Arsenal (The Gunners) | Special Thread

unaposajili CB unaangalia pia na kigezo tunaita height

👆on madern football kumetawala setpieces kama una beki mfupi kazi unayo 😁

kwa uwepo wa saliba na gabriel wapinzani watasubiri sana kuona arsenal ambayo watafungwa goli la kona au cross

Msimu uliopita Kama sikosei tulifungwa goli 1 au 2 kwa kona
 
Mkuu urefu wa mabeki tu peke yake hausadii kuzuia kufungwa magoli ya corner, nadhani ni jinsi gani hao mabeki wako trained katika kuzuia set pieces

Na Kwa msimu uliopita nadhani kilichosaidia arsenal kufungwa goal chache za corner ni kutokana na mafunzo ya kocha wa set pieces

Nitakutolea mfano wa msimu uliopita Kati ya team ambayo imefungwa magoli mengi ya corner ambayo ni Leicester na team ambayo imefungwa magoli machache ambayo ni Man city

Tuangalie urefu wa CB za hizi team mbili
LEICESTER
Fonana 190cm Evans 188cm
MAN CITY
Ruben 186cm Raporte 191cm na kumbuka kuwa kuna game alikuwa anacheza pia Fernandinho kama CB 179cm
ARSENAL
Gabriel 190cm Ben White 185cm

Kwahiyo ukiangalia hizo takwimu issu sio urefu wa CB bali ni how team nzima na hao CB wanadefend na kuattack corner

Kwa upande wa Arsenal msimu uliopita sifa ziende Kwa set pieces coach ambae amefanya Arsenal iwe miongoni wa team zilizofungwa magoli machache ya corner nadhani 2 na imefunga magoli mengi ya corner 13

Ukiangalia Man city ndio wanaongoza Kwa Kufunga magoli mengi ya corner na pia wanafungwa magoli machache ya corner (1) kwahiyo hizo ni sifa za set pieces Nicolas Jover na sio urefu wa CB
 
Wala sijabisha ,na nilishawahi kueleza humu kazi ya Nicolas Jover ,Kocha wa set pieces ,

Urefu Ni moja ya factor inayozingatiwa Sana
 
Arteta on transfers:

"We only want to bring top quality through that door. If not, it's not worth it."
 
Nikusahihishe!

Thomas Partey hakuletwa kuchukua nafasi ya Xhaka ndio maana wapo wote uwanjani. Xhaka hakuwahi kushindwa kazi yake, kinacho kuchanganya na wengine wengi ni kudhani Xhaka ni DF.

Xhaka alitumika hiyo nafasi unayosema "Kazi ilimshinda" kwa kuwa Wenger hakuwa na option ya ziada baada ya majeruhi ya Francis Coquelin, Jack Wilshire, Aaron Ramsey, Santi Cazorla, Chamberlain, inconsistency ya ElNeny, Flamini na Rosicky walikuwa wanondoka na Mikel Arteta alikuwa amestaafu.

Xhaka ndiye aliyecheza nafasi hizo za kati tofauti katika vipindi tofauti pasipokuwa na watu ilifika kipindi baada ya Monreal kuondoka akacheza LB na mara nyingine CB, Ilhali sio nafasi zake.

NAHESHIMU maoni, mtazamo na mawazo yako kama haki ya kila mtu, pia naamini huwezi kupendwa na wote na kuchukiwa na wote. Lakini kitendo cha Xhaka kucheza chini ya makocha 6 timu 5 tofauti First Eleven kila mchezo na zote amekuwa Captain! Lazima kichunguzwe.
 
Mkuu sidhani kama ulimuelewa jamaa, sijaona sehemu uliyomsahihisha kama ulivosema na wala sijaona sehemu ambayo jamaa ameandika kuwa Partey alikuja Arsenal kuwa mbadala wa Xhaka

Na kingine jamaa wala hajaongelea issue ya kwanini Xhaka amepata nafasi Kwa kila kocha na hapo ndio hoja yako ilipo, sijui waga kwanini unapenda sana kuchomekea hii issue ata sehemu ambayo haijaongelewa

Kwa nilivomuelewa Mie, jamaa hapo alikuwa anamjibu mdau ambae alikuwa anasema Partey hana IQ ya mpira Kwa sababu anashindwa kucontrol game

Ndio mshkaji kamjibu Kwa kusema kuwa Partey anatekeleza majukumu yake Kwa A+ akikumbushia last two seasons ambazo hiyo nafasi alikuwa anacheza Xhaka vile alivokuwa anachomesha team na kuishia kufungwa, which is true

Xhaka saizi ana majukumu tofauti na mwanzo ndomana kila mtu saizi anamfurahia, yeye anasogea juu na partey anabaki chini kulink na mabeki akiungana na zinny, ila kwakuwa umekalili kila anapotajwa Xhaka basi atakuwa amesemwa ndomana ata comment husomi inahusu nini we unavamia tu
 

Hatubishani, tunapeana mbili
3 za soka kaka.

Rudia kusoma ulichoandika mkuu, vinajifunga vyenyewe.

1.umesema
"thomas Partey hakuletwa kuchukua nafasi ya Xhaka ndio maana wapo wote uwanjani. Xhaka hakuwahi kushindwa kazi yake, kinacho kuchanganya na wengine wengi ni kudhani Xhaka ni DF.
Sote humu tulikuwa tunalalamika xhaka kutumika katika nafasi asiyoimudu, atumike kama anavyojicheza timu ya taifa, ikafika hatua tukagawanyika, wengine wakisema auzwe (mimi mmoja wapo), japo msimu huu kaimarika.

2. Umesema
"Xhaka alitumika hiyo nafasi unayosema "Kazi ilimshinda" kwa kuwa Wenger hakuwa na option ya ziada baada ya majeruhi ya Francis Coquelin, Jack Wilshire, Aaron Ramsey, Santi Cazorla, Chamberlain, inconsistency ya ElNeny, Flamini na Rosicky walikuwa wanondoka na Mikel Arteta alikuwa amestaafu"
Hapa kwa kilugha maana yake ushakubali xhaka katumika DF, basi partey hakuja kuchukua nafasi ya xhaka ila alikuja kuchheza nafasi ambayo sisi hatuna wa kuicheza kiasi xhaka analazimishwa kucheza hapo.

Mimi sikuwa huko kwanini xhaka anapata nafasi kwa kila kocha, wala partey kaja chukua nafasi, nilikuwa nazungumzia PARITEY KUONEKANA HANA IQ YA SOKA.

ukisoma tena uttanielewa kaka, nimezungumzia kuna vitu si cha mchezaji mmoja, ila ni timu nzima hao kina busquets si kazi ya mtu mmoja ila ni kazi ya timu nzima, na ndio maana ikaitwa timu(kiingereza TEAM)
 
Naona ndugu isajorsergio alisoma ila hakuelewa nimaanishacho.

Shukrani kwa ufafanuzi.

Binafsi alipoluwa anatumika position tofauti na ya national team na kutoa maboko nikatamani hata auzwe aende kwa watu wanaojua kumtumia, ilipokuja pauni milioni 18 ya roma nilitamani aende kiukweli maana tulikuwa tumamdhalilisha.
Msimu huu niliandika sehemu kuwa xhaka ana mabadiliko atatufaa, yule akianza fresh, akiwa benchi fresh pia unakuwa na kikosi kipana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…