Kwa nini umchukie ?? na hiyo ni kazi kama kazi nyingine na hayo ni maoni yake binafsi anachokifanya kimefanikiwa maana ana watu wa kumjibu kwa hiyo hata wewe unampa publicity.
Hajafanikiwa mkuu, ukitoa mafanikio ya kujipatia Ridhki Kwa njia halali hakuna tena mafanikio zaidi ya kuambulia dharau, maana sio mashabiki wa team zingine tu ndio huchukizwa na Neville bali ata wa man Utd kwa sababu jamaa hachambui bali anakuwa CHAWA
Kuongelewa vibaya haijawahi kuwa mafanikio na haitokuja kuwa, Garry hajui kuchambua mpira na hataki kujifunza, ni mtu kwenye wivu na ushabiki maandazi kama vile shabiki wa Simba na Yanga
Hizo kazi za uchambuzi wanazifanya wachezaji wengi wastaafu na bado wanaongea sense na sio ushabiki, wapo kina Roy Keane, Wright, Barbatov,callagher na wengine wengi ambao wakiwa wanachambua mpira wanakuwa very honest
Garry yeye kila siku hakuna team inayocheza vizuri kama man Utd au zaidi ya man Utd, ,utaskia mara Arsenal wameshinda tu ila wamezidiwa sana, Wana bahati sana ila watamaliza nyuma ya man Utd
Jamaa alipata tu bahati ya kucheza mpira ila kichwani kuhusu mpira ni mweupe sana, ye kazi yake ni kukosoa tu makocha na kuhimiza wafukuzwe ni kama vile alivomkalia kooni Potter na Klop
Yeye ukocha ulimshinda mapema sana alipoenda Spain kaishia kushinda game 3 Tu katika game 16 na akatimuliwa, na wenye timu zao wakiskliza uchambuzi wake wa kijinga ndomana hakuna offer yoyote aliyopata ya kufundisha hadi leo
Neville Kwa kibongo bongo ni kama Jorge Job tu wa Wasafi FM, kikubwa anapata Ridhki basi, ila mambo ya kuchambua mpira ni wazi kuwa hajui na hawezi at least kwenye ngumi huko ndio waga anaeleweka, ila achambue mpira unabaki unashangaa tu huyu jamaa alipataje kazi ya uchambuzi ndo alivo Neville sasa