Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Umeongea hekima Sana Flano japo Kuna muda unajichetuaga ,

Huyo jamaa mijadala mingi kaiungia juu kwa juu

Sasa kwakuwa sisi wengine hatutaki mabishano tunakaa pembeni aendelee kubwabwaja
mimi kujichetua kwangu hua ni kwa ajili tu ya kuchangamsha jukwaa kwa utani wa hapa na pale, na sio kwenye hili jukwaa peke yake, ukitembelea jukwaa la Chelsea utanikuta nawachokoza kenge huko, ukienda kwenye jukwaa la Liverpool utanikuta pia huko nawatia moto, ila ikifikia hatua ya kutoleana lugha chafu na matusi huo napotea zangu tu kimya kimya.
Mpira ni burudani iliyojaa furaha na shangwe lakini ukishaingia ugomvi na matusi inakua sio tena burudani.
Pamoja sana mkuu mimi nalikubali jukwaa lenu kwa sababu limechangamka sana siku hizi yaani lina amsha amsha kama zote tofauti na majukwaa ya timu nyingine yamepoaaaa, sijui kwa sababu mnaongoza ligi?
Ila kileleni baridi kali sana aaaiiiseee hamis77 ameshaanza kuganda.
Screenshot_20221119_110602.jpg
 
Vyombo vya Spain ndio vina danganya Sana kuhusu arsenal kuwa serious na Felix

Tier 1 wanasema ,Wakala wake amemuofa Felix kwa vilabu mbalimbali Hadi Astonvilla


“Despite some reports about Arsenal moving into a strong position, my understanding is that there are no favourites at this stage for Joao Felix.

“His agent is speaking to many clubs. Nothing is advanced yet with Atletico or with the player."

- @FabrizioRomano
 
Huyu jamaa amekuja juzi juzi humu Basi anavamia mijadala juu juu anaruka nayo analeta ujuaji wake .

Huyu sio wakumjibu
hamis77 humu jukwaani wewe ndio na kutegemea uwe kama kaka yao kutokana na busara zako, hata ukikosekana siku moja humu hua lazima nikuulizie.
Kwa hili naomba lipite haina haja ya kulumbana pasipo sababu ya msingi.
Tujihadi kuvumiliana katika mambo madogo madogo tunayotofautiana na huo ndio ubinaadamu wenyewe, mawazo yetu wote kamwe hayawezi kua sawa.
Jitahidini kuliimarisha hili jukwaa kwa negative comments, Mashabiki wa Arsenal wote mnatakiwa kua kitu kimoja haya malumbano yasiyokwisha hayasaidii lolote zaidi ya kujengeana chuki tu wenyewe kwa wenyewe.
 
Imo Mudryk is the next big thing, a superstar in the making, habari za Felix zinakuja cuz Jesus kaumia, Felix ni versatile na anafanya majukumu ya Jesus lakini hatukumuhitaji toka mwanzo, tulihitaji natural winger, Mudryk ni natural winger kama saka & Martinelli, Jesus / Felix wanaweza cheza wide areas lakini sio natural. Tujifunze kuangalia profile ya mchezaji tunayemuhitaji, ni vizuri kuwa na Mudryk, Jesus & Nketiah itatupa balance kuliko kuwa na Jesus, Felix & Nketiah.
IMG_20221213_153003.jpg
 
Kama alivyosema Arteta ,lokonga DM haiwezi hivo wanamsogeza no.8 anayocheza Xhaka


Vieira anacheza No.10 ya Odegaard pia anacheza no.8 anayocheza Xhaka Lakini anacheza pia RW kwa saka


Mechi na Wolves alicheza no.8 kwa Xhaka akacheza Vizuri

Baadhi ya mechi ikiwepo iliyopita na ya leo atacheza RW


Arteta alisema wachezaji wanatakiwa ku adapt nafasi tofautitofauti ,


Mpaka Sasa Ni wachezaji wachache Sana ndani yakikosi wapo limited kucheza nafasi moja .
 
Reiss Nelson looks dangerous.

Nketiah, Partey & Sambi have all started very well.
 
| GOAL! #Arsenal take the lead as Martin Ødegaard scores! Fantastic free kick. #afc

#Arsenal 1-0 AC Milan
 
Back
Top Bottom