Mwaka 2021 Tuchel akiwa anamlinda Werner akasema Werner aache kufikiria magoli akafananisha na kumuomba date mwanamke, akasema huwezi kumlazimisha inabidi usubiri. Tulia magoli yatakuja.
Jana Arteta katumia mfano wenye muktadha huo huo kwa Kai.
Sasa Tuchel siku anatoa huo mfano ilikua Werner kacheza games 31 na kascore magoli mawili. Nilikua naona Tuchel hamtumii Timo inavyotakiwa, same janga litaanguka kwa Nkunku, na ninafikiri Kai pia hatumiwi inavyotakiwa.
Pasi zake ni fupi fupi na ni back pass au sideway passes na hii ni kwakua Kai hana vision kwenye passing, anamove muda mwingi wa mchezo, katika kupress anamove kama vile hataki au amechoka.
Henry aliwahi kumlalamikia Wenger juu ya Bergkamp nafikiri kisha Wenger akamuambia Henry "Usilalamike, jitahidi ucheze kwa kuangalia strength ya Bergkamp, jifunze ni muda gani atakua anaenda mbele muda gani atasimama" muda huo Henry kazoea kucheza na Pires.
Henry anasema akaanza kujifunza Bergkamp anachezaje, by doing so, Henry akaonekana bora na Bergkamp akaonekana bora. (Naweza kua nimechanganya majina hapa)
So tuanze Kai ana strength gani? Kwanini alikua anascore easily Ujerumani? Kai anakua comfortable akiwa kati huku akiwepo mtu anayeweza kufanya naye one two za karibu. Naturally ni AM hii ni kusema jamaa with enough confidence kupangua watu wawili siyo shida.
Chelsea na Arsenal hakuna Kocha aliyejaribu kucheza kwa strengths zake. Vieira ni tactically gifted and technical genius hii isikufool ukatamani aanze mechi bado hana hiyo stamina but ana vision na hii ndiyo silaha best kwake, due to this, hata kudefend anaweza.
Kai anastruggle kote, aanzie benchi. Niliwahi kua reddit siku fulani kuna member akasema anaishi karibu na Kai kama kuna ujumbe wowote tumpe amgee. Mashabiki wengi tukasema of coz bado hajaclick ila mwambie tunamuamini, wachache wakasema ukikutana naye mtaani ongea mambo ya mtaani siyo kazini.
We all know jamaa bado anatafuta njia na tunatamani aipate, swali ni lini strength yake itakua unlocked?