Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Sawa dau hilo linamake sense lakini jamaa anakula kwa wiki nafikiri ni 300K kama sikosei.

We unadhani kuna timu itamleta yule ale 300K wakati wenyeji hawana mshahara huo?

Pia mshkaji anafaa City kuliko united, timu inayomiliki mpira, dribble zinaruhusiwa ila temple siyo ya counter
 
Forwards hutengenezi nafasi, huna goals, huna assists ndiyo unataka tuanze stori za Weghorst za mikimbio si ndiyo?
 
Hivi huyu Timber ni beki kweli? Na kama ni beki je anajua kukaba? Maana kila compilation yake YouTube namuona anashambulia tu na kuwatoka wapinzani kwa spins na feints. Utani pembeni...Inaelekea atafaa kama Eboue flani kwenye attacking ila kwenye kakaba isije ikawa ni Trent Alexander-Arnold type. Kwa YouTube unaweza kudhani jamaa hakutani na attackers wa maana. EPL itamchallenge
 
Akubali mshahara wa £120k per week
 
Yule mwana hamna kitu kwa salary anayoruka nayo
Halafu Kumbe hii Ni sababu wachezaji wa manjesta hawauziki aisee kwa Salary hizo hata ukimnunua kwa £10m , akishusha mshahara hata nusu bado Ni mkubwa
 
Ana invert Sana kwenda kwenye midfield ,Anajua kukaba kuliko Zinny ndio utofauti wao

Ana accuracy kubwa ya pass , inamaana itakuwa rahisi kufanya buildup haraka na kwa usahihi
 
Man City wana watu "smart" sana, hiyo ni kuanzia uongozi wa kiofisi mpaka benchi la ufundi, watasumbua sana.
Watasumbua sana.
Watamsumbua nani?, wameshinda treble na mchezaji hawataki, timu haina class, haina tradition wala fanbase, just a plastic club. kwa usajili wa pesa za mafuta hata Norwich inaweza kushinda UEFA.
 
Acha unafiki ,Alivyopost Di marzio siku ile ulisemaje ?

Simamia msimamo wako Kama mwanaume
Huyo jamaa huwa kama demu, kuna mwamba alimquote akamwambia natunza hii comment, haijapita hata wiki anaenda kuumbuka, ana force uhasimu wa liverpool na Arsenal, sisi hasimu wetu ni Man u na Spurs basi, nyie wengine msilazimishe hatuna uhasimu na timu zenu.
 
It's unrealistic assumptions kama unavyojiona wewe kwamba unajua mpira kuliko hao uliowasema
Read between lines chief?
Usisome mambo kimihemko
Ww unajua mm ni shabiki wa timu gani?
Sijasema mm najua mpira wala kuufahamu sana,Am speaking with the experience chief Marafiki zangu wengi ni man united na hawafahamu mpira kiuhalisia
 
Timber na Zinchenko watakuwa wakipanda kusaidia mashambulizi na kukaa sehemu ya kiungo.

Hio ndo sababu Arteta amtaka Timber.

Tomiyasu aweza lakini kuna kipindi hushindwa kusimamia mashambulizi.

Ben White ndo kabisa hawezi mara nyingi huwa weak point.

Hivyo kutafuta balance ya upande wa kulia na kushoto ndi Timber kapatikana acheze na Zinchenko.

Liverpool nao huwatumia Robertson na Trent Alexandra Anold kupanda kusaidia mashambulizi.

Man City huwatumia Kyle Walker (kulia) na Nathan Ake (kushoto) na kuna wakati beki wa kati John Stones huwa mchezaji wa kiungo.

Hiyo ndo system mpya ya uchezaji kwa kuwatumia mabeki wa pembeni na wa kati kuwa wachezaji wa viungo jinsi game linavyoenda.
 
Ana invert Sana kwenda kwenye midfield ,Anajua kukaba kuliko Zinny ndio utofauti wao

Ana accuracy kubwa ya pass , inamaana itakuwa rahisi kufanya buildup haraka na kwa usahihi
Erik alimtaka huyu Timber alivyokaziwa kwa Timber akamgeukia Martinez.

Hapo Arsenal tupo tunafanya donoa donoa Erik akaingia akaweka ofa nene kwa Ajax na mshahara kufuru Martinez akatua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…