Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Inavutia kutoka kwa Arteta.

Anasema majuto yake makubwa kama meneja ni kutokuwa na ujasiri wa kubadilisha kipa wakati wa mechi mbili hivi karibuni ili kubadilisha kasi ya michezo
 
“Ninachotaka ni wachezaji wanaostahili kucheza, wancheze.

Fabio [Vieira] alistahili kucheza - Amekuwa akibisha mlangoni kwa wiki chache. Unaweza kusema alikuwa tayari. Alichangia na alikuwa na vitendo vikubwa."

- Mikel Arteta kuhusu Fabio Vieira.
 
Sijacheki game mniambie nketiah alifanya kipi cha maana, maana sikupenda ye kuanza na je alivyoingia jesus alifanya bora zaidi ya nketiah? Nimeona kai ana rate ya 4.0 leo kacheza vizuri? Fabio huyu mara nyingi akianza hawi poa kama akiingia,je ilikuwa hivyo? Wengine sina mashaka nao.
 
Flano na Allypipi...kadi za uanachama bdo zipo nyingi sana tunagawa bure....karibuni ndugu zetu tuje tuburudike na bolu la kisasa....tikitaka flani...yaani unacheki unaona kabisa mpira unapelekwa wapi....siyo Yale mambo ya Bruno akiupata anamcheki Rashidi Makame ypo wapi anabutua huko mbele kwa mbele
Kwa hiihii Arsenyo inayobakiza mechi 8 kumaliza ligi ikiwa inaongoza kwa points 8, halafu inabaki mechi 1 ligi kuisha inakua ipo nyuma kwa points 8?
Hapana aiseeee mara 100 nishangilie Fulham walau yenyewe inamiliki kombe la Ulaya.
Arsenyau mkinionesha kombe lenu linalofanana walau na hili mimi nitawaonesha Maguire anavyokabidhiwa tuzo ya Ballon d'Or.
TELEMMGLPICT000338571077_16861744698580_trans_NvBQzQNjv4BqpVlberWd9EgFPZtcLiMQf0Rf_Wk3V23H2268...jpg
 
Sijacheki game mniambie nketiah alifanya kipi cha maana, maana sikupenda ye kuanza na je alivyoingia jesus alifanya bora zaidi ya nketiah? Nimeona kai ana rate ya 4.0 leo kacheza vizuri? Fabio huyu mara nyingi akianza hawi poa kama akiingia,je ilikuwa hivyo? Wengine sina mashaka nao.
Nketiah alikua involved na game mwanzoni baadaye akapotea. Amekosa nafasi kwa kutokua mtulivu.

Jesus alikosa nafasi za kumfanya awe hatari.

Mpaka muda anaingia mid yetu ilikua haifanyi sawa na timu kama ilisharidhika na goli moja. Huo muda ndiyo ilibidi Fabio aingie.

Kai hakua na impact positive. Bado hana confidence, anagongana na wenzake anatoa pasi za kusingizia.

Fabio strong feature yake ni defence splitting passes na amejitahidi mno kufanya hivyo.

Tafafhali kumbuka Eveton kaja huku anacheza 4 5 1 so alidhamiria kupaki basi
 
Chini ya hii niliandika Arsenal ingepata tabu kumuacha Martinelli kwa ajili ya Mudryk.

Kuna member akasema Mudryk kawekewa kipengele akipata Ballon D'Or kuna add ons na roho inamuuma hajaja Arsenal nikamjibu hata Martial ana kipengele hicho hicho.

Leo namuangalia Mudryk hadi muda anatoka naona ni kweli Arsenal tusingepata shida kujua tumuweke benchi our best shooter ama la. Beki akimfanyia take on Martinelli utamuona kijana yupo nyuma anakimbiza mpira, ila Mudryk pace yake haitumii kumsaidia kulinda
Hhaha mim pia nmetumia muda kumuangalia,first tch yake tu ni ile ile kila akipata mpira na mabeki washamjua saivi.
 
Sijacheki game mniambie nketiah alifanya kipi cha maana, maana sikupenda ye kuanza na je alivyoingia jesus alifanya bora zaidi ya nketiah? Nimeona kai ana rate ya 4.0 leo kacheza vizuri? Fabio huyu mara nyingi akianza hawi poa kama akiingia,je ilikuwa hivyo? Wengine sina mashaka nao.
Bado nketiah Hana level za Jesus , Ni rotation tu iliamua aanze ,

Kai katokea sub
 
Presenter: "No new number 1?"

Mikel Arteta: What number is Fabio Vieira? You say number 1, Fabio what number is it?

Presenter: We are talking about goalkeepers.

Arteta: Yes, but we play with 11 players in football. They are all the same. 11 players."
 
Mikel Arteta:

"Mimi ni meneja mchanga sana, nimekuwa na miaka 3 na nusu tu katika kazi na nina majuto machache.

Ilikuwa mara kwa mara, kwamba baada ya dakika 60 na dakika 85 katika michezo miwili katika kipindi hiki ningeweza kubadilisha kipa wakati huo, na sikufanya hivyo."

"Sikuwa na ujasiri wa kufanya hivyo, lakini nina uwezo wa kufanya mabadiliko ya winga au mshambuliaji na kumweka beki wa kati nyuma kutengeneza mabeki watano nyuma na kulinda matokeo hayo. Tulitoka sare kwenye michezo hiyo na sikuwa na furaha."


[Arsenal]
 
Hongereni kwa ushindi wana Gunners.
Mechi ijayo na Spurs ni ngumu sana, ukizingatia ni derby.. lakini vile vile jamaa siku hizi wanaweka mali chini.

Ila advantage tutakayokuwa nayo ni ya uwanja wa nyumbani, mana mashabiki wamerudi na nguvu kubwa sana.. hata akija City, anapigiwa kelele mpaka aseme po!
 
Mwandishi wa habari: kwanini umeamua kumwanzisha David Raya dhidi ya Everton:


Mikel : "Mawazo sawa na ambayo Fabio alicheza au ambayo Eddie [Nketiah] amecheza mbele ya Gabriel Jesus. Sijawa na swali hata moja kuhusu kwa nini Gabriel hajaanza na ameshinda mataji zaidi.... [hawaulizi kwanini]

"Ni jambo ambalo kihistoria linafanyika hivi lakini siwezi kuwa na wachezaji wawili katika nafasi hii na nisiwachezeshe.

"David ana sifa nzuri sana kama Aaron [Ramsdale] alizonazo na Karl [Hein], lazima tuzitumie.


"Mimi ni meneja mchanga sana, nina miaka mitatu na nusu tu kwenye kazi na nina majuto machache. Ilikuwa mara mbili, kwamba baada ya dakika 60 na dakika 85 katika michezo miwili katika kipindi hiki ningeweza kubadilisha kipa wakati huo, na sikufanya hivyo.

"Sikuwa na ujasiri wa kufanya hivyo, lakini nina uwezo wa kufanya mabadiliko ya winga au mshambuliaji na kumweka beki wa kati nyuma kutengeneza mabeki watano nyuma na kulinda matokeo . katika michezo hiyo sikuwa na furaha.

"Ikiwa una sifa zote katika kipa mwingine kufanya kitu, au ikiwa kitu kinatokea na unataka kubadilisha kasi ya mchezo basi fanya hivyo.

"Ni majuto niliyo nayo na sasa hisia zangu ni kumfanya kila mtu ashiriki katika timu anayopaswa kucheza, bila kujali ushindani - huu ni ujumbe wangu."

[@arsenal]
 
Havertz dakika zake ndio kama hizo. Dk 15 mpaka 20 zinatosha kuanza kumjengea confidence taratibu mana kabla ya hapo wenzie wakina Fabio Vieira walikua wakipewa time kiduchu hivyo hivyo.

Lakini kama Arteta ana akili yake nyengine ya kumpanga UEFA basi nitashangaa sana kwa sababu afadhali leo timu imerudi kwenye ile identity na namna ya uchezaji tuliyoizoea.
 
Naomba na UEFA aanze na kikosi hiki hiki, afanye mabadiliko sehemu moja tu, aanze Jesus badala ya Nketiah japo najua Ramsdale lazima ataanza golini.
 
Back
Top Bottom