Arsenal (The Gunners) | Special Thread


Jana limepigwa pira la kiume haswa
yaani unaona kabisa tupo pale kushindana si kuzurura .

Arsenal 2004 na wenzake walikuwa wanabana mbupu tu na kuwanga kwa sana ila kimya kimya mioyoni mwao wana enjoy soka . Group zilipotoka tu wauza matikiti wakajitangazia point 18 group lao then sisi tutaburuza mkia ila now tupo top of group , hata ukituweka kwenye group lao bado tutakuwa top.
 

baada ya match kuanza kuchezwa mnaona sasa zile false hope tuziondoe tusubiri match za mwisho.

Mwanzoni ilikua points 15-18 ila sasa zimepungua ni point 12-15 yaani zitapungua mpaka mnatupwa europa huko.
 
Hili kundi litamuwa gumu sana.
 
Man Utd tunaweza kupindua meza halafu kima zote humu zikabaki kinywa wazi. Jumapili mkigongwa na Mancity jukwaa litajaa matusi mengi sana hili.
Asenyo ni kadudu flani hivi kadogo kama sisimizi ila mashabiki wake wanajitutumua sana kukafananisha na tembo.
 
Hili kundi litamuwa gumu sana.
Shida sio ugumu wa kundi, shida kubwa ni mentality ya timu inaingia kwenye mashindano kwa malengo gani?
Timu kama Arsenyo unaona kabisa mentality yao ni kufanya pressing na over loading huku malengo yao wawe wanaongoza kwenye ball possession.
Halafu timu kama Newcastle United unaona kabisa wao malengo yao ni kupata 3points muhimu haijalishi takwimu yao ndogo ya possession.
Kwa takwimu hizi hapa za Newcastle atakuja masingeli kuwapondea kwa kushindwa kuoverload kiungo na kupata ushindi wa papatu papatu
 

Attachments

  • 1696503670222.jpg
    21.9 KB · Views: 2
Usiwajaze upepo wenzako....kama wao walivyoshinda jana kuna viwanja bdo wanaenda vya ugenini...jana ile mikelele ya mashabiki wa nyukesto iliwachanganya kabisa psg wakawa wanapoteza mpira tu....kikubwa wajipange gemu za nyumbani zte washinde kwa vyvyte vile....vngnevyo yale maigizo ya jana hayatakuwa na maana yyte
 
Man U ndo kubwa jinga la kwanza kwa mwaka huu kutoka uefa mapema....Man City wale tutawavuruga vzuri tu j2..sisi hatutapishana nao maana hatuwawezi wale wanaficha sana mpira ila tutawafunga na kuwa wa 2 tena maana Tottenham ataongoza ligi
 
Nimeona mahali:

Team ya marefa waliohusika game ya Liverpool na Spurs , pamoja na VAR, hawatapangiwa game kwa gameweek ijayo. Pia, ile team nzima au ile VAR team haitahusika kwenye games zozote za Livepool msimu huu.
Je hii inamaanisha nini?
Kama walishaamua na dunia imeamua ni human error, naweza kidogo kuelewa kutowapangia game inayofuata, labda ni kama fine ya kukosa ujira wa mechi moja. Ila sielewi kwa nini wasihusike na game za liverpool. Ina maana wanawashutumu kwa kuwa na ajenda dhidi ya Liverpool? Kama ni hivyo kwa nini wasifukuzwe kazi tu moja kwa moja? Na je kama wanawaona wako 'incompetent', kwa nini waachiwe waharibu mambo kwa timu zingine?

Nafikiri PGMOL walipaswa tu kurekebisha masuala kadhaa ili kuhakikisha maakosa anayofanya yanakoma, kama walivyosema, kisha maisha yaendelee kama kawaida.
 

Upepo mnajazana humu nyinyi wauza matikiti. Viwanja vya ugenini vipi hivyo tumeenda san siro tukatoka na point sasa sembuse huko kwa Dortmund na PSG bomba litashikiliwa vilivyo then wakija st james wanaingia kwenye mfumo wanakula vyuma.

Man city kafa then kafuata PSG nae kafa
pale ndo st james na wewe utakuja utakufa ni suala la muda.

Hapo bado barnes, willock, wilson, botman na joelinton majeruhi na wala hakuna anayelalamika ball linatembea . J2 visingizio vitakuwa vingi sana humu.
 
Narudia tena....usijae upepo wale Ac Milan ndo wenzenu mtakaomaliza nao nafasi ya 3 na 4...kikubwa mshinde nyumbani....vngnevyo utakuja kurudi na kauli hapa kwmba ndo mwaka wa kwanza huu kushiriki...mara tumejifunza wapi tumekosea na tutarudi tukiwa na nguvu zaidi....wakati inajulikana mkitoka mwaka huu ni mpk miaka 20 ijayo ndo mtapata kanafasi tena ndugu zetu
 
Na kama ingekuwa hivi...mwaka jana sisi marefa wametuhujumu sana basi wangetakiwa wasichezeshe mechi zetu tena na kufungiwa juu...mechi na Manunu walikataa goli pale Trafford wakaishia kuomba radhi...mechi na Southampton pale St Mary's stadium tulinyimwa penalt ya wazi Jesus kachezewa faulo na beki alivyolalamika mwamuzi akamwambia ungedondoka mpk chini ndo ningekufikiria...bdo mechi na Brentford pale Emirates walitufunga goli limetokana na Offside kabisa wakaishia kuomba radhi tu....hzi mechi zte tulidondosha Point ambazo pengine maamuzi yangekuwa vngne labda sasahv tusingekuwa tunapewa shombo na kina Labyrinth 84 hapa maana tungekuwa mabingwa
 
Kabisa. Kila timu imedhulumiwa na marefa at some point. Tena timu ndogo ni kwamba tu zinakosa sauti kama timu kubwa kama Liverpool ila kwao hali ni mbaya zaidi, haswa wanapocheza na timu kubwa. Sisi tunaweza kusema tumedhulumiwa tukakosa ubingwa, ila tukamaliza nafasi ya pili na financial impact yake siyo kubwa kihivyo. Labda pride na confidence vinaathirika ila zingatia makosa/dhulma hii itokee kwa timu inayojikuta imeshuka daraja kama ilivyotokea kwa Bournemouth 19/20 season. Makosa yasingetendeka msimu huo, Bournemouth angebaki EPL na Aston Villa ndiye angeshuka. Financial impact hiyo ni kubwa mno kwa Bournemouth kuliko difference ya nafasi ya kwanza na ya pili.
 
True
 
TRANSFER NEWS: Reported by @alex_crook...Wolves winger Pedro Neto is back on the radar of Arsenal

January move is possible as #AFC seek for further depth on the wings. Interest only at this stage for the Portugese.

#Transfers
 
Arsenal tumepoteza points kisa maamuzi ya marefa mwaka jana na msamaha tukaombwa kwenye scenario zaidi ya moja.

Maamuzi hayakua hivi
 
Southgate kamuita Saka kwa mechi za international break
 
“He’s still being assessed, they [Arsenal] have got a big game this weekend and then there’s another 7 days before we play Australia then 10 days before we play Italy.”

- Gareth Southgate on Bukayo Saka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…