Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Sasa hapo hao average players Nani kawasajili kumbuka mmiliki wenu msimu huu katoa mpunga mkubwa Sana ndio Arsenal mmeongoza kwa utoaji wa mkubwa wa usajili nyinyi mkaenda kusajili wachezaji 8 Thomas partey, Tomiyasu, Nuno tavares, Gabriel, Aaron Ramsdale Tierney, lukonga na Ben white kwa huu usajili kwanini umtupie lawama Mmiliki wakati yeye kaplay part yake kwa kutoa mpunga wa kusajili? Kwani yeye ndio wamewasajili hawa wachezaji?
Na ww huelewi chochote kuhusu timu yetu,na timu yako vilevile ina matatizo kibao ndo unapaswa kudeal nayo
 
Hebu chora mchoro wa kubadilishana Makocha Conte aje Arsenal achezeshe kina Nketiah na Arteta aende Spurs awe na kina Son na Kane pale mbele halafu tuone kama Experience matter au Qualities/Class matter.
Huyo conte kwa kikosi kilichopo Arsenal hawezi kukubali kazi ya kuifundisha na ndio alivyo na timu yetu makocha wengi walikuwa wanakimbia kuifundisha na Arteta akavaa hilo Bomu na kwa kocha mwingine kwa kikosi hiki tungekuwa tumeshuka daraja kabisa
 
Mnamfichia udhaifu kocha wenu Arteta kwa kumrushia lawama zote Mmiliki
Wachezaji wenu kibao wanaondoka free kabisa kwasasa
Rudiger
Azpilicueta
Christensen
Alonso

Nedeni mkatafute mabeki wakureplace wanaondoka kwanza

Matatizo yetu yanatutosha wenyewe
 
Mnamfichia udhaifu kocha wenu Arteta kwa kumrushia lawama zote Mmiliki
Mmepoteza fainali mbili dhidi ya Liverpool tens kwa penalty, Mara mbili mfululizo.......nendeni mkajipange na mkaangalie ni wapi mlikosea ili msimu ujao msipoteze fainali kipumbavu

Sisi matatizo yetu yanatutosha mzee
 
Huyo conte kwa kikosi kilichopo Arsenal hawezi kukubali kazi ya kuifundisha na ndio alivyo na timu yetu makocha wengi walikuwa wanakimbia kuifundisha na Arteta akavaa hilo Bomu na kwa kocha mwingine kwa kikosi hiki tungekuwa tumeshuka daraja kabisa
Mashabiki wa AsaniWali kwa kupenda kumkingia kifua Arteta utafikiri yamelishwa limbwata.
Hziyech22 ameuliza Wakati mnawasajili Thomas partey, Tomiyasu, Nuno tavares, Gabriel, Aaron Ramsdale Tierney, lukonga na Ben white kwa mkupuo kocha wenu alikua nani?
 
Mashabiki wa AsaniWali kwa kupenda kumkingia kifua Arteta utafikiri yamelishwa limbwata.
Hziyech22 ameuliza Wakati mnawasajili Thomas partey, Tomiyasu, Nuno tavares, Gabriel, Aaron Ramsdale Tierney, lukonga na Ben white kwa mkupuo kocha wenu alikua nani?
Hilo swali hawawezi kujibu ukimtoa computerarsenal mashabiki wote waliobakia wa Arsenal ni mbumbumbu mnapewa mpunga wa maana na Mmiliki mnaenda kumnunua Lokonga Cha ajabu lawama wanampa Mmiliki?
 
Mmepoteza fainali mbili dhidi ya Liverpool tens kwa penalty, Mara mbili mfululizo.......nendeni mkajipange na mkaangalie ni wapi mlikosea ili msimu ujao msipoteze fainali kipumbavu

Sisi matatizo yetu yanatutosha mzee
Penalty siku zote hazina mwenyewe, wewe hujashiriki kwenye michuano yoyote ya european alafu unashindwa hata kuingia big 4 uoni unamatatizo? Sisi tulipopata bahati kama yenu ya kutocheza michuano yoyote ya ueropen tulitumia vizuri hiyo fursa na tukashinda kombe la Ligi kuu la England uoni tofauti yenu na sisi?
 
Hilo swali hawawezi kujibu ukimtoa computerarsenal mashabiki wote waliobakia wa Arsenal ni mbumbumbu mnapewa mpunga wa maana na Mmiliki mnaenda kumnunua Lokonga Cha ajabu lawama wanampa Mmiliki?
Siku zote hua namlalamikia sana computerarsenal kua hilo litimu analolishabikia haliendani kabisa na IQ yake, ndio maana migogoro kati yake na mashabiki wenzake hua haiishi, na wenzake hua waishia kumtukana na kumuona kama vile ni mamluki kila anapo jitahidi kuelezea mapungufu ya timu yao.
 
Msimu huu namba 4 ilikuwa yetu,tumechanga karata zetu vibaya.....kuwa nje ya top 4 inasumbua sana kwenye usajili maana wachezaji wengi wanapenda kucheza Champions league
 
Arteta aliipokea timu ikiwa Europa. Akaitoa nje ya top six ila ikarudi Europa kwa mlango wa nyuma. Kisha akashindwa kuifikisha Europa, CL na hata conference league.

Na msimu huu ameirudisha tena Europa.

Huku kikosi chake kikipoteza mechi 5 ambazo alitakiwa kushinda moja ili aende CL.

Tuhesabu tumefanikiwa? Anafaa kubaki kua kocha?

Mimi nafikiri anafaa lakini kuna maeneo anatakiwa kujirekebisha haswa katika kusajili, priority na namna anavyohandle wachezaji.

Tukianza katika usajili;

- Baada ya kua kocha akaazimia kupunguza upana wa kikosi ambacho kiliongeza wage bill ila performance ilikua hovyo. Akaachana na wachezaji wengine kwa mkopo, wengine free, wengine wakauzwa. Wakaondoka wakina Sead, Ozil, Iwobi, Auba, Bellerin, Guendouz, Torreira, Saliba, Mari, Mustafi, Nelson, Niles, n.k.

Kisha kiangazi akasajili Lokonga, Partey, Tavares, White, Martin, Ramsdale na Tomiyasu. Ilivyofika January akawa ana option ya kumsajili Melo na Kulusevski lakini akaona haina maana waliopo watamaliza msimu.

Ngwe ya pili ilivyofika katikati it was obvious kwamba timu haiwezi survive na Lokonga na Xhaka wakiwa kati ikabidi Elneny apate namba.
Wakati Arteta anakuja alimuambia Elneny hayupo kwenye mipango yake ni goli la Elneny la pre season ndiyo limembakisha Arsenal. Meaning kama asingescore Elneny asingekuepo na tungebaki na Lokonga na Xhaka pekee na tungejikuta tupo chini zaidi ya hapa.

Kisha unakumbuka kwamba amewaachia kwa mkopo Niles, Guendouz na Nelson wana uzoefu kuzidi Lokonga na ingekua sahihi angebaki na angalau wawili. Torreira simsemei sana kwakua alishasema anataka aondoke so isingekua na maana kumlazimisha abaki. So Arteta angeweza kubaki na Guendouz na Niles akamtoa kwa mkopo Nelson na pale kati bado tungekua tuna watu wanaoweza kusimama bila wewe kuhofia.
 
Tuje kwenye priority;

Msimu unapoanza kocha hua ana vipaumbele kwamba msimu huu kikosi changu kitafocus na CL kama kipaumbele namba moja. Namba mbili ni nafasi ya pili mpaka ya nne, namba tatu ni FA na nne ni Carabao. Wakati tunaanza msimu hatukua kwenye mashindano ya nje hivyo vipaumbele vilikua vichache pia.

Hajaweka wazi vipaumbele vilikua nini lakini naamini cha kwanza kilikua kufuzu mashindano ya nje, FA na Carabao. Kwa kumsikiliza CEO ni kwamba tungeenda CL tungekua tume-overachieve, bodi ilitarajia twende Europa, hivyo kipaumbele cha kwanza kakifuzu.

Cha pili na cha tatu tumefeli na ninafikiri tumefeli kwa ajili ya usajili, hivyo Arteta amejichoma mwenyewe kwenye hivi vipaumbele viwili. Na hata hivyo wachezaji hawakuwa wakicheza kama wanamaanisha wanachokitaka, game tuliyotolewa FA ilikua ya hovyo sana. Na ukitazama shida ni nini unaona shida ni kikosi ambacho ni yeye mwenyewe alikitrim na hakujali sana mahitaji.

Kwa kuandika hivi nafikiri msimu ujao ukianza kipaumbele namba moja ni Europa, kisha namba 1 kwenye ligi, FA na Carabao. Usajili tutakaoufanya (kama tutafanya) hapa kiangazi utasema kama kuna vipaumbele vitafikiwa ama la.
 
Handling ya wachezaji

Arteta alimtoa kwa mkopo Guendouz kwakua Guendouz alimwambia mchezaji wa timu pinzani kwamba analipwa pesa nyingi kumzidi. Kwa Arteta huo ni utovu wa nidhamu na alisema anatarajia uact accordingly.
Kwa hoja hii hii ya utovu wa nidhamu Auba akavuliwa kitambaa akalamba benchi, Lacazette akalambishwa benchi katika mechi zaidi ya 5 za mwisho.

Online Arteta wanamuita control freak.

Bellerin akaenda kwa mkopo Betis na inasemwa ni kwavile Arteta ameshindwa kumfanya Bellerin ajiamini. Juzi Bellerin anacheza mechi ya mwisho huko Hispania akawa analia. Kisha akamlambisha benchi Ozil na Pepe.

Hata wakati timu inashindwa Arteta haikumtikisa ilikua kama ameonyesha wewe unakaa benchi ni unakaa benchi. Kwa ajili ya msimamo huu tumepoteza mechi nyingi ambazo unaweza thubutu kusema hatukutakiwa kupoteza.

Simaanishi abembeleze wachezaji ila angalau awe anaweza kuona zaidi ya utovu wa nidhamu wa mchezaji. Siku kadhaa baada ya Guardiola kuchaguliwa kufundisha Barca alisema hana mpango na Deco, Etoo na Gaucho lakini hakuwafukuza kesho yake alikaa nao na kuwatumia kabla hawajaondoka.

Kwanini asingeopt hii njia? Vya kurithi vinazidi?
 
Sasa Arteta Ni kocha sahihi? Ndiyo.

Inexperienced, young ni kama Ferguson alivyofika united kisha akaonekana hafai. Arteta aliipokea timu ambayo Mourinho aliikwepa, hakuna namna kocha mzoefu angekuja Arsenal aliyoiacha Emery.

Timu ambayo haiwezi piga pasi kwenda mbele hiyo siyo timu lakini Arteta ndiyo akaipokea na ndiyo hiyo ameenda nayo Europa. Na ameenda huku msimu huu ligi ikiwa ngumu kuliko misimu miwili nyuma.

Chini yake tumeona timu ikianza kucheza kwa pattern, ikicheza huku inaonyesha ina mpango na goli isipokua ST hakuna. Chini yake pia akiwa na wakina Mustafi na Sokratis Arsenal ikawa miongoni wa timu zenye defense ngumu kutoka kuitwa defense isiyofundishika.

So timu in a big picture is doing fine than ever tangu Wenger aondoke akirekebisha hizo ishu tatu nina uhakika we will be going places.
 
Unashibikiaje timu ambayo n disappointment?? Si uende huko ambako sio disappointment?? Wewe ni matatizo sana. Umekaa kama mke anaeetoa Siri za chumbani kwa mashoga zake. Better shut up
Hehehehe acha nikae kimya sababu msimu umeisha na Arsenal haipo champions league tukutane August sina cha kubishana nonsense nipoteze muda wakati EPL imeisha nilisema Arsenal kwenda champions league hatutapata hyo nafasi sababu ya Management nzima ilivyo sasa mimi na wewe nani alikuwa sahihi?vile vile I am gentleman kubishana na ladies haipendezi
 
Arteta aliipokea timu ikiwa Europa. Akaitoa nje ya top six ila ikarudi Europa kwa mlango wa nyuma. Kisha akashindwa kuifikisha Europa, CL na hata conference league.

Na msimu huu ameirudisha tena Europa.

Huku kikosi chake kikipoteza mechi 5 ambazo alitakiwa kushinda moja ili aende CL.

Tuhesabu tumefanikiwa? Anafaa kubaki kua kocha?

Mimi nafikiri anafaa lakini kuna maeneo anatakiwa kujirekebisha haswa katika kusajili, priority na namna anavyohandle wachezaji.

Tukianza katika usajili;

- Baada ya kua kocha akaazimia kupunguza upana wa kikosi ambacho kiliongeza wage bill ila performance ilikua hovyo. Akaachana na wachezaji wengine kwa mkopo, wengine free, wengine wakauzwa. Wakaondoka wakina Sead, Ozil, Iwobi, Auba, Bellerin, Guendouz, Torreira, Saliba, Mari, Mustafi, Nelson, Niles, n.k.

Kisha kiangazi akasajili Lokonga, Partey, Tavares, White, Martin, Ramsdale na Tomiyasu. Ilivyofika January akawa ana option ya kumsajili Melo na Kulusevski lakini akaona haina maana waliopo watamaliza msimu.

Ngwe ya pili ilivyofika katikati it was obvious kwamba timu haiwezi survive na Lokonga na Xhaka wakiwa kati ikabidi Elneny apate namba.
Wakati Arteta anakuja alimuambia Elneny hayupo kwenye mipango yake ni goli la Elneny la pre season ndiyo limembakisha Arsenal. Meaning kama asingescore Elneny asingekuepo na tungebaki na Lokonga na Xhaka pekee na tungejikuta tupo chini zaidi ya hapa.

Kisha unakumbuka kwamba amewaachia kwa mkopo Niles, Guendouz na Nelson wana uzoefu kuzidi Lokonga na ingekua sahihi angebaki na angalau wawili. Torreira simsemei sana kwakua alishasema anataka aondoke so isingekua na maana kumlazimisha abaki. So Arteta angeweza kubaki na Guendouz na Niles akamtoa kwa mkopo Nelson na pale kati bado tungekua tuna watu wanaoweza kusimama bila wewe kuhofia.
Inasikitisha sana Arsenal leo wakuzungumzia lokonga wakati kipindi Cha nyuma mlikuwa mnawatu wamaana sana Watu kama diaby, song, Nasri, Arshavini, Thomas Rosisky, Carzola na wato hawa mliwasajili kwa pesa za madafu
 
Back
Top Bottom