Arsenal (The Gunners) | Special Thread

1st half started a bit sloppy at least for the entire team. White, Partey na Martinelli walikuwa worse - White imetokana na kadi hivyo hakuwa na budi kucheza kwa umakini asiangushe timu.

2nd half ingizo la Tomiyasu limeleta spirit mpya upande wa kulia na deep central right, ilifikia hatua Arsenal wakabaki mabeki wawili na juu yao akibaki Partey.

Partey alirudi kiasi mchezoni na kuanza kuhimili, huku mstari wa Tomiyasu, Xhaka na Zinchenko ukitengenezwa hapa ndio Arsenal ilianza ku-control mpira kwa kiasi chake.

Saka alikuwa tishio na Tomiyasu wamehimili vyema wing ya kulia. Zinny alikuwa the best kwa kila hatua, Xhaka showed determination, Nketiah played his part right. Trossard showed determination na alistahili kuingia dakika ya 65.

What I've learned from the game? Saliba ni mchezaji mzuri lakini bado anakosa utulivu na kusoma mchezo tofauti na Gabriel Magalhães.

Saliba anachelewa kureact likitokea tukio la haraka refer goal la kwanza la Manchester United pia utoaje wake wa pasi ni very predictable timu kupewa pressure.

Martinelli has been awful toka World Cup Qatar kumalizika 1st alipata chance mbili za kupenyeza mpira kwa Saka na Odegaard walikuwa kwenye nafasi nzuri akufanya hivyo.

Anahitaji kusimama na kuwa bora tena na challenge iliyokuja mbele yake Trossard na akirudi Gabriel Jesus anaweza kupoteza game time asipojitathmini.
 
Una safari ndefu sana ya kujifunza mpira
Acheni kukufuru nyie viumbe,
Umfunge Man Utd zaidi ya goli 3 kwa kikosi gani hasa mlichonacho?
Hilo goli la 3 lenyewe refa aliamua kuwapa tu ili mpunguze maneno maneno, maana kabla ya mechi mlikua mmeshaanza kumtuhumu kua atawabeba united.
 
Hongereni Gunners, ule msako mlioupiga dakika 20 za mwisho ilikua haina budi mpate goli.
Saka leo ndio MoTM, huyu dogo akikutana na beki inayovuja kama Shaw hua anang'aa kwelikweli.
View attachment 2491891
Sio kwamba shaw anavuja, timu zote zinazokutana na Arsenal Saka hua anakabwa na wachezaji wawili hadi watatu ila kwa leo Man u alikua ni shaw tu kwaiyo lazima uone anavuja sana.
 
Mkuu pep saizi anatusubiri tu kwenye game zetu maana anajua fika tutakuwa na pressure juu juu kama kuku kwenye joto kali
Kila mechi huwa ina mbinu yake na sometimes pia wachezaji nao wana ari zao kila mechi.

Pep naye ni mtu wa mpira ana pressure na Arsenal sifikirii kama atakuja kwa mazoea. Kwa ari waliyonayo wachezaji wa Arsenal, mentality yao ni ushindi ni lazima uwe na mentality ya ushindi kabla ya kushinda.

Binafsi Man Utd leo hatupaswi kumbeza wamecheza vizuri saaana wanakosa Unity tu. Niliangalia interview za wachezaji wa Arsenal kabla ya hii mechi hasa Odê na Saliba ni watu ambao walikuwa wamekamia mechi na Utd. Mechi baada ya mechi makosa yanapungua kwa Arsenal.
 
David Beckham’s son, Romeo - a BIG Arsenal fan - on Instagram: “Sleep tight dad
️” #afc


Beckham Ni mzaliwa wa London aliyeenda Manchester United kutafuta ugali , ndio maana mwanae Romeo Ni mshabiki wa Arsenal

Na Mara kadhaa Beckham alikuwa anafanya mazoezi Colney
 
Sio kwamba shaw anavuja, timu zote zinazokutana na Arsenal Saka hua anakabwa na wachezaji wawili hadi watatu ila kwa leo Man u alikua ni shaw tu kwaiyo lazima uone anavuja sana.
Saka akigundua unataka kumsumbua Sana ,huwa anatabia wanakuwa karibu na ode wanapiga Killer pass

Ndio maana naweza kukupa homework Ni beki gani mechi iliisha ukasema kweli leo Saka kakamatika ,ndio maana mpango kazi huwa anawekewa beki wawili wamdhibiti,

Ikitokea silaha yake ya pili Ni kupiga pass za karibu kwa Øde
 
Wenzio tayari wameshakaza mafuvu ya vichwa vyao, hawataki kabisa kusikia habari nyingine zaidi ya Arsenal kubeba ndoo na Haaland kiatu.
Sitashangaa wenzio kukuita mamluki/msaliti kwa huu ukweli uliowaambia.
 
Wenzio tayari wameshakaza mafuvu ya vichwa vyao, hawataki kabisa kusikia habari nyingine zaidi ya Arsenal kubeba ndoo na Haaland kiatu.
Sitashangaa wenzio kukuita mamluki/msaliti kwa huu ukweli uliowaambia.
Acha tu waniite mamluki ila me naongea ukweli, points 8 Kwa pep ni ndogo sana labda kama aendelee kusua sua kama mwanzo

Mfano game ya leo tungesuruhu zilikuwa zibaki point 3 na mchezo mmoja mkononi, tufanye huo mchezo tungeshinda zimekuwa points 6

Sasa unamzidi points 6 pep ambaye bado una game nae home and away, na wote tunajua ukweli ni kwamba city uwezo wa kutupiga anao, kwahiyo kama akishinda hizo game 2 ingekuwa tuna level points

Kama shabiki wa Arsenal nataka sana kubeba hii ndoo ila haitokuwa rahisi hivi kama ambavyo tunataka kujifariji, pep kama kocha mzoefu kuliko wetu na wachezaji wake Wazoefu kuliko wetu

Kuanzia game ya tote city ni kama vile wameamka Fulani hivi na ikitokea waka maintain consistency kuanzia hapa hadi mwisho sio ajabu wao wanaweza, swali je nasie tunaweza?

Tunaweza kucheza under pressure kila game bila kupoteza focus yetu? Tunaweza kumantain hii form hadi mwisho? Tunaweza kuendelea kuwa na focus ata kama ikitokea tukapoteza game kadhaa?

Ukweli ni kwamba haiwezi kuwa rahisi ila kwakuwa hatujafika hapa kwa bahati mbaya basi batuna budi kukomaa tu hadi game ya mwisho, ila ukweli utabaki kuwa sio rahisi kama ambavyo tunataka kuaminishana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…