Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

| Gabriel Martinelli:

"Nataka kushinda mataji, nataka kuwa mabingwa. Nadhani klabu, mashabiki na wachezaji tulionao, wanastahili kushinda kitu. "Na hiyo ndiyo ndoto yangu, kushinda Ligi Kuu, kushinda Ligi ya Mabingwa."

| Gabriel Martinelli kuhusu Vibe la mashabiki Emirate

"....... unapokimbiza mpira, na unahisi kuchoka unataka kukata tamaa ... mashabiki 60,000 wanaimba pande zote ... utaupata mpira huo. The energy boost is incredible."

unakumbuka mnamo Agosti wakati Saliba alipojifunga bao dhidi ya Leicester? Alikuwa anarudi nyuma huku akiwa na hasira, na labda mashabiki wengine wangemzomea. Lakini mashabiki wetu walishangilia. Walikuwa wakimuimba”

"Wao [mashabiki] walikuwa wakimwambia [Saliba baada ya kujifunga], 'Tuko pamoja nawe hata iweje.' Dakika mbili baadaye, tulifunga bao.

Hiyo ndiyo Arsenal.”


: "Tutaendelea kutafuta ushindi kila mchezo, ndivyo klabu hii inapaswa kufanya. Arsenal sio kuhusu ‘kupata pointi’. Arsenal sio kuhusu kumaliza nafasi ya nne. Arsenal inahitaji kupigania mataji, ligi, Ligi ya Mabingwa. Hicho ndicho ambacho mashabiki wanastahili.”



SAFARI YA KUJA ULAYA

Ninamshukuru Mungu kwamba nilikuja Arsenal mwaka wa 2019. Ninaamini sana kwamba mambo hutokea kwa sababu fulani, na nina furaha sana hapa.

Inafurahisha kutazama nyuma nilipotoka, kwa sababu ningeweza kuishia mahali pengine kwa urahisi. Unaona, niliwahi kuwa sehemu ya majaribio huko Manchester United. Kwa kweli nilikuwepo kwa majaribio kadhaa.

Nilikutana na wachezaji wengi wakubwa. Nilipokuwa na umri wa miaka 17, nilifanya majaribio yangu ya mwisho huko, kwa hiyo nilirudi Brazili nikingoja Matokeo.

Siku moja baba aliniita sebuleni. Alikuwa amezungumza na wakala wangu ..

Aliniambia Manchester United walikuwa wamesema hapana. Sio tu, "Hapana, kwa mwaka huu." Lakini, “Hapana, hatumtaki. hata kidogo.”


Kusema kweli, niliumia. Walikuwa wameniona nikicheza mara kadhaa katika Majaribio na nilikuwa na uhakika wangenisajili.

Wiki chache baadaye nilipata majaribio mengine, huko Barcelona. Nilitumia siku 15 huko. Hawakunitaka pia. Hilo lilikuwa rahisi kukubali, kwa sababu ilikuwa TRIAL(jaribio) moja tu, tofauti ya Kule Manchester United ambako nilifanya majaribio mengi….

Nakumbuka niliketi na baba yangu na kusema,

“Tutafanya nini?”

Nikurudi BRAZIL TU.....

Miaka kadhaa baadaye, Baada ya United kusema hawakunitaka

. Kwa bahati nzuri, mara baada ya hapo nilikuwa nikifanya vyema sana katika Copinha - Kombe la Vijana maarufu la São Paulo .

Ofa mpya zilikuwa zinakuja. Rafael aliponiambia kuwa Arsenal wananihitaji, sikufikiria mara mbili.

Nilimuuliza Baba, “Unaonaje?”

Alisema, "Twende London."

Hatua bora tuliyowahi kufanya.



MAISHA LONDON HAYAKUWA MARAHISI

Sikuweza kuendesha gari pia. Lazima uzungumze Kiingereza ili kupata leseni.

Nilitumia miaka miwili kupata usafiri au kuagiza Ubers. Unajua ni nani aliyeniokoa? Emi Martinez.

! Aliishi dakika 10 kutoka nyumbani kwangu, kwa hivyo alinichukua ili kunipeleka kwenye mazoezi na uwanjani. Wakati mwingine tungemchukua Dani Ceballos. Emi daima alijaribu kusaidia kila mtu. Wakati mmoja, hata nilitumia muda wa Mwaka Mpya nyumbani kwake na familia yake.

Pia nilipata usaidizi mwingi kutoka kwa David Luiz, mtu mwingine wa kustaajabisha. Bila watu kama hawa mwanzo wangu ungekuwa mgumu sana.

Nilichukua masomo ya Kiingereza mara tatu kwa wiki. Nilitazama sinema na mpenzi wangu. Ninampenda, lakini jamani, ananikera! Ingawa anatoka Rio de jenairo daima anataka kutazama kwa Kiingereza na mimi nataka kutazama kwa Kireno.


Lakini wakati ambao nilihitaji sana usaidizi ni nilipopata jeraha la goti msimu wa joto wa 2020.

Nilikuwa nikifanya mazoezi niliposikia maumivu kwenye goti langu.

Madaktari waliniambia nilikuwa nimeharibu gegedu(Cartilage).

Miezi mitano nje.

Nilitokwa na machozi. Sikuweza kuamini. Nilikuwa nimeteguka kifundo cha mguu hapo awali, lakini hii ilikuwa nusu mwaka bila kufanya kile ninachopenda. Sikuweza hata kuweka uzito kwenye mguu wangu. Lakini baada ya wiki moja nilijisemea,

"Hey, hakuna maana ya kulia. Tuendelee.”

Mnamo Desemba nilirudi. Basi nini kilitokea? Nimeumia tena!! Katika mwanzo wangu wa kwanza, kipa wa pili wa Man City, Zack Steffen, aliruka ndani yangu. Nilikuwa najizungusha kwa maumivu, ikabidi nitoke nje.

Bila shaka nilikuwa na wasiwasi. Bahati nzuri haikuwa serious. Wiki chache baadaye nilikuwa karibu kuanza dhidi ya Newcastle, na nilitonesha kifundo cha mguu wangu . Wiki nyingine nje.

Kwa hivyo kurudi kwangu hakukuwa rahisi kabisa.

Mikel amekuwa mtu mzuri kwanu kila wakati. Wakati sikuwa nikicheza sana msimu uliopita, nilienda ofisini kwake, na akanihakikishia kwamba nitapata nafasi yangu. Ninataka tu kucheza kila mchezo, unajua?

Hata nilipotoka sub dhidi ya Forest siku nyingine, nilisema, "Ah, ningependa kufunga bao lingine ...."

Lakini tuna michezo mingi. Naelewa. Nimefurahia sana kwamba nilichukua nafasi yangu nilipoipata. Naipenda sana klabu hii. Kikosi ni kama familia kubwa.

Sote tunaheshimiana sana. Ukituona kwenye mazoezi utaelewa kwa nini tunacheza vizuri, kwa sababu hata katika mchezo rahisi wa pasi hakuna anayetaka kupoteza. Nyumbani bado hatujapoteza pointi, kwa sababu hali ya msimu huu ni bora zaidi kuliko hapo awali. Wapinzani wanahisi presha kila wakati Emirates.


Chanzo😛layer Tribune

Mtafsiri: Mimi



View attachment 2420976
ha haaaaaaaaaaaaa mtafsiri wewe
 
That's why hata timu yao ya Taifa(England 󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿)haina Maajabu! Miaka nenda rudi
Hivi sasa England tayari imeshapangiwa first 11 vs Iran na waandishi wa habari, columnists, wapambe, mawakala, majarida, mucisians, editors, fans, walevi, mashoga, pundits, akina Neville..
etc. Hapo kuna timu kweli?
 
England wana timu nzuri, quality all over the pitch, ila final nadhani watacheza Brazil & Argentina. Timu km Brazil/Argentina kuna wachezaji wengi wanaocheza timu kubwa ulaya siku hizi, hivyo wamepata elimu bora kimbinu chini ya makocha bora ex: Pep, Simeone, klopp, Arteta plus vipaji walivyonavyo, kama technical bench watakuja na system inayofit profile walizonazo now they're unstoppable. Sidhani kama kuna timu nzuri kuzidi Brazil kwenye WC, all eyes on Tite now, binafsi naipenda Brazil ila Messi nampenda zaidi, God save the king.
 
Ukiachana na ARSENAL sina uzalendo na timu yoyote hapa duniani club or taifa

Argentina
Nimekua muargentina kwa sababu ya andunje messi, lapulga
Japo kabla ya kulikuwepo pia batistuta
Na akija retire national team, na mimi itakua bye bye na Argentina
I wish this year uwe mwaka wao

Netherlands
Niliipenda kwa sababu ya akina Ruben, Snider,
Na aina ya mpira wao ulikua unanikosha sana
Netherland ya sasa hivi wanajaribu kunivuta tena lakini ndio hivyo, hakuna kitu

Germany
Hili taifa huwa nalikubali tu
Kuanzia mambo ukoloni, technology na nyanja zingine

Binafsi ndio huwa naliona taifa teule
Achana na mtu anaeitwa mjerumani, ata zile adhina zao (Mali za mjerumani)
Ata Tanzania tungekua chini ya mjerumani tungekua mbali sana
Huwa nasikitika kutawaliwa kwa muda mchache na hili taifa
Sifurahii kutawaliwa, ukweli ni kuwa akili za watanganyika na afrika kiujumla zililala, kwaio ilibidi tupate external force ya kutuamsha

Mjerumani muda wa kazi ni kazi
Na kazi za mjerumani hana show mbovu
Majengo, vifaa,
Na inasemekan mjerumani ni miongoni mwa taifa top3 kwa uchawi duniani
Wenzetu uchawi wanautumia vizuri sana
Sio sisi watanzania

Hayo maelezo ndio yanafanya hadi timu yao ya taifa niwe naifatilia
Wakiwa vizuri naburudika nao, wakiwa hovyo wanabaki wao wenye
Lakini WC hii siwaoni wakifika mbali


Brazil
Hii ni timu ya dunia, haujaipenda Brazil haujaupenda mpira
Kizazi cha kina ronaldinho 2002 pale Japan
Ilikua hatari sana
Kizazi cha pekee sana kuwai kutokea
Nkumbuka michuoano hiyo nilikua nacheki na bimkubwa, bimkubwa mwenyewe alikua anaburudika jinsi ronaldinho gaucho alivyokua anafanya matusi yake uwanjani
Ronaldo og, gaucho, Carlos, cafu, rivaldo
Hilo combo sidhani kama litakuja kutokea
Ata WC hii nawao wapo vizuri kimtindo

Argentina
Brazil

NB
Sinagana uzalendo na taifa lolote hapa duniani
 
England wana timu nzuri, quality all over the pitch, ila final nadhani watacheza Brazil & Argentina. Timu km Brazil/Argentina kuna wachezaji wengi wanaocheza timu kubwa ulaya siku hizi, hivyo wamepata elimu bora kimbinu chini ya makocha bora ex: Pep, Simeone, klopp, Arteta plus vipaji walivyonavyo, kama technical bench watakuja na system inayofit profile walizonazo now they're unstoppable. Sidhani kama kuna timu nzuri kuzidi Brazil kwenye WC, all eyes on Tite now, binafsi naipenda Brazil ila Messi nampenda zaidi, God save the king.
Eti kocha bora ukamtaja Arteta, hivi nyie Arse88 mmerogwa? Nahisigi kuna nyaya zinagusanga nyie watu.
 
Arteta has ruined the fun of this sport because every team I watch now that isn’t Arsenal play so dead compared to us
 
Eti kocha bora ukamtaja Arteta, hivi nyie Arse88 mmerogwa? Nahisigi kuna nyaya zinagusanga nyie watu.
Bora umuelekeze,,,, anapewa ubora kwa kipi ? Huyo ni upcoming, lets wait and see ! One season wonder !!!!

Kashinda kombe gani la maana ? Au Ni ile FA ?
 
Bora umuelekeze,,,, anapewa ubora kwa kipi ? Huyo ni upcoming, lets wait and see ! One season wonder !!!!

Kashinda kombe gani la maana ? Au Ni ile FA ?
Season wonder gani? wkt hata robo y msimu bado, msimu huu akijitahid sana nafas y tano. Wanajazanaga ujinga hapa kama hujui utafikiri wana timu y kina xav,inesta,mess na kocha pep.
 
Bora umuelekeze,,,, anapewa ubora kwa kipi ? Huyo ni upcoming, lets wait and see ! One season wonder !!!!

Kashinda kombe gani la maana ? Au Ni ile FA ?
Unaumia Sana ,Arteta ana miaka 2 na miezi 10 , ana FA cup kabatini, timu ipo mikono salama, au unadhani sawa na kina ole guna, Kama mlivyokuwa mnadai,?

One season wonder? Wivu utakuua, hata Cr7 mwenyewe anataman jinsi Arsenal wanavyokichafua,

Manyumbu mnahitaji miaka 3 angalau mcheze hivi anavyocheza arsenal ,japo CR7 na waliopita hapo unyumbuni wanadai inaweza kuwachukua miaka 10
 
Season wonder gani? wkt hata robo y msimu bado, msimu huu akijitahid sana nafas y tano. Wanajazanaga ujinga hapa kama hujui utafikiri wana timu y kina xav,inesta,mess na kocha pep.
Ulitaka tusifie litimu lako ambalo hata pass mbili haliwezi?

Timu limetumia £300m linazidiwa hata na ihefu kiuchezaji

Ulitaka tulizungumzie ?

Kumbe tunavyojadili Arsenal inawauma


Unanunua Sterling, nafasi 20 goli 1, auba mzee, kolobai mzee, unataka tuseme timu yenu Bora
 
Unaumia Sana ,Arteta ana miaka 2 na miezi 10 , ana FA cup kabatini, timu ipo mikono salama, au unadhani sawa na kina ole guna, Kama mlivyokuwa mnadai,?

One season wonder? Wivu utakuua, hata Cr7 mwenyewe anataman jinsi Arsenal wanavyokichafua,

Manyumbu mnahitaji miaka 3 angalau mcheze hivi anavyocheza arsenal ,japo CR7 na waliopita hapo unyumbuni wanadai inaweza kuwachukua miaka 10
Mwezi wa tano next year utakuja na kauli nyingine hapa jukwaani !
 
Mwezi wa tano next year utakuja na kauli nyingine hapa jukwaani !
Unapiga ramli manyumbu bhana ,timu lako bovu ,najua mnataman icheze Kama Arsenal ila haiwezekani hata cr7 kasema

Zlatan Ibrahimovic
“Kila Mtu Anafikiri Kuwa Manchester United Ni Klabu Kubwa Miongoni mwa Klabu Tajiri Na Klabu Yenye Nguvu Duniani,Kwa Mtazamo Wa Nje Ndivyo Inavyoonekana."
“....Lakini Nilipokuwa Pale Niligundua Ni Timu Ndogo, Yenye Mawazo Yaliyofungwa.." h
 
Back
Top Bottom