Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Tusimpuuze city kiasi hicho...

Kuuthibitishia umma kuwa tuko serious, tumfunge huyu Liverpool nusu, tukishindwa kumfunga Liverpool kiwete tutakuwa hatuko serious na ule ugonjwa wetu wa big games utakuwa haujaisha.
Liver hakuna kitu pale labda wakamie mechi kama ndugu zao manyuu
 
Partey ni mtu na nusu, binafsi anapocheza Partey nakuwa na amani kuwa mido itatawala mchezo na uwezo wa kushinda ni mkubwa sana.

Hongereni gunners, walau tumeona total dominance against a top team, hivi kumbe spurs sit back kiasi hicho?
 
Bila hiyana wala choyo Arsenyani mnaubonda mwingi ingawa magoli yenu mengi ni ya kubahatisha sana, yaani mpira unauona kabisa unaenda nje halafu ghafla unadunda kwenye jiwe unajaa wavuni


Msibisheeeeeee

Ila kipa wa Spurs lazima kamati ya FA tumuite kwa mahojiano, lile goli la pili mpira alikua ashaudaka kabisa halafu akauachia makusudi upite, kama hakubeti basi lazima atakua amepokea hongo ili auze mechi.

Will Jr usijitoe ufahamu na kujifanya kukanusha kua Partey ana low IQ.
 
Japo Ni msumbufu humu, ila nakukubali kwakutucharua ,

Kesho mkazieno city hata sare TU inatosha
 
Partey ni mtu na nusu, binafsi anapocheza Partey nakuwa na amani kuwa mido itatawala mchezo na uwezo wa kushinda ni mkubwa sana.

Hongereni gunners, walau tumeona total dominance against a top team, hivi kumbe spurs sit back kiasi hicho?
Spurs Toka ligi inaanza nilisema ,kwa uchezaji ule watakamatika TU,the same na man u ,weatham,

Wanakaa nyuma wanategea kaunta


Spurs Hana tofaut na Burney ,, tofaut Spurs ana Hary kane

Spurs mech karibu 98% anakaa nyuma hata kwa weak opponent

UCL alikutana na Sporting Lisbon wanaupanga mpira hatari ,

Spursy alimfunga 6 Leicester Cha ajabu Leicester ndiye aliikamata game in terms of control

Kilichotokea Leicester Wana shida ya kipa , hivo Spurs akashinda 6 ila kwa matatizo individual ya kipa Leicester.

Huwez kuwa Bingwa kwa ule Mpira wa Spurs ,
 
Ndio maana nikasema kuthibitisha kama tulo serious tuwagonge liver nusu.
Msimu uliopita mech za Emirates dhidi ya Liverpool and mancity tulitoa warning

Mech na city kabla ya red card na refa kutunyima penalty , City tulimkamata kisawasawa ,

Mech dhidi ya Liverpool 1st half ode ,laca ilikuwa waimalize mech, 2nd half Ramsdale aliumia hakusema akafungwa goli za kizembe

But hizi mech mm sikutoka na matokeo tu kuwa tumefungwa basi, nilionddoka na positive things

Kwanza mech zote mbili Partey aliwaonyesha Viungo wa Liverpool and mancity kuwa anauwezo wakuwapoteza na wakatulia

Ile kwangu ilikuwa Alarm kwa hata tunavyocheza Sasa,
 
Japo Ni msumbufu humu, ila nakukubali kwakutucharua ,

Kesho mkazieno city hata sare TU inatosha
mpira bila ya utani (tambo) na kejeli za mashabiki hua haunogi kabisaaaa.
Ila kiukweli mnaupiga mwingi mpaka tunawaonea wivu ila mtambue tu kutangulia sio kufika.
Kuhusu City wala usiwe na shaka kabisa, timu zinazojifanya unbeaten sisi ndio kiboko yao, hata nyie Arse
mnalitambua hilo.
Hivi hamis 77 amepotelea wapi?
Jamaa hua namkubali sana yule, kama wiki inafika sijamuona humu.
Kwenye mechi kubwa kama za leo sio kawaida yake kabisa kukosena kwenye hili jukwaa.
 
Liver hakuna kitu pale labda wakamie mechi kama ndugu zao manyuu
Ukicheza na Arsenal hii ndani ya uwanja wa Emirates hakuna timu inayoweza kubisha.

Ni mwendo wa kufatwa mwanzo mwisho.

Uwepo wa hawa watu; Partey, Zinchenko, Saliba, Jesus bila ya kumsahau Saka na Ødegaard unanipa amani sana ya kuendelea kuishabiki hii timu.
 
William Saliba is yet to be successfully dribbled past by an opponent in his 720 minutes of Premier League football this season, while he has also won possession more times (71) than any other player in the league. [@Squawka] #afc
 
Mkuu Leo hautupitishi darasani kidogo kwenye somo la historia??
 
Ukiacha ushindi, mambo mengine yaliyonipa furaha leo ni kuona Jesus amemaliza bila ya yellow card na Partey amemaliza akiwa salama.

Sasa tunaweza kuwakaribisha Liverpool kwenye uwanja wetu wa ndege.
Jesus kuna rafu 2 alicheza zilikua za kula njano kabisa ila refa aliamua kupotezea.
Ila ile direct red card ya Emerson Royal ilikuwa ni uonevu, refa kwa makusudi kabisa aliamua kuua tu hii game.
 
Jesus kuna rafu 2 alicheza zilikua za kula njano kabisa ila refa aliamua kupotezea.
Ila ile direct red card ya Emerson Royal ilikuwa ni uonevu, refa kwa makusudi kabisa aliamua kuua tu hii game.
Ile ilikuwa dangerous play, ndio maana hata var hawakwenda cz ilikuwa lazima red
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…