Bachelor ll
JF-Expert Member
- Dec 15, 2019
- 4,103
- 6,698
Nipo mkuu! Nipo brother
Di marzio anasema kweli kuwa Chelsea wanaweza act km ilivyokuwa kwa Mudryk, ni suala la Declan mwenyewe kuamua aende wapi, Chelsea sasa hawana natural #6 baada ya kumuuza Jorginho, lakini km tutamkosa Rice bado kuna kiungo mzuri tunaweza kumpata Moses Caicedo. Ila kwangu priority ni Declan Rice jamaa anajua.
Kuna chambuzi linaitwa joji jobuWaliomtilia mashaka Arteta since day one huwa siwaelewi hoja zao Ni zipi
Binafsi mechi ya Kwanza tu nilijua huyu Sasa ndiye mrithi sahihi wa Arsene Wenger
Kaka nakumbuka ulisema msimu wetu ni 23/24 ila tupo ahead of schedule tayariBrother, Ahsante sana kwa kunikumbuka. Nipo japo nimepotea kiasi.
Nawamiss wanangu nyote, nitarudi kuja kusheherekea ubingwa nanyi hapa hapa jukwaani. Sijui kama kuna sherehe yoyote inaandaliwa ya kusheherekea ubingwa na kama ipo basi ntahudhuria kama itakuwa Dar.
Mwanangu isajorsergio upo?
Hivi hatuwezi wapata wote kisha tukaongeza RW?Di marzio anasema kweli kuwa Chelsea wanaweza act km ilivyokuwa kwa Mudryk, ni suala la Declan mwenyewe kuamua aende wapi, Chelsea sasa hawana natural #6 baada ya kumuuza Jorginho, lakini km tutamkosa Rice bado kuna kiungo mzuri tunaweza kumpata Moses Caicedo. Ila kwangu priority ni Declan Rice jamaa anajua.
Binafsi ningependa tumpate CaicedoCaicedo ana pumzi kuliko Rice
Wakati ukifika tutabebaNaona nimepiga kisu Cha mbavu wote mnatoka mafichoni kuja kutapatapa hapa mni jibu kwanini mjawai kubeba hata ueropa kwanza.
Arsenal ingekuwa Man city in the passed 10yrs, sisi wengine tungekua
Tumetoroka Tanzania
Du gori6 kweri nyuma wapo wazi
Haongeze nguvu kweny kukaba yupo softi sanaBEN WHITE
Msimu huu kwa " baadhi " ya mashabiki wa Arsenal wachezaji ambao wapo kwenye mawazo na midomo yao sana ni Saka, Odegaard , Martinelli , Partey , Zinchenko , Saliba , G.Jesus lakini kuna jina inawezekana ukakutana na wana " Gunners " kumi lakini wasilitaje : BEN WHITE
Binafsi naamini ukitaja wachezaji wanne muhimu wa Arsenal msimu huu nitataja jina la Ben White nikiambatanisha na sababu zangu ambazo ni :-
1: Upatikanaji wake uwanjani . Sikumbuki lini nilisikia Ben White atakuwa nje ya dimba kwa miezi kadhaa au wiki 3 . Moja ya sifa kubwa kwa mchezaji bora ni upatikanaji wake
2: Kutoka kuwa beki wa kati mpaka beki wa kulia na kucheza hiyo nafasi utasema ndio ulianzia huko maisha yako ya soka sio rahisi hata kidogo . Binafsi naamini ni nafuu kuwa beki wa pembeni kucheza beki wa kati kuliko wa kati kuwa fullback
3: Ben White amekuwa muhimu sana katika muundo wa uchezaji wa Arsenal na ana husika katika phase zote tatu . Kuna wachezaji ambao wanahusika :-
A : Kwenye phase ya kwanza pekee ( kuanzisha mpira nyuma ) build up
B: Phase ya pili pekee ( kwenye kiungo )
C: Phase ya tatu pekee : kwenye ushambuliaji
Lakini Ben White ndani ya Arsenal anatumika kwenye phase zote tatu ... kivipi ?
Arsenal wakiwa na mpira White anabaki nyuma kutengeneza BACK 3 ( White Saliba na Gabriel ) ili kumruhusu Zinchenko kuingia ndani kama kiungo karibu na Partey kwenye muundo wa 3-2-2-3
Arsenal wakisogea juu Ben White anakuwa kama msingi wa Bukayo Saka na Odegaard ule upande wa kulia wa Arsenal ( Odegaard kama namba 8 wa kulia , Saka winger na White anakuwa nyuma yao .
Wakifika eneo la wapinzani Ben White anakuwa mara nyingi mpishi wa Saka kwa kupiga pasi za ndani zaidi ni mara chache kumuona White anafanya overlaps
Kuna hili sasa la muhimu sana : waangalie Arsenal wakiwa na mpira na position ya White : kwenye ile " REST DEFENSE " ya Arsenal ( Yani namaanisha shape yao ya ulinzi wakiwa wanashambulia ) yeye anakuwa sambamba na Zincheno Partey na White katika mstari mmoja compact mbele ya Saliba na Gabriel wakiwa tayari kuzuia counter attacks lakini pia kupora mpira na kuurejesha kwa watu wa mbele ( recycle possession to sustain attacks )
Wakubwa tunaposema tutaidominate hii ligi kwa miaka 10+ tunamaanisha
Kuna balaa hili hapa dogo anaitwa Charlie Patino yupo Blackpool kwa mkopo
Anacheza CM(LCM) nafasi ya Granit Xhaka
Unyumbulifu
Tackling
One touch football
Press resistant
Tight spaces
Long balls
Interception
Kama atarudi msimu ujao sehemu ya kuimprove ni physicality tu
Naweza kum-rate huyu ahead of Vieira (Maoni yangu)
Kama tukimpata Caicedo/Rice tukaongeza RW na RB naona tutaenda kuchallenge UEFA next season
makaveli10 ukipata muda mfatilie huyuView attachment 2564677
Na kuna uwezekano tusimrudie pia ila tukimpata Rice ni good dealNi ngumu kumpata Caicedo kuliko Rice, simpi nafasi ya kuja Arsenal kwa sababu price tag itakuwa kubwa mno
Na uzinguaji wa timu yake umezidi.Ni ngumu kumpata Caicedo kuliko Rice, simpi nafasi ya kuja Arsenal kwa sababu price tag itakuwa kubwa mno
Aah HapanaNext week tupo na Leeds ,anakuja Emirates
Another chance ya kuongeza points 3
Man City atakuwa na Liverpool , Liverpool akikaza ambatue au sare inatosha
Gepu la points liwe 10-11