
Mwandishi wa habari

: kwanini umeamua kumwanzisha David Raya dhidi ya Everton:

Mikel : "Mawazo sawa na ambayo Fabio alicheza au ambayo Eddie [Nketiah] amecheza mbele ya Gabriel Jesus. Sijawa na swali hata moja kuhusu kwa nini Gabriel hajaanza na ameshinda mataji zaidi.... [hawaulizi kwanini]

"Ni jambo ambalo kihistoria linafanyika hivi lakini siwezi kuwa na wachezaji wawili katika nafasi hii na nisiwachezeshe.

"David ana sifa nzuri sana kama Aaron [Ramsdale] alizonazo na Karl [Hein], lazima tuzitumie.

"Mimi ni meneja mchanga sana, nina miaka mitatu na nusu tu kwenye kazi na nina majuto machache. Ilikuwa mara mbili, kwamba baada ya dakika 60 na dakika 85 katika michezo miwili katika kipindi hiki ningeweza kubadilisha kipa wakati huo, na sikufanya hivyo.

"Sikuwa na ujasiri wa kufanya hivyo, lakini nina uwezo wa kufanya mabadiliko ya winga au mshambuliaji na kumweka beki wa kati nyuma kutengeneza mabeki watano nyuma na kulinda matokeo . katika michezo hiyo sikuwa na furaha.

"Ikiwa una sifa zote katika kipa mwingine kufanya kitu, au ikiwa kitu kinatokea na unataka kubadilisha kasi ya mchezo basi fanya hivyo.

"Ni majuto niliyo nayo na sasa hisia zangu ni kumfanya kila mtu ashiriki katika timu anayopaswa kucheza, bila kujali ushindani - huu ni ujumbe wangu."
[@arsenal]