Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Kwani nimemtolea heshima yake ? Mimi naongea uhalisia hata yeye anakubali alipotezwa hasa first half

Mechi inaisha alishinda but anatoka na possession ya 36% sikumbuki mwaka gan aliwahi kutoka na possession ndogo hivo ,sikumbuki lini Pep anabadili kutoanzia mpira nyuma Bali anabutua ,

Tunachambua mpira kwa uhalisia nyie mnaleta ushabiki


Ndio nyie mlikuwa mnatupigia kelele Conte ni title contender kwa ule mpira wa ovyo
Imagine tunacheza knockout stage FT unaanza sifia possesion wakati ukisoma ubao tumekufa sisi!
Kumfunga pep kwa aina ya mpira wao na sisi tunaocheza ni zaidi ya kumiliki mpira, yaan inabidi uwe katili kwenye kutumia nafasi.
 
Imagine tunacheza knockout stage FT unaanza sifia possesion wakati ukisoma ubao tumekufa sisi!
Kumfunga pep kwa aina ya mpira wao na sisi tunaocheza ni zaidi ya kumiliki mpira, yaan inabidi uwe katili kwenye kutumia nafasi.
Mbona nimezungumza haya Mambo labda Kama unatafuta ubishani

Nimeongelea nafas walizokosa Nketiha ,Xhaka ,n.k

Thus why nimesema mechi ya 2 naimani nayo Coz ,tutakuwa na kina Trossard ,Jesus pale mbele ,mbona simple tu kuelewa
 
Arteta on Jesus


-"Yesterday I looked in his eyes and he said ‘I’m ready’. I said ‘OK!’. It’s that first step to give him the big boost. He looks free, he looks ready and straight away he generated those two big chances. It’s great to have him back."

(@kayakaynak97 )
 
Halaf kuna mataahira huko yanaropokwa from no where "landan iz buluu..." smh
20230312_202808.jpg
 
BUILDUP MONSTERS

Umeiona Ile Pasi ya William SALIBA kwa Granit Xhaka kwenye bao la pili la Arsenal? Tena kwa kutumia mguu wa kushoto? World class

Ile ndo Sababu Arsenal ni team bora EPL kwenye kujenga shambulizi Kuanzia nyuma.Ili ujenge shambulizi vizuri kuanzia nyuma unahitaji (A) Uwe Wana wachezaji ambao wapo vizuri mpira ukiwa mguuni kwao.Arsenal Ina Saliba, Gabriel,Ben White, Zinchenko, Ramsdale.

Lakini pia Lazima kuwepo na Muundo mzuri wenye virutubisho vyote kuwezesha ujenzi Bora wa hilo shambulizi.Arsenal mara nyingi wanajenga mashambulizi Muundo ukiwa 3+2.Gabriel , SALIBA na White+Thomas Partey na Zinchenko

Hata hivyo wakati Mwingine Inategemea na team pinzani inapeleka wachezaji wangapi kufanya Pressing? Kwa mfano kwenye hili bao, Fulham walifanya Man to Man Pressing kwa Sekunde 30.Maana yake walipeleka wachezaji 6 , Mitrovic akiweka Pressure kwa Ramsdale.

Lakini bado Arsenal walifanikiwa kutoka, unajua Kwanini? Position ya Granit Xhaka ule upande wa kushoto ikawa sehemu maalumu ya Arsenal kutoka kwenye Presha ya FULHAM (Out ball)

Hata dhidi ya team bora zenye Muundo mzuri kwenye kuweka presha ndani ya EPL kama Manchester City Bado Arsenal wana uwezo wa kujenga shambulizi kuanzia nyuma Bila wasi wasi na kufanikiwa

Nini umuhimu wa kujenga shambulizi kuanzia nyuma? (A) Kuufungua kwa urahisi Muundo wa kuzuia wa team pinzani.Kwanini? Kwasababu sio rahisi sana kwenye team kwenda kufanya Pressing Halafu bado Muundo wao kwenye kuzuia ukabaki umeungana.Lazima Kuna mashimo mengi mnaayacha nyuma.(B)Kuipa team Muundo mzuri wa kushambulia kwa utulivu na pasi za uhakika

FT English premier league FULHAM 0-3 ARSENAL

Note; Umeshawahi kusikia neno HAT TRICK OF ASSIST? Muulize Leandro Trossard,nitamleta Baadae View attachment 2547896
IMG_20230312_210816.jpg
 
Bao la 2 la Arsenal

Moja ya bao langu bora msimu huu , Sio Goli la papatu papatu

Limetengenezwa kuanzia nyuma

 
Kituo kinacho fuata
Week end ijayo tunakipiga na Palace tukiwa home Ni week end ambayo Mancity hatocheza Epl atakuwa anacheza FA vs Burnley yaani tukishinda hapa tutatengeneza gape la point 8 baada ya hapo mechi inayofuata Mancity vs Liverpool Kama city asipopata ushindi hapo itakuwa poa Sana kwetu maana siku hiyo tutakuwa tunacheza na Leeds daaaaah kila la heri timu yetu kuelekea kwenye mbio za ubingwa....


Kingine Cha kufurahisha tunazidi kupunguza goal difference Kati yetu na city kwa Sasa Ni magoli matano tu.....


Note that zimebaki mechi 11 ligi kutamatikao
IMG_20230312_204627.jpg
 
Week end ijayo tunakipiga na Palace tukiwa home Ni week end ambayo Mancity hatocheza Epl atakuwa anacheza FA vs Burnley yaani tukishinda hapa tutatengeneza gape la point 8 baada ya hapo mechi inayofuata Mancity vs Liverpool Kama city asipopata ushindi hapo itakuwa poa Sana kwetu maana siku hiyo tutakuwa tunacheza na Leeds daaaaah kila la heri timu yetu kuelekea kwenye mbio za ubingwa....


Kingine Cha kufurahisha tunazidi kupunguza goal difference Kati yetu na city kwa Sasa Ni magoli matano tu.....


Note that zimebaki mechi 11 ligi kutamatikaoView attachment 2547942
Asante brO
 
Back
Top Bottom