Hakuna cha kufungua jukwaa,
Labyrinth 84 humuhumu kwenye jukwaa la Arsenyani ana uhuru wa kuongelea misukule ya Arteta kwa hoja zozote anazoziona yeye zinafaa kikubwa asivunje kanuni tu zilizowekwa na uongozi wa Jf.
Mimi mwenyewe ni nyumbu lakini ni mara chache kunikuta Unyumbuni muda mwingi nashinda humu kuzipiga spana hizi Arsenyau.
Wewe mwenyewe Mc
hamis77 mara kibao unakua unyumbuni kumpiga spana Antony na Kocha la makombe 10hag.
Labyrinth 84 huyu ni muhanga wa false hope alizikua anaaminishwa na maArsenyau wengine kama wewe kwa miaka zaidi ya 20 iliyopita, sasa hivi akili imemkaa sawa na kujitambua kua alikua ni msukule kwa miaka kibao bila ya yeye mwenyewe kujua, hivyo ameamua kuanzisha kampeni maalumu ya kuwazindua misukule mingine ili ijitambue.
Kikubwa inatakiwa mumpe ushirikiano wa kutosha.
Labyrinth 84 una kinga ya turufu kutoka kwangu, endelea kuupiga mwingi maana wewe umeuishi usukule kwa zaidi ya miaka 20 hivyo unajua siri nyingi zaidi za ndani za hawa misukule na virembwe vyao, ndio maana wewe ukiongea hua inawauma sana kuliko hata sisi ambao hatujui mengi kuhusu hawa maFreemason.