mkorea
JF-Expert Member
- Aug 16, 2016
- 8,592
- 19,228
Nyumbu uliekomaa katika ubora wakokikubwa kuwe na uhuru wa kutoa maoni sio watu wachache wajimilikishe jukwaa, pia members wajitahidi kukubaliana katika kutokukubaliana, humu kila mtu ana mawazo tofauti kulingana na upeo wake, unapolazimisha members wote wakubaliane na hoja zako ndio kunapelekea mgawanyo, chuki, kudharauliana na kuanza kutukanana wenyewe kwa wenyewe humu.
Pia members wajitahidi kuheshimu mawazo ya wenzao hata kama wanatofautiana kwenye mitazamo, mtu umemkosoa mara moja, mbili lakini bado anang'ang'ania msimamo wake achana nae endelea kujadiliana na wale ambao mitazamo yenu inafanana, haina haja ya kumuita mtu majina mabaya kisa tu mnatofautiana kwenye jambo moja.
Nyinyi kama mashabiki ya Shenalii mnapohitilafiana katika jambo moja juweni kuna mambo 100 yanayowaunganisha, sasa kwa nini hilo jambo moja linalowatenganisha mnalipa nguvu kuliko yale 100 yanayowaunganisha?
Huu ni ushauri tu kutoka Unyumbuni lakini kipigo chenu leo jioni kiko palepale
View attachment 2737556
Chuma kuanzia 3 zipo pale pale, saka anaweka mawili