikuwa wanafuatilia kiwango cha Martinelli.
Mwaka 2019 Arsenal walimsajili Martinelli kama U21 ambaye atakuja kufanyiwa majaribio ya kupandishwa timu ya wakubwa.
Note:
Martinelli alipelekwa academy ya Arsenal Hale End akakutana na kina Saka,Smith Rowe,, alicheza michezo kadhaa ya U21 Kama academy wa Arsenal , hivo Martinelli huwa anahesabika pia katokea Academy ya Arsenal
TUENDELEE SASA
Lakini wakati huo kulikuwa na vigezo kwa vilabu vya England kumsajili mchezaji kutoka Amerika ya Kusini ambavyo Martinelli alikuwa navyo kutokana na kuwa na Uraia wa Italia akiwa na paspoti kutokana na mzee wake kuwa ni Muitaliano.
Hii ilimsaidia kusafilri na timu kwenda Pre Season sehemu ambayo alienda kufanya makubwa, baadae alipandishwa Timu ya wakubwa akipewa nafasi ya kuonyesha alichonacho.
Baada ya kusaini mkataba na Arsenal kutokana na umaskini wa Familia yake, aliichukua Familia yake na kuja kuishi nayo London, Baba yake alikuwa na hofu kama wangeweza kuishi London kutokana na kiwango cha mwanae.
Baada ya Martinelli kuingia kwenye kikosi cha kwanza zilikuwa ni furaha kwa familia yake huku akiifungia klabu yake mabao muhimu kwenye nyakati tofauti. Hadi leo Gabi ameingia kwenye kikosi cha kwanza na anaitumikia Brasil kwenye National Level.
Good luck Gabi.
Zingo sports