Kimbinu jamaa wamejiandaa vizuri plus wana morale na hali ya kuwa na kocha mpya basi balaa tupu
Wameweza kumzuia Odegard asipate Uhuru wa kuamua game na pia wameziba mianya ya Saka na Martinel alafu Edie wamemuacha huru kwa sababu hapati huduma
Hapo ndio tunaona umuhimu wa Jesus, jamaa angekuwa anahama na beki za kati muda wote kutokana na movement zake anazofanyaga na sio kama Edie ambae ye anastick tu kati anasubiri kulishwa
Labda aingie Trossard maana yeye anacheza tofauti na Martinel, jamaa waga akipata mpira lazima alazimishe kuingia ndani kwa kuwafata mabeki tofauti na Gabi yeye mara nyingi anaangalia second runner wa kumpa mpira
Anyway, tunajua mechi zote ni ngumu ila hatuna namna zaidi ya kupambana mwanzo mwisho #COYG